Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rk seh. ya 6 kur. 15-17
  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?
  • Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Akusudia Kwamba Mwanadamu Aone Shangwe ya Maisha Katika Paradiso
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Dunia?
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Paradiso Inayotajwa Katika Biblia Iko Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Kwa Nini Ni Muhimu Kujua Yaliyotukia Edeni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
rk seh. ya 6 kur. 15-17

Sehemu ya 6

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?

MUNGU aliumba dunia iwe makao yanayowafaa wanadamu. Neno lake linasema: “Mbingu ni mbingu za Yehova, bali dunia amewapa wana wa binadamu.”—Zaburi 115:16.

Kabla ya kumuumba mtu wa kwanza, Adamu, Mungu alichagua sehemu ndogo ya dunia iliyoitwa Edeni na huko akatengeneza bustani nzuri. Maandiko yanasema kwamba mto Efrati na mto Tigri (Hidekeli) ilitoka katika bustani ya Edeni.a Inadhaniwa kwamba bustani ya Edeni ilikuwa katika sehemu ambayo leo ni mashariki mwa Uturuki. Ndiyo, bustani ya Edeni ilikuwa duniani!

Mungu alimuumba Adamu na kumweka katika bustani ya Edeni “ailime na kuitunza.” (Mwanzo 2:15) Baadaye, Mungu akamuumbia Adamu mke—Hawa. Mungu akawaamuru wenzi hao: “Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia na kuitiisha.” (Mwanzo 1:28) Bila shaka, Mungu “hakuiumba [dunia] tu bila sababu, [bali] aliiumba ili ikaliwe na watu.”—Isaya 45:18.

Hata hivyo, Adamu na Hawa walimwasi Mungu kwa kuvunja sheria yake kimakusudi. Hivyo, Mungu akawaondoa kutoka katika bustani ya Edeni. Paradiso ikapotea. Nayo madhara yaliyosababishwa na dhambi ya Adamu yakaendelea. Maandiko yanasema: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.”—Waroma 5:12.

Je, Yehova alitupilia mbali kusudi lake la awali—kwamba dunia iwe paradiso inayokaliwa na watu wenye furaha? Hapana! Mungu anasema: ‘Neno langu linalotoka katika kinywa changu, halitarudi kwangu bila matokeo, bali hakika litatenda yale ambayo yamenipendeza, na hakika litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma.’ (Isaya 55:11) Paradiso itarudishwa duniani!

Maisha katika Paradiso yatakuwa namna gani? Fikiria ahadi za Kimaandiko zinazoonyeshwa katika kurasa mbili zinazofuata.

a Andiko la Mwanzo 2:10-14 husema: “Kulikuwa na mto unaotoka katika Edeni ili kuinywesha bustani maji, na kutoka hapo ukaanza kugawanyika na kuwa vichwa vinne. Jina la ule wa kwanza ni Pishoni . . . jina la mto wa pili ni Gihoni . . . jina la mto wa tatu ni Hidekeli [au, Tigri]; ndio unaoelekea upande wa mashariki wa Ashuru. Na mto wa nne ni Efrati.” Mito miwili ya kwanza haijulikani wala mahali ilipokuwa hapajulikani.

Ungejibu Namna Gani?

  • Ni nini lililokuwa kusudi la awali la Mungu kwa dunia na kwa wanadamu?

  • Tunajuaje kwamba Mungu atatimiza kusudi hilo?

Watu watakavyoishi katika Paradiso

Dunia Itakuwa Paradiso

Wafu watafufuliwa: “Wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka.”—Yohana 5:28, 29.

Uzee hautakuwapo, magonjwa, au kifo: “Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’” (Isaya 33:24) Mungu “atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”—Ufunuo 21:4.

Kutakuwa na chakula kingi kizuri: “Hakika dunia itatoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, atatubariki.”—Zaburi 67:6.

Makao mazuri na kazi yenye kuridhisha: “Hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake . . . Watu wangu waliochaguliwa wataitumia kazi ya mikono yao wenyewe kikamilifu.”—Isaya 65:21, 22.

Hakutakuwa na vita, uhalifu, au jeuri: Yehova “anakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia.” (Zaburi 46:9) “Waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani.” —Methali 2:22.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki