Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/12 uku. 2
  • Wahubirie “Watu wa Namna Zote”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wahubirie “Watu wa Namna Zote”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Broshua—Vifaa Vyenye Thamani kwa Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Kumbuka Kutumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Toa Broshua Ili Ushiriki Tumaini Lako la Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • “Mtolee Mwenye Nyumba Gazeti la Zamani au Broshua Yoyote Inayomfaa”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 1/12 uku. 2

Wahubirie “Watu wa Namna Zote”

1. Wahubiri stadi wanaweza kulinganishwaje na fundi stadi?

1 Fundi stadi huwa na vifaa vingi, na anajua wakati na jinsi ya kutumia kila kifaa. Vivyo hivyo, tuna vifaa mbalimbali vya kutusaidia kutimiza kazi yetu ya kuhubiri. Kwa mfano, broshua zinazozungumzia mambo tofauti-tofauti zimechapishwa ili kutusaidia kuwahubiria “watu wa namna zote.” (1 Kor. 9:22) Nyongeza iliyo katika huduma hii imeorodhesha baadhi ya broshua hizi, inaeleza ni nani wanaokusudiwa kuzisoma, na ina madokezo ya jinsi zinavyoweza kutolewa shambani.

2. Tunaweza kutumia broshua wakati gani katika huduma?

2 Wakati wa Kutumia Broshua: Fundi stadi hutumia kifaa fulani wakati inapofaa kukitumia. Vivyo hivyo, tunaweza kumwachia mtu broshua wakati tunapohisi kwamba atafaidika kwa kuisoma, hata ikiwa broshua hiyo si toleo la mwezi huo. Kwa mfano, ikiwa toleo la mwezi ni kitabu Biblia Inafundisha na tunamhubiria mtu asiye Mkristo ambaye hapendezwi sana na Biblia, huenda ikafaa kumpa broshua inayofaa na kisha kumtolea kitabu Biblia Inafundisha baada ya kumsaidia kusitawisha upendezi.

3. Kwa nini tunapaswa kutumia vifaa vyetu kwa ustadi tunapotoa ushahidi?

3 Biblia inawapongeza watu ambao ni stadi katika kazi yao. (Met. 22:29) Bila shaka, hakuna kazi iliyo ya maana zaidi leo kuliko “kazi takatifu ya habari njema.” (Rom. 15:16) Ili tuwe ‘wafanyakazi wasio na lolote la kuonea aibu,’ tutajitahidi kutumia vifaa vyetu kwa ustadi.—2 Tim. 2:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki