“Mtolee Mwenye Nyumba Gazeti la Zamani au Broshua Yoyote Inayomfaa”
Katika miezi ambayo tunatoa kitabu Biblia Inafundisha na kuanzisha funzo katika ziara ya kwanza, tunatiwa moyo “kutoa gazeti la zamani au broshua yoyote inayofaa” ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu na hakubali kujifunza. Kwa nini?
Broshua na magazeti ya zamani huzungumzia habari mbalimbali za wakati unaofaa. Huenda jambo fulani katika moja ya machapisho hayo likagusa moyo wa mwenye nyumba. Kwa hiyo, unapopanga mkoba wako wa mahubiri, tia ndani broshua nyingi tofauti na nakala za zamani za magazeti yetu. Ikiwa huna magazeti ya zamani, unaweza kuchukua kadhaa kutoka kwa dawati la magazeti. Kisha, ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu Biblia Inafundisha na hakubali kujifunza Biblia, unaweza kumwonyesha magazeti kadhaa au broshua ulizo nazo na kumwomba achukue yanayompendeza. Baadaye, fanya mipango ya kumrudia ili kuchochea upendezi wake. Huenda mwishowe akajifunza Biblia.