Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ba uku. 3
  • Kitabu Kipasacho Kusomwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu Kipasacho Kusomwa
  • Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Kisicho na Kifani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Saidia Wengine Wajifunze Juu ya Yule Mtu Mkuu Zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Kwa Nini Uisome Biblia?
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Unaweza Kupata Wapi Uongozi?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
Pata Habari Zaidi
Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
ba uku. 3

Kitabu Kipasacho Kusomwa

“Biblia haipasi kuchukuliwa kwa uzito.” Ndivyo profesa wa chuo kikuu alivyomwambia mwanamke kijana mwenye kusema mambo waziwazi.

“Je, umepata kuisoma Biblia?” mwanamke huyo akauliza.

Kwa kushtuka, huyo profesa alilazimika kukiri kwamba hakuwa ameisoma.

“Waweza kutoaje usadikisho wenye nguvu juu ya kitabu ambacho hujakisoma kamwe?”

Huyo mwanamke alitoa hoja thabiti. Profesa aliamua kuisoma Biblia kisha atoe maoni juu yayo.

BIBLIA, inayotia ndani maandishi 66, imefafanuliwa kuwa “labda ndio mkusanyo wa vitabu wenye uvutano zaidi katika historia ya kibinadamu.”1 Kwa kweli, imeathiri baadhi ya sanaa, fasihi, na muziki, zilizo kuu kupita zote ulimwenguni. Imekuwa na uvutano mkubwa juu ya sheria. Imesifiwa kwa ajili ya mtindo wayo wa kifasihi na imestahiwa sana na wataalamu wengi. Matokeo yayo juu ya maisha za watu katika matabaka yote ya jamii yamekuwa yenye kina hasa. Imetokeza katika wengi wa wasomaji wayo kiwango chenye kutokeza cha uaminifu-mshikamanifu. Baadhi yao hata wamehatarisha uhai wao ili kuisoma tu.

Wakati uleule, kuna hali ya kutia shaka juu ya Biblia. Kuna watu walio na maoni thabiti juu yayo ingawa wao binafsi hawajaisoma kamwe. Huenda wakakiri thamani yayo ya kifasihi au ya kihistoria, lakini wanataka kujua: Kitabu kilichoandikwa maelfu ya miaka iliyopita chawezaje kuhusu ulimwengu huu wa kisasa? Twaishi katika “enzi ya habari.” Sisi hupata kwa urahisi sana habari za sasa hivi tu juu ya matukio na tekinolojia ya karibuni. Shauri lenye “ustadi” juu ya karibu matatizo yote ya maisha ya kisasa linapatikana kwa urahisi. Je, Biblia yaweza kwa kweli kuwa na habari yenye kutumika leo?

Broshua hii inajaribu kujibu maswali ya aina hiyo. Haikusudiwi kukulazimisha ufuate maoni au itikadi fulani za kidini, bali ina nia ya kuonyesha kwamba kitabu hiki chenye uvutano wa kihistoria, yaani, Biblia, chastahili uchunguzi wako. Ripoti iliyochapishwa mwaka wa 1994 ilionyesha kwamba waelimishaji fulani huona kwa dhati kwamba Biblia imekazwa imara sana katika tamaduni za Magharibi hivi kwamba “mtu yeyote, awe ni mwamini au asiyeamini, ambaye hafahamu mafundisho na masimulizi ya Kibiblia hatakuwa na elimu yoyote ya kitamaduni.”2

Labda, baada ya kusoma yaliyochapishwa humu ndani, utakubali kwamba—mtu awe ni wa kidini au la —Biblia ndiyo, kwa msingi kabisa, kitabu kipasacho kusomwa.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 3]

“Kwa kweli ufahamu wangu wa kiroho unatokana na usomaji wa kitabu.—Kitabu? Ndiyo, nacho ni kitabu cha zamani kilicho sahili, cha waziwazi kama maumbile yenyewe, na cha asili vilevile . . . Na jina la kitabu hiki ndilo kitabu chenyewe tu, Biblia.”—Heinrich Heine, mwandikaji Mjerumani wa karne ya 19.3

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki