Tutajifunza Kitabu Upeo wa Ufunuo Tena
1 Ukurasa wa kichwa kikuu wa kitabu Upeo wa Ufunuo hunukuu Ufunuo 1:3 (NW): “Mwenye furaha ni yeye ambaye husoma kwa sauti kubwa na wale ambao husikia maneno ya unabii huu.” Furaha ya watu wa Yehova leo kwa hakika imezidishwa zaidi kwa matimizo ya siku hizi yaliyo kwenye kitabu cha Biblia cha Ufunuo. Uelewevu wetu wa siku ya kisasa kuhusu hii “siku ya Bwana,” umefafanuliwa katika kitabu Ufunuo Upeo Wao Mtukufu U Karibu! (Ufu. 1:10) Kupitia kujifunza kwacho tumepata ufahamu wenye kina kuhusu matukio ya maana ya ulimwengu, hasa yale yanayohusu milki ya ulimwengu ya dini bandia na kuelekea kwa mataifa kwenye Har–Magedoni na vilevile kushughulika kwa Yehova pamoja na watu wake.
2 Kwa wengi wetu, funzo la kichapo hiki halitakumbusha akili zetu juu ya mambo yaliyofikiriwa wakati uliopita tu bali pia litaimarisha maoni yetu ya kiroho kuhusu matukio ya karibuni yanayoongoza kwenye siku ya Yehova ya ushindi kwa adui zake wote. Maelfu ambao wamejiunga nasi wakati wa miaka miwili au mitatu iliyopita kwa hakika watanufaika kutokana na ufikirio huu wa mara ya pili wa kitabu Upeo wa Ufunuo katika Funzo la Kitabu la Kutaniko.
3 Hakikisha unajitayarisha vema, uwepo, na kushiriki kwa njia yenye maana kila juma, kuanzia Julai 24, 1995. Utathawabishwa kwelikweli na kubarikiwa unapotambua waziwazi zaidi umaana wa matukio yenye kuendelea kwa kufikiria unabii uliorekodiwa katika kitabu cha Ufunuo. Kwa kweli, twahitaji kufikiria kwa uzito habari hiyo, kwa kuwa ni ya wakati wake hasa sasa kuliko wakati wowote. Hebu na tuonee shangwe furaha iliyoahidiwa tunaposoma, kusikiliza, na kutafakari kuhusu unabii huu wenye kusisimua kuhusu nyakati zetu!