Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/94 uku. 6
  • Wasihi Wawe Wafuasi Wake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasihi Wawe Wafuasi Wake
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 12/94 uku. 6

Wasihi Wawe Wafuasi Wake

1 Kwenye 1 Wakorintho 3:6, Paulo aliandika: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.” Paulo alitumia kusababu huku ili kusaidia ndugu zake kuona uhitaji wa kufanya kazi kwa muungano chini ya ukichwa wa Kristo. Kwa njia hii pia aliwasaidia wathamini sehemu muhimu waliyokuwa nayo katika kazi ya maana ya kupanda na kutia maji.

2 Kazi hiyo ya kuokoa uhai italetwa kwenye tamati siku hiihii. Tukiwa Wakristo walio wakfu, twashiriki daraka zito la kusaidia wengine wawe wafuasi wa Yesu. (Mdo. 13:48) Utafuatiaje kupendezwa ulikoweza kuamsha kwa kutumia kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi?

3 Ikiwa unarudi kuzuru mtu aliyekubali kitabu, waweza kusema:

◼ “Tulipoongea mara ya mwisho, tulizungumzia Yesu Kristo alikuwa ni mtu wa aina gani. Nilifurahia kukuachia kile kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ni nini kimekupendeza zaidi kuhusu mafundisho ya Yesu na kuhusu utu wake?” Ruhusu itikio. Fungua sura ya 113, na uzungumzie kielelezo bora zaidi cha Yesu cha unyenyekevu. Soma Wafilipi 2:8 kuonyesha jinsi mtume Paulo aliona mwelekeo wa Yesu wa unyenyekevu. Kisha unaweza kueleza jinsi tunavyoweza kujifunza mengi zaidi kupitia funzo la kawaida la Biblia.

4 Huenda ukapendelea utangulizi huu:

◼ “Tuliongea kuhusu mambo aliyofanya Yesu alipokuwa duniani ambayo yaonyesha anatujali kwelikweli. Unafikiri atafanya nini mwishowe ili apumzishe wale ambao wameteseka sana?” Ruhusu itikio. Fungua ukurasa 133, na upitie maelezo yaliyo kwenye fungu la tano. Fungua kwenye picha iliyo katika ukurasa ufuatao, na ueleze kutakavyokuwa wakati mapenzi ya Mungu yafanywapo duniani kama yalivyo mbinguni. Taja manufaa zitakazopatikana kwa kujifunza mengi zaidi.

5 Ikiwa yaonekana hakuna upendezi wa kutosha kusikiliza, labda unaweza kuanza mazungumzo yako kwa njia hii:

◼ “Nafikiri sote wawili twakubali kwamba watu wengi leo hupatanisha maisha zao na mtu fulani wamwonaye kama kielelezo cha kuigwa. Yesu Kristo ni mtu wa kuigwa aliye bora zaidi. Ningependa kushiriki nawe somo la maana sana nililojua kwa kujifunza kielelezo kilichowekwa na Yesu. [Fungua sura ya 40 katika kitabu Mtu Mkuu Zaidi, na utoe uangalifu kwa somo lenye fadhili la Yesu juu ya rehema.] Hili lilinikumbusha kwa mkazo jinsi ninavyohitaji sana kuonyesha wengine sifa hii.” Soma Mathayo 5:7. Ikiwa sasa kunaonekana kupendezwa kwingi zaidi, toa kitabu au broshua Je! Kweli Mungu Anatujali?

6 Au huenda ukataka kutumia mfikio huu wa moja kwa moja:

◼ “Mara ya mwisho nilipokuwa hapa, tulizungumzia umaana wa kupata ujuzi kuhusu Yesu. Yohana 17:3 husema kwamba ‘kwamaanisha uhai wa milele’ kutwaa ujuzi huo. Twaweza kufanyaje hivyo?” Ruhusu itikio. Endelea kwa kueleza mpango wetu wa kujifunza Biblia na jinsi ya kuutumia kwa manufaa.

7 Paulo asema kwamba mfanya kazi “atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe” wakati wa mavuno. (1 Kor. 3:8) Tukijitahidi wenyewe kwa bidii katika kusaidia wengine wawe wafuasi wa Yesu, thawabu yetu itakuwa kubwa kwa hakika.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki