Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/94 uku. 6
  • Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Saidia Wengine Wajifunze Juu ya Yule Mtu Mkuu Zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Wasihi Wawe Wafuasi Wake
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Kutolea Ushahidi “Watu wa Namna Zote”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 12/94 uku. 6

Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi

1 Kama ilivyorekodiwa kwenye Mathayo 5:14, Yesu aliambia wanafunzi wake: “Ninyi ni nuru ya ulimwengu.” Wafuasi wa Yesu walikuwa waambie watu kila mahali kuhusu Ufalme wa Yehova na uandalizi Wake wenye upendo wa wokovu kupitia Yesu. Tukiwa na agizo hilo akilini, wakati wa mwezi wa Desemba twatazamia kwa hamu kutoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Hapa pana madokezo ambayo huenda ukataka kuyatumia.

2 Baada ya kujijulisha, unaweza kusema yafuatayo kwa maneno yako mwenyewe:

◼ “Wengi wamejiuliza Yesu alikuwa mtu wa aina gani alipokuwa duniani. Wewe unafikiri ni katika njia zipi alikuwa tofauti na wengine? [Ruhusu jibu] Kitabu hiki chenye kusisimua, Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, chasimulia mambo makuu ya maisha na huduma yake, nacho huandaa uelewevu wa ndani kuhusu aina ya mtu aliyokuwa. Baada ya kukisoma, watu fulani huhisi kana kwamba walipata kuwa na fursa ya kushiriki naye kibinafsi, kushiriki mateso yake, na kuangalia huduma yake moja kwa moja.” Elekeza kwenye kielezi cha kwanza katika kitabu, ambacho hukazia kichwa. Kisha fungua kwenye utangulizi, na usome fungu la pili chini ya kichwa kidogo “Faidika kwa Kujifunza Juu Yake.” Itikio likiwa zuri, toa kitabu.

3 Au unaweza kusema jambo kama hili:

◼ “Wakati wa majira haya watu wanamfikiria Yesu. Hata hivyo, kwa sababu mambo mengi sana mabaya yanatokea ulimwenguni pote, wengine huenda wakajiuliza ikiwa kweli Yesu anatujali. Wewe wahisije kuhusu hilo?” Ruhusu jibu. Fungua sura ya 24 ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi, na uzungumzie kifupi sababu ya Yesu kuja duniani. Kisha soma Yohana 15:13, ukikazia upendo wa Yesu kwa wengine wa kuhisiwa moyoni. Kumbuka kuwa na magazeti ya karibuni zaidi, broshua, au trakti inayofaa ili uitoe ikiwa kitabu hakikubaliwi.

4 Hapa pana dokezo jingine:

◼ “Vijana walio wengi wanatafuta watu wenye vielelezo vya kuigwa, lakini ni vigumu kuwapata. Yesu Kristo aliweka kielelezo kikamilifu kwa kila mtu. [Soma 1 Petro 2:21.] Maisha yake yote yalikazia ibada ya Baba yake wa kimbingu. Unafikiri ingekuwaje ikiwa watu wengi zaidi wangejaribu kumwiga yeye?” Ruhusu jibu. Rejezea fungu la tatu kwenye kabla ya ukurasa wa mwisho wa kitabu, ambalo laeleza sifa zake za kipekee. Eleza jinsi kitabu Mtu Mkuu Zaidi kinavyoweza kutusaidia sote tuwe Wakristo bora.

5 Huenda ukataka kutumia jambo kama hili:

◼ “Mtu anapotaja Yesu Kristo, watu wengi humfikiria kuwa ama mtoto ama mwanamume anayeteseka akikaribia kufa. Mawazo yao juu ya Yesu hutia ndani kuzaliwa na kufa kwake tu. Mambo ya ajabu aliyosema na kufanya wakati wa maisha yake mara nyingi hayaonwi. Yale aliyotimiza huathiri kila mtu aliyepata kuishi katika dunia hii. Ndiyo sababu ni muhimu tujifunze mengi tuwezayo juu ya mambo mazuri ajabu aliyofanya kwa ajili yetu.” Soma Yohana 17:3. Fungua ukurasa wa kwanza wa utangulizi wa kitabu Mtu Mkuu Zaidi, na usome fungu la nne. Eleza jinsi kitabu hiki kinavyoweza kupatikana na kutumiwa kwa funzo la kibinafsi.

6 Hakikisha umeweka rekodi ya kupendezwa na maangusho ili kwamba uweze kufuatia kwa kufanya ziara za kurudia. Kukiwa bado kuna wakati, na tutafute kwa bidii watu wenye mioyo ya kufuatia haki na tuwasaidie wawe wafuasi wa Mwokozi wetu, Yesu Kristo.—Mt. 16:24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki