Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/95 uku. 8
  • Yehova Ndiye Muumba Wetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Ndiye Muumba Wetu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwasaidia Wengine Wamheshimu Mfanyi Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kutoa Habari Njema Tukiwa na Mtazamo Chanya
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 6/95 uku. 8

Yehova Ndiye Muumba Wetu

1 Mamilioni ya watu huamini kwamba Mungu aliumba uhai. Wengine wengi huamini mageuzi. Kisha kuna wale wasio na uhakika waamini nini. Kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? ni cha watu wote hao. Kichapo hiki hutoa maelezo yaliyofanyiwa utafiti kamili wa jinsi uhai ulivyoanza na linalomaanisha kwa wakati wetu ujao. Wakati wa Juni, tutakuwa tukitoa kitabu hiki katika Kiingereza. Katika Kiswahili toleo litakuwa kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?

2 Hata watu mashuhuri katika jamii ya kisayansi wamekubali mantiki ya hicho kitabu. Mtafiti mmoja wa kisayansi katika Uholanzi aliandika hivi: “Kwa kweli kitabu hiki kinayazidi matazamio yote. Mfuatano wa mambo yenye kutokezwa kiakili ya sura zile na mifano iliyomo ni mambo yanayopatana na hali ya sasa ya kisayansi hivi kwamba ungeweza kuyakataa tu ikiwa wewe ni kipofu.” Kwa hiyo twaweza kuwa na uhakika kwamba wengine watakithamini kitabu hiki.

3 Unaweza kuchagua kufanya utoaji mfupi kama huu:

◼ Fungua ukurasa wa 6, na useme: “Watu wengi hufikiri kwamba dunia yetu maridadi na uhai uliopo ulitokea kutokana na aksidenti. Wewe wafikiri ni maelezo gani yaliyo ya kiakili kuhusu jinsi vyote hivi vilivyotokea? [Ruhusu itikio.] Uthibitisho mwingi mno wahakikisha simulizi la Biblia juu ya Muumba ambaye si mwenye nguvu tu bali pia atupendaye sana sana. Ndiye Mungu wa kweli, na jina lake ni Yehova.” Soma Zaburi 83:18, na ueleze kifupi jinsi lilivyo kusudi lake kugeuza dunia yote kuwa paradiso. Kwa toleo la Kiswahili waweza kutumia utoaji ulio juu bila marejezeo ya namba ya ukurasa. Habari ya mada ya mageuzi yaweza kupatikana kwenye kurasa 104-109.

4 Ikiwa wataka kufikia sehemu yenye umaana ya utoaji wako, unaweza kusema:

◼ “Je, umepata kujiuliza kuhusu swali hili?” Elekeza kwenye kichwa cha hicho kitabu, fungua ukurasa wa 7, soma maswali yaliyo kwenye fungu la 2, na ueleze kwamba hicho kitabu huandaa majibu yenye kuridhisha kutoka Biblia.

5 Au huenda ukajaribu huu:

◼ “Je, ulipata kujiuliza jinsi dunia ilivyokuja kuwepo? Wengi husisitiza kwamba ni tokeo la ghafula la nadharia. Wewe wafikirije? [Ruhusu itikio.] Biblia hufundisha kwamba Mungu aliumba dunia iwe makao yetu ya milele. Hiyo ni tofauti na sayari zile nyingine katika mfumo wetu wa jua. Kadiri tujuavyo, ndiyo peke yake katika ulimwengu mzima iliyo na maandalizi mengi ya kutegemeza uhai.” Fungua katika fungu la 5 kwenye ukurasa wa 130, na ueleze ni kwa nini dunia lazima iwe ni kazi ya Mfanyizaji Stadi. Katika kitabu Neno la Mungu unaweza kutumia habari fulani kwenye kurasa 99-101, hasa fungu la 7 kwenye ukurasa 101.

6 Mfikio mwingine waweza kuwa jambo linalofanana na hili:

◼ “Watu fulani hufikiri kwamba tuligeuka kutoka watu-nyani. Wao hudai kwamba mababu wetu wa kale walifanana hivi. [Onyesha picha ukurasa wa 89.] Wafikiri nini kuhusu hilo?” Ruhusu itikio. Taja linalosemwa katika fungu la 20, kisha usome Matendo 4:24, linalotambulisha Yehova kuwa Muumba wetu na Mpaji-Uhai. “Kitabu hiki huchunguza nadharia yote ya mageuzi kuhusiana na yaliyoandikwa katika Biblia.” Rejezea kwenye yaliyomo ukurasa wa 5, na utaje vichwa fulani, kama vile vya sura 1, 7, 15, na 19.

7 Kitabu hiki chaweza kuwa baraka kwa watu wenye mioyo minyoofu ambao wanadanganywa na wale wasio na imani katika Yehova na Neno lake. Habari ya uhakika iliyo kwenye kitabu Creation yaweza kusaidia watu kama hao kukuza uthamini kwa Muumba, atujaliye kwa upendo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki