Wasaidie Wale Wasiokuwa na Imani
1 Katika nyakati za ki-siku-hizi, limekuwa jambo la kawaida kuonekana kuwa mwenye elimu na maendeleo katika kufikiri. Filosofia za binadamu na nadharia za kutunga zatukuzwa, ilhali thamani za kiroho zapuuzwa. Watu wenye mioyo minyoofu wanaopendezwa na mambo hakika yaliyo sahili na kweli zinazoeleweka watakubali fursa ya kuchunguza kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? au Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Vitabu hivi vyaweza kusaidia wale wasio na imani. (Rum. 1:19, 20) Hakikisha unafanya ziara za kurudia kwa wote wanaoonyesha kupendezwa.
2 Unaweza kuanza mazungumzo yako kwa njia hii:
◼ “Nina hakika unajua kwamba waelimishaji wengi huunga mkono itikadi ya kwamba familia ya kibinadamu ilipata kuwepo kupitia mageuzi. Hufundisha kwamba kila kitu kipo kupitia aksidenti. Wahisije kuhusu hilo? [Ruhusu itikio.] Wazo hili bado larejezewa kuwa nadharia. Nadharia ni ‘kisio’ au ‘dhana isiyothibitishwa.’ Kwa karne nyingi watu wameamini kwamba dunia ilikuwa tambarare; sasa twajua hiyo ilikuwa dhana ya kipumbavu isiyotegemea mambo hakika. Je, yawezekana iwe hivyo kuhusu nadharia ya mageuzi?” Soma utangulizi kwenye ukurasa wa 4, kisha uzungumzie Isaya 42:5.
3 Ukiwa na Biblia yako karibu, waweza kufungua mazungumzo kwa kusema:
◼ “Tunazuru tena ili kuonyesha ni kwa nini funzo la Biblia ni lenye mafaa kwa nyakati zetu. Watu walio wengi wana Biblia, lakini ni wachache huchukua wakati wa kuisoma. Wengine hutuambia waziwazi kwamba hawana tumaini zaidi tena katika Biblia. Wewe wahisije kuhusu hilo? [Ruhusu itikio.] Mojapo mambo yanayotusadikisha kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililopuliziwa ni utimizo wa unabii walo.” Rejezea Maandiko yaliyo katika fungu 6 kwenye ukurasa 234. Katika kichapo Neno la Mungu fungua kwenye habari katika sura 9.
4 Wazo hili laweza kupata itikio zuri:
◼ “Twaweza kuona urembo na ushuhuda wa ajabu wa hekima katika vitu ambavyo vyatuzunguka kwenye dunia hii. Picha hii yenye kupendeza ya machweo ya jua ni kielelezo kifaacho.” Onyesha kielezi kwenye kurasa 12 na 13. Taja mambo kutoka “Some Things to Think About,” na ueleze jinsi kitabu hiki huandaa majibu yenye kutosheleza maswali muhimu kuhusu ulimwengu wetu.
5 Twaweza kuwa baraka kwa wengine kwa kutumia toleo letu kuwasaidia kupata msingi ufaao wa imani katika Muumba wao.