Toa Utumishi Mtakatifu Usiku na Mchana
1 Tumepewa pendeleo la pekee. Ni lile la kuwa mashahidi wa Yehova. Sisi ni sehemu ya tengenezo la ulimwenguni pote la waeneza evanjeli linalotumiwa na Yehova kutimiza kazi ya kupiga-mbiu ya Ufalme kubwa kupita zote zilizopata kufanywa! (Mk. 13:10) Kwa kufikiria uharaka wa nyakati zetu, je, twashiriki katika kazi hii kikamili iwezekanavyo?
2 Hatujui ni wangapi watakaoitikia kuhubiri kwetu mwishowe. Yehova atuhakikishia kwamba utakuwa “umati mkubwa,” wote ambao watambuliwa kwa ‘kumtolea utumishi mtakatifu usiku na mchana.’ (Ufu. 7:9, 15, NW) Zaidi ya Mashahidi milioni tano ambao tayari wanafanya utumishi wa Mungu si wasikiaji wenye kupendezwa tu, wala wao si wahudhuriaji wa mikutano tu. Wao ni wafanyakazi wanaopiga mbiu ya habari njema ulimwenguni pote!
3 Kila siku, kuna fursa za kumsifu Yehova, ama katika utumishi wa shambani ama kivivi hivi. Wazia ushahidi mkubwa ambao ungetolewa kama kila mmoja wetu angechukua hatua ya kushiriki kweli na mtu mmoja tu kila siku. Uthamini wetu kwa Yehova wapaswa kutusukuma tuseme juu yake kwa idili.—Zab. 92:1, 2.
4 Saidia Wengine Watoe Utumishi Mtakatifu: Yehova aendelea kutubariki kwa ongezeko. (Hag. 2:7) Wakati wa mwaka wa utumishi uliopita katika Afrika Mashariki, wastani wa mafunzo ya Biblia 35,000 yaliongozwa kila mwezi. Mradi wetu wa kujifunza na watu hawa ni kuwasaidia wawe wanafunzi wa Yesu. (Mt. 28:19, 20) Wengi wao tayari wamefanya maendeleo mazuri kwa kuhudhuria mikutano kwa ukawaida. Wameanza kuongea na watu wanaowafahamu “matendo makuu ya Mungu” ambayo wamejifunza. (Mdo. 2:11) Je, wanaweza kualikwa sasa ili washiriki katika huduma ya peupe?
5 Wakati wa Aprili twapaswa kufanya jitihada ya pekee kualika wapya wanaostahili, wajiunge nasi katika utumishi wa shambani. Je, mwanafunzi wako ameonyesha tamaa ya kufanya hivi? Ikiwa ndivyo, je, anatimiza matakwa ya Kimaandiko? (Ona kitabu Huduma Yetu, kurasa 97-99.) Mwanafunzi anapotaka kushiriki katika utumishi wa shambani, zungumza matazamio yake na mwangalizi-msimamizi, atakayepanga ili wazee wawili wachunguze jambo hilo. Mwanafunzi akistahili kuwa mtangazaji asiyebatizwa, mwalike ajiunge nawe shambani. Waangalizi wa utumishi na viongozi wa funzo la kitabu hasa wanapaswa kuwa chonjo kuwasaidia wale ambao huenda wakastahili kuanza kutangaza katika Aprili.
6 Wazazi wanaweza kuchunguza kama watoto wao wanastahili kuwa watangazaji wasiobatizwa. (Zab. 148:12, 13) Mtoto wako akitaka kujieleza mwenyewe katika utumishi wa Ufalme naye ana mwenendo mzuri, unaweza kuwafikia wazee wa halmashauri ya utumishi ili mzungumze hali hiyo. Baada ya kukutana nawe pamoja na mtoto huyo, wazee wawili wataona kama anastahili kuhesabiwa kuwa mtangazaji. Kuna sababu ya kuonea shangwe watoto wanapojiunga nasi katika kumsifu Mungu!
7 Ni Yehova tu anayestahili utumishi wetu mtakatifu. (Luka 4:8) Kila mmoja wetu na atumie pendeleo letu zuri ajabu la kumsifu ‘sana.’—Zab. 109:30; 113:3, linganisha NW.