Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/96 uku. 1
  • Kutimiza Nadhiri Yetu Siku kwa Siku

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutimiza Nadhiri Yetu Siku kwa Siku
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • “Kile Unachoweka Nadhiri, Timiza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kuishi kwa Kupatana na Nadhiri Yako ya Ndoa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 7/96 uku. 1

Kutimiza Nadhiri Yetu Siku kwa Siku

1 Mtunga-zaburi Daudi alichochewa kumtangazia Yehova hivi: ‘Nitaliimbia jina lako daima, ili niondoe nadhiri zangu kila siku.’ (Zab. 61:8) Daudi alijua kwamba kuweka nadhiri ni jambo la kujitolea kabisa. Lakini, yeye alijua pia kwamba ikiwa angeweka nadhiri, alikuwa na wajibu wa kuitimiza. Hata hivyo, alimsifu Yehova kwa fursa aliyokuwa nayo ya kutimiza nadhiri zake siku kwa siku.

2 Tulipojiweka wakfu kwa Yehova, tulinadhiria kwa hiari kufanya mapenzi yake. Tulijikana wenyewe na kufanya kumtumikia Yehova kuwa jambo letu kuu maishani. (Luka 9:23) Hivyo, sisi pia lazima tulipe nadhiri yetu siku kwa siku. (Mhu. 5:4-6) Tangazo letu la peupe lililofanywa wakati wa ubatizo wa maji lazima lionyeshwe katika kigezo cha maisha yetu yote, kwa kuwa twajua kwamba “kwa kinywa [mtu] hukiri hata kupata wokovu.” (Rum. 10:10) Hilo latia ndani kuhubiri habari njema. (Ebr. 13:15) Hali za kibinafsi hutofautiana sana, lakini siku kwa siku sisi sote twaweza kukazia uangalifu umaana wa kushiriki habari njema na wengine.

3 Tokeza Fursa za Kuhubiri Kila Siku: Kushiriki habari njema na mtu mwingine ni jambo lenye shangwe. Ili kufanya hivi kila siku, lazima tutafute fursa za kuhubiri wakati wowote ule ambao hali zetu zaruhusu. Mambo mengi yaliyoonwa yenye kuleta furaha yamefurahiwa na wale ambao wamechukua hatua ya kutoa ushahidi kivivi-hivi kwa watu mmoja-mmoja kazini au shuleni na kwa majirani na wengine wanaokutana nao kila siku. Hata kuandika barua au kutumia simu kwaweza kuwa njia ya kutolea wengine ushahidi. Kutumia kwa manufaa njia zote hizi pamoja na kutenga wakati wa kutoa ushahidi wa mlango kwa mlango kwa ukawaida na kufanya ziara za kurudia zaweza kuongoza kwenye shangwe ya pekee inayotokana na kuongoza funzo la Biblia nyumbani. Naam, kila siku twaweza kutokeza fursa za kuhubiri.

4 Dada mmoja alianza kusoma Kuyachunguza Maandiko Kila Siku wakati wa pumziko lake la kazini. Alimwalika mfanyakazi mwenzake asome andiko la siku pamoja naye, na upesi hilo likaongoza kwenye Funzo la Biblia pamoja na mwanamke huyo. Walijifunza kwa nusu saa kila siku, siku tano kwa juma. Mfanyakazi mwenzao mwingine aliona funzo lao la kila siku. Hatimaye akajitambulisha kuwa ndugu asiyetenda. Akichochewa na bidii ya dada huyo, alimwendea mzee mmoja ili awe ndugu mwenye kutenda tena. Dada huyu alikuwa na uvutano mzuri kwa watu wawili kwa sababu ya kuendelea kwa bidii kutimiza nadhiri yake siku kwa siku.

5 Tunapohamasishwa na moyo unaofurika na uthamini kwa mambo yote mazuri ambayo Yehova ametufanyia, kutimiza nadhiri ya wakfu wetu vizuri tuwezavyo kila siku kutatuletea shangwe na uradhi. Kama mtunga-zaburi, twaweza kutangaza: “Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu, kwa moyo wangu wote, nitalitukuza jina lako milele.”—Zab. 86:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki