Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/97 kur. 3-4
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Afrika Mashariki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Afrika Mashariki
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Upanuzi Wenye Kuendelea Waongeza Uhitaji wa Majumba ya Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Fungu Lako Katika Kujenga kwa Ajili ya Wakati Ujao
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Kudhihirisha Imani kwa Matendo Mema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme—Sehemu Muhimu ya Utumishi Mtakatifu
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 8/97 kur. 3-4

Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Afrika Mashariki

1 Tunapotazama shamba la ulimwenguni pote, inachangamsha kuona maongezeko makubwa yanayoonwa na tengenezo la Yehova la kidunia. Mwaka uliopita katika Marekani peke yake, makutaniko mapya 246 yalifanyizwa, huku kukiwa na jumla ya makutaniko 3,288 yaliyoongezwa ulimwenguni pote. Kukiwa na ongezeko hili lote, haishangazi kuona kwamba kuna uhitaji wa Majumba ya Ufalme zaidi.

2 Ndugu na dada wengi huonyesha bidii na tegemezo lenye kutokeza kwa tengenezo la Yehova kwa kutoa kwa hiari wakati wao na mali zao katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Halmashauri za Ujenzi za Kimkoa 8 zinazofanya kazi katika Afrika Mashariki zinatunza Majumba ya Ufalme 48 yanayojengwa wakati huu. Halmashauri za kimkoa zimekabidhiwa uangalizi wa miradi hii, na kazi zao zathaminiwa. Mpango wote wa ujenzi wa Majumba ya Ufalme unatimizwa kupitia roho ya Kikristo ya kutoa na ya kujidhabihu—kinyume cha roho inayoonyeshwa sana katika ulimwengu.—2 Tim. 3:2, 4.

3 Ili kusaidia katika kufanya Majumba ya Ufalme yawe ya aina moja, Sosaiti imetolea halmashauri za kimkoa michoro ya ramani ya majengo ya Jumba la Ufalme ya kiwango kimoja. Kwa kuongezea huku kwetu tumesitawisha michoro sahili kwa ajili ya makutaniko madogo. Hiyo imesaidia katika usimamizi wenye hekima wa Hazina za Jumba la Ufalme. Wazee kwa msaada wa Halmashauri za Ujenzi za Kimkoa wanafanya uchaguzi wao wenyewe kutokana na michoro hii ya msingi. Kuwa na michoro hii kutatusaidia pia tufikie viwango vinavyofanana, vilivyosawazika vya Majumba ya Ufalme. Makutaniko yanaposhirikiana katika kutegemeza kufanywa kwa Majumba ya Ufalme kuwa ya aina moja, twatazamia kwamba mzigo wa wasanifu-majengo waliojitoa, wahandisi na makontrakta ambao wamejitolea kusaidia utapunguzwa sana.

4 Wajitoleaji Wategemeza Kazi Bora: Sosaiti inatoa shukrani kwa wale wajitoleaji ambao wanasaidia katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Kwa kweli inafurahisha kuona idadi kadhaa ya wajitoleaji wakijitoa wenyewe katika pande zote za ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Mafanikio ya programu hii yanawezekana kwa sababu roho hiyo ya kuwa tayari, ya ukarimu, na ya ushirikiano kwa upande wa wafanyakazi wenye kujitolea, ambao wanadhabihu wakati ambao ungeweza kutumiwa kwa makutaniko yao na familia zao. (Zab. 110:3; Kol. 3:23) Itikio hilo lenye upendo huwafanya wastahili pongezi yetu, uthamini wetu, na tegemezo letu kamili.—Rom. 12:10; Ebr. 13:1.

5 Wote ambao wana sifa ya kustahili kusaidia Halmashauri za Ujenzi za Kimkoa kwa ukawaida wataombwa wakamilishe fomu za Kingdom Hall Volunteer Worker Questionnaire (S-82). Kutaniko litazipeleka kwa halmashauri ya kimkoa, zikionyesha sifa za ustahili na hali ya kupatikana kwa mfanyakazi. Wakati kuna marekebisho katika hali ya mjitoleaji, kama vile anapohama au kuwekwa kuwa mtumishi wa huduma au mzee, fomu mpya zitajazwa bila kukawia na kupelekwa kupitia mwandishi wa kutaniko. Ikiwa mjitoleaji hana sifa ya kustahili tena, wazee wapaswa kujulisha halmashauri ya kimkoa mara moja kwa barua. Fomu zaidi zihitajiwapo, zaweza kuombwa katika fomu ya Kuomba Fasihi ya kila mwezi.

6 Kutunza Gharama za Ujenzi Zikiwa za Kiasi Kidogo: Halmashauri za Ujenzi zapaswa kupanga kuwe na idara ya ununuzi chini ya usimamizi wa mzee mwenye uwezo. Ndugu wanaofanya kazi katika idara hii hushughulika na ununuzi wa bidhaa na kuchunguza ili kuona bei zilizo nafuu kwa ununuzi wa kulinganisha na kujadiliana juu ya bei. Kwa njia hii, azimio laweza kufanywa ili kuona ni bidhaa gani zapasa kutumiwa na vifaa gani vinunuliwe. Wakati wa kujenga Jumba la Ufalme, ndugu wenye sifa ya kustahili katika kutaniko la mahali hapo hualikwa kusaidia katika idara hii.

7 Ili kuhakikisha pesa zitatumiwa kwa uangalifu iwezekanavyo, Halmashauri ya Ujenzi ya Kimkoa itapitia matumizi yote pamoja na halmashauri za kimkoa za kwenu.

8 Kusaidia Uhitaji wa Makutaniko Mengine: Kuna makutaniko ambayo yamepanga kusaidia makutaniko mengine kujenga Majumba ya Ufalme. Makutaniko hayo huenda yakawa yamemaliza kujenga Majumba ya Ufalme yao na mengine hayana mkopo wa kulipa wa Jumba la Ufalme. Usaidizi huo umethaminiwa sana na makutaniko ambayo yangeona ni vigumu kujenga Majumba ya Ufalme yao wenyewe. Twatiwa moyo kuona makutaniko yakiwa na roho ya usawazisho. (2 Kor. 8:12-15) Tungependa kupongeza makutaniko yote ambayo yameonyesha utayari wa kusaidia mengine yawe na Majumba ya Ufalme ambayo yanachangia sana mahudhurio ya juu ya mikutano.

9 Kwa sababu ya uhitaji wenye kuongezeka daima wa Majumba ya Ufalme, kuna uhitaji wa kutumia pesa kwa hekima iwezekanavyo. Twapaswa kutumia pesa vizuri kadiri iwezekanavyo katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme mapya yaliyo na ukubwa wa kadiri na katika kurekebisha yale yaliyoko tayari. Twafurahi kuona kwamba makutaniko yaliyo mengi hulipa kwa ukawaida mikopo yao ya Jumba la Ufalme. Hili hufanya iwezekane kuwa na pesa za kusaidia miradi mingine ya Majumba ya Ufalme.

10 Uhitaji wa Majumba ya Ufalme zaidi katika nchi kadhaa unakaziwa katika 1997 Yearbook. Kwa mfano, Ukrainia inatajwa, ambapo Majumba ya Ufalme 47 yamejengwa kufikia sasa na ujenzi wa mengine 56 unaendelea. Uhitaji katika nchi kama hizo ni dhahiri. Ripoti hiyo yaonyesha: “Majumba ya Ufalme mengi yanahitajiwa katika Urusi. Ongezeko katika idadi ya Mashahidi huko ni ya haraka, lakini karibu asilimia 85 ya makutaniko chini ya ofisi ya tawi ya Urusi hayana mahali pa kudumu pa kukutania. Katika Zimbabwe, ambapo pana makutaniko yapatayo 800, imekuwa lazima kwa mengi ya hayo kukutania nje mahali palipo wazi. Hilo limefanya wapya wengi waache kuhudhuria.” Hali kama hizo ziko katika nchi nyingine za Ulaya Mashariki, Afrika, na Amerika ya Latini.

11 Ijapokuwa upendo wa idadi kubwa ya wanadamu umepoa katika siku hizi za mwisho, watu wa Mungu wanaendelea kuonyesha uthibitisho wa upendo walio nao, wao kwa wao, upendo unaovuka mipaka ya jamii na mipaka ya maeneo. (Mt. 24:12) Kwa kumwiga Baba yetu wa kimbingu, na tuendelee kuonyesha upendo huo kupitia kutegemeza kwetu ujenzi wa Majumba ya Ufalme katika Afrika Mashariki. Kufanya kwetu hivyo kutaleta baraka nyingi za Yehova na kibali chake.—Mal. 3:10; Ebr. 6:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki