Teua Makala za Kuvutia Mapendezi Hususa ya Watu
1 Kama wapiga-mishale ambao hulenga mishale yao kwa uangalifu, wahubiri wengi wa kutaniko na mapainia wanafurahia mafanikio bora kabisa kwa kutumia makala zilizoteuliwa za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kuvutia mapendezi hususa ya watu katika eneo lao. Wao huamua ni akina nani ambao yaelekea zaidi wangependa kusoma makala fulani za magazeti hayo. Wao hufanyaje hivyo?
2 Kwanza wao husoma kila toleo kutoka jalada hadi jalada. Kisha wanajiuliza wenyewe, Ni mtu wa aina gani ambaye angevutiwa na kila toleo? Kisha jitihada hufanywa ya kutembelea watu ambao yaelekea wangependezwa kusoma hiyo makala. Wanapotazamia kwamba toleo mahususi litakubaliwa sana katika eneo lao, wao huagiza mengine zaidi.
3 Magazeti Yetu Yaheshimiwa Sana: Mmoja wa waandikishaji wetu anayefanyia kazi gazeti la kimataifa la Nigeria linalosomwa kwa wingi zaidi alisema hivi kuhusu Amkeni!: “Pongezi kwa gazeti bora zaidi ulimwenguni kuhusu habari mbalimbali.” Msomaji mwenye bidii wa magazeti yetu alisema hivi: “Ni vito vya ajabu vya hekima yenye thamani sana kama nini! Hakuna habari inayonipendeza inayokosa kuzungumziwa mahali fulani katika kurasa za mmojawapo ya [majarida] haya.”
4 Magazeti haya hushughulikia habari mbalimbali, kutia ndani Biblia, matukio ya ulimwengu, mahangaiko ya familia, matatizo ya kijamii, historia, sayansi, maisha ya wanyama na mimea, tukiorodhesha chache tu. Kwa hakika mtu ataelekea zaidi kusoma jambo fulani linapohusu mahitaji yake, hali zake, au kazi yake. Kwa kuwa sisi huongea na watu wengi, kila mmoja wao akiwa na mapendezi yake na matatizo yake mwenyewe mahususi, kuteua makala hasa ziwavutie watu tunaokutana nao ni kwenye matokeo sana.
5 Ona kilichotokea wakati Mashahidi wawili walipomtolea mwandishi wa makala maalum za gazeti la habari, toleo la Amkeni! la Septemba 8, 1996. Yeye aliandika hivi: “Kabla sijapata nafasi ya kusema kwamba sikupendezwa, mmoja wao alisema hivi: ‘Kuna makala inayohusu Wahindi wa Amerika. Twajua kwamba umekuwa ukiandika mengi kuhusu habari hiyo.’” Alichukua gazeti hilo, na wakati wa kiamsha-kinywa, alisoma habari hiyo iliyohusu Wahindi, akikubali baadaye kwamba “ilikuwa bora kabisa” na “iliyofuata haki kabisa.”
6 Ni Nini Ambacho Hupendeza Watu Katika Eneo Lako? Ni nini ambacho umeona katika magazeti miezi ya juzijuzi ambacho huenda kikawavutia wenye duka na watu wafanyao kazi katika eneo lako au jirani zako, wafanyakazi wenzako, au wanadarasa wenzako? Ni nini ambacho kingependeza hasa wanasheria, waelimishaji, washauri wa familia na shule, washauri wa vijana, waandalizi wa huduma za kijamii, na wafanyakazi wa kitiba? Kuwafikiria watu unaohubiria unapochanganua kila toleo, kutakupatia njia bora kabisa za kueneza neno la kweli.
7 Unapopata mtu anayeonyesha kupendezwa kipekee na makala fulani ya Mnara wa Mlinzi au Amkeni! na ambaye anakubali gazeti hilo waweza kusema hivi: “Kutakapokuwa na makala ya wakati ujao ambayo nitahisi ingekupendeza pia, nitafurahi kukuletea nakala moja.” Unaweza kuongeza mtu huyo katika njia yako ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida, ukimrudia kila mara ukiwa na magazeti ya karibuni. Hilo ni sawa na jambo ambalo limekuwa likifanywa katika kupata mwaliko ulio wazi wa kufanya ziara za kurudia kwa watu ambao huenda wakapendezwa hasa na makala fulani zinazopatikana katika magazeti yetu.
8 Uwe na Lengo la Kiroho: Miaka michache iliyopita, mwanamume mwenye kufuatia sana kazi-maisha alipokea gazeti la Amkeni! kuhusu habari iliyompendeza. Hata hivyo, mwanamume huyu mwenye kushikilia dini sana alisoma pia toleo linaloandamana na gazeti hilo, Mnara wa Mlinzi, ambalo lilikuwa na makala iliyomchochea achanganue itikadi yake ya muda mrefu ya Utatu. Miezi sita baadaye alibatizwa! Kwa sababu hiyo, usisite kuhusisha wasomaji wa magazeti yetu katika mazungumzo ya kiroho. Unaweza kutoa broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? na kujitolea kuchukua dakika chache tu kuzungumzia somo moja katika kila ziara kila mara unaporudi ukiwa na magazeti mapya.
9 Fikiria kwa uangalifu ni nani kati ya ziara zako za kurudia na watu wa biashara unaokutana nao ambao yaelekea zaidi wangethamini kuwa na matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kisha jitahidi kwa bidii kuwafikia. Fikia watu wengi uwezavyo ukiwa na majarida haya yenye thamani. Na usisahau kamwe kwamba ujitahidipo kusaidia watu wengi zaidi wasome magazeti yetu, ‘unatupa chakula chako usoni pa maji.’ Baada ya muda, huenda ukapata mafanikio ya kupata wanafunzi wenzako wa wakati ujao.—Mhu. 11:1, 6.