Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/98 uku. 3
  • Una Mipango Gani Likizo Ijayo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Una Mipango Gani Likizo Ijayo?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Mipango Yako ya Desemba Ni Nini?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kupata Faida Zote za Kitheokrasi Desemba Huu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Fuliza Kufuatia Utendaji wa Kitheokrasi Wakati wa Desemba
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Twaa Fursa Utoe Ushahidi Wakati wa Desemba
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 5/98 uku. 3

Una Mipango Gani Likizo Ijayo?

1 Je, si kweli kwamba yaelekea zaidi kwamba tutafikia miradi yetu yenye kustahili ikiwa tutapanga jinsi ifaavyo zaidi kutumia wakati tulio nao? Likizo hutupatia fursa mbalimbali za kusongeza mbele masilahi za kitheokrasi. (Mit. 21:5) Baadhi ya fursa hizi ni zipi?

2 “Njia ya Mungu ya Maisha” Mkusanyiko wa Wilaya, ni mojawapo ya matukio ambayo sisi sote twapaswa kutia ndani ya mipango yetu. Panga uwe na wakati kutoka kazini au shuleni ili uwepo kila siku ya mkusanyiko. Panga mapema vya kutosha mahali pa kulala na jinsi ya kusafiri.

3 Kwa nini usipange kuongeza utendaji wako wa utumishi wa shambani wakati wa likizo? Kufungwa kwa shule hupatia vijana fursa ya kufanya upainia-msaidizi mwezi mmoja au zaidi katika miezi ya likizo. Wengine pia wanaweza kupanga kimbele wafanye upainia-msaidizi katika Agosti, kutakapokuwa na miisho-juma mitano kamili. Mwezi huu wa Agosti, tunapomaliza mwaka wa utumishi, jitihada ya pamoja itafanywa ili kila mtu ashiriki kikamili iwezekanavyo katika huduma.

4 Je, wapanga kusaidia kutaniko la karibu linalohitaji msaada kumaliza eneo lake? Mwangalizi wa mzunguko anaweza kujulisha wazee juu ya mahitaji hayo katika eneo lenu. Au, ikiwa una sifa za ustahili na ungependa kutoa ombi kwa Sosaiti uhubiri eneo lisilohubiriwa mara nyingi au eneo lisilogawiwa mtu, andika kupitia wazee wako. Ikiwa utakuwa ukilikiza mbali na nyumbani, panga uhudhurie mikutano na kushiriki katika utumishi wa shambani pamoja na kutaniko la mahali hapo. Ikiwa utatembelea watu wa jamaa ambao si Mashahidi wa Yehova, tayarisha mapema njia unazoweza kushiriki kweli pamoja nao.

5 Una mipango gani likizo ijayo? Bila shaka wataka kujiburudisha kimwili. Lakini usipuuze fursa za maana zaidi zilizoko za kujiimarisha mwenyewe kiroho kwa kuendelea kutanguliza Ufalme maishani mwako.—Mt. 6:33; Efe. 5:15, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki