Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/90 kur. 7-8
  • Twaa Fursa Utoe Ushahidi Wakati wa Desemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Twaa Fursa Utoe Ushahidi Wakati wa Desemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUNAPOKUWA LIKIZONI
  • UNAPOHUDHURIA MKUSANYIKO
  • UTENDAJI ULIOONGEZEKA MKIWA FAMILIA
  • Fuliza Kufuatia Utendaji wa Kitheokrasi Wakati wa Desemba
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Mipango Yako ya Desemba Ni Nini?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Una Mipango Gani Likizo Ijayo?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Tumia Wakati wa Desemba kwa Hekima
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 11/90 kur. 7-8

Twaa Fursa Utoe Ushahidi Wakati wa Desemba

1 Maandiko hutuhimiza hivi: “Mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Kor. 10:31) Desemba hutupatia fursa za kufanya hilo kwa njia kadhaa.

2 Wengi watachukua likizo wakati wa Desemba. Hata hivyo, hapana mmoja wetu anayepaswa kupuuza kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha hata majira yawe yapi. Kwa hiyo, unapokuwa katika likizo, ukihudhuria mkusanyiko, au wakati wa likizo ya shule, uwe na moyo wa bidii kuwatolea wengine ushahidi. Twaweza kufanyaje hilo?

TUNAPOKUWA LIKIZONI

3 Je! wewe unapanga kutembelea watu wa ukoo mwezi ujao? Walio wengi wetu huonea shangwe kufanya upya vifungo vyetu vya kijamaa. Ikiwa watu wa ukoo wako hawamo katika ukweli, huenda ukaweza kushiriki nao ujumbe wa Ufalme. Ndugu wengi huwa na mafanikio mazuri kwa kungojea kwa saburi mpaka wakati unaofaa ili wawatolee ushahidi watu wa ukoo wao. Kwa njia hiyo, baadhi ya watu wa ukoo wamejifunza ukweli.—Ona Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1990, kurasa 25-7.

4 Ikiwa unapanga kusafiri mbali na nyumbani kwa ajili ya likizo, kwa nini usipange uhudhurie mikutano na kufanya kazi katika utumishi wa shambani na kundi la mahali hapo. Sisi ‘tuna upendo kwa ajili ya ushirika mzima wa ndugu,’ na kufanya kazi katika utumishi wa shambani pamoja nao hutupatia furasa tunufaishwe na ujuzi wao katika ukweli huku tukipata kuwajua vizuri zaidi. (1 Pet. 2:17) Kwa kuhudhuria mikutano na kujitia katika kazi ya kuhubiri unapokuwa likizoni, tunaweza kujinufaisha sisi wenyewe na kuonea shangwe burudisho la kweli pamoja na ndugu zetu.—Mt. 11:28, 29.

UNAPOHUDHURIA MKUSANYIKO

5 Unapohudhuria mkusanyiko, watolee wengine ushahidi. Kuvaa beji kwaweza kuamsha udadisi wa wengine na kutufungulia njia ya kunena nao juu ya ukweli. Tafuta fursa utoe ushahidi unapotua upate petroli, ule chakula katika hoteli, au unapotumia usafiri wa umma. Mazungumzo ya vivi hivi katika hali hizo mara nyingi huleta matokeo mazuri. Hivyo uwe na Biblia yako na fasihi inayofaa karibu, na uwe tayari kutoa ushahidi.

UTENDAJI ULIOONGEZEKA MKIWA FAMILIA

6 Kwa kuwa wengi wetu hatutakuwa shuleni au tutakuwa na likizo kutoka kazi ya kilimwengu mwezi ujao, kwa sababu gani tusitumie wakati zaidi katika huduma ya shambani kwa kufanya painia msaidizi na ‘kupanua’ upendo wetu kwa kufanya kazi pamoja na wengine. Kwa nini usifanye kazi na ndugu wengi iwezekanavyo katika kundi? (2 Kor. 6:11-13) Familia nzima nzima zimetumia Desemba kufanya painia msaidizi pamoja. Hilo limetia nguvu imani yao na kuwafunganisha karibu zaidi na Yehova na mmoja na mwenzake wakiwa familia. Pia, hilo linatia moyo kundi, na wengine huenda wakachochewa kama tokeo wawe na utendaji zaidi.

7 Kwa kawaida Desemba hujawa na utendaji. Kwa sababu mambo mengi sana yaweza kuchukua wakati wetu, tunahitaji kudhamiria kuweka utaratibu mzuri ili tutumie kwa faida zaidi wakati wetu. Kwa kutanguliza mambo ya kiroho sasa, ‘tutaacha taa zetu ziangaze mbele ya watu.’ Kwa kuwa wataona kazi zetu njema, na huenda wakasukumwa wamtukuze Yehova, yote hayo kwa sababu tulitwaa kila fursa kushiriki ukweli na wengine wakati wa Desemba.—Mt. 5:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki