Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/99 uku. 3
  • Azimio Letu—Kufuatia Njia ya Yehova ya Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Azimio Letu—Kufuatia Njia ya Yehova ya Maisha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Endelea Kutembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kaeni Macho, Songeni Mbele kwa Ujasiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Je, Wajinufaisha?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Elimu—Itumie Kumsifu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 3/99 uku. 3

Azimio Letu—Kufuatia Njia ya Yehova ya Maisha

1 Jambo kuu la Mikusanyiko ya “Njia ya Mungu ya Maisha” lilikuwa lile azimio lililokubaliwa katika hotuba ya mwisho. Lilianza na tangazo hili: “Sisi . . . twakubali kwa moyo wote kwamba njia ya Mungu ndiyo njia bora ya maisha.” Kumbuka mambo makuu ya azimio hilo ambayo tuliitikia “NDIYO!”

2 Ni azimio letu kubaki tukiwa safi mbele ya Yehova, bila doa kutokana na ulimwengu. Tutaendelea kutanguliza mapenzi ya Mungu katika maisha yetu. Tukitumia Neno lake, Biblia, likiwa mwongozo wetu, hatutakengeuka kwenda kulia wala kushoto, hivyo tukithibitisha kwamba njia ya Mungu ya maisha ndiyo njia bora kuliko ya ulimwengu.

3 Kwa ujumla ulimwengu hukosa kuheshimu njia ya Mungu ya maisha nao huvuna matokeo yake. (Yer. 10:23) Kwa hiyo, lazima twendelee kufundishwa na Mfunzi wetu Mtukufu, Yehova asemaye: “Njia ni hii, ifuateni.” (Isa. 30:21) Njia ya Yehova ya maisha, kama ilivyoonyeshwa katika Maandiko, ni bora katika kila namna. Ili tufuatie njia hiyo, ni lazima tutumie kwa manufaa yale yote ambayo Yehova hutufundisha.

4 Programu Bora ya Ufundishaji ya Yehova: Yehova hutufundisha kusudi halisi la uhai na jinsi ya kutumia maisha zetu ili kupata manufaa bora. Yeye hutufundisha jinsi ya kuboresha hali ya maisha zetu kiakili, kiadili, na kiroho. Hutufundisha jinsi ya kuishi kwa amani na ndugu zetu, familia yetu, na binadamu mwenzetu. Yeye hufanya hivyo kupitia kitabu chake cha mafundisho, Biblia, na kupitia tengenezo lake.

5 Mikutano yetu ya kutaniko ni ya maana zaidi katika jambo hili. Tuhudhuriapo na kushiriki katika mikutano yetu yote mitano kwa ukawaida, twapokea mazoezi yenye mambo mengi tukiwa wahudumu wa habari njema na elimu yenye usawaziko ya maisha ya Kikristo. (2 Tim. 3:16, 17) Mfunzi wetu Mtukufu huandaa elimu zaidi ya kitheokrasi kupitia makusanyiko na mikusanyiko. Mradi wetu wapaswa kuwa kutokosa kamwe mkutano hata mmoja au kipindi kimoja ikiwa afya yetu na hali zetu zaturuhusu kuhudhuria.

6 Na twendelee kwa bidii kufuatia njia ya Mungu ya maisha katika siku za usoni, yote kwa sifa ya Yehova na kwa manufaa yetu ya milele!—Isa. 48:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki