Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/99 uku. 1
  • Hubiri Habari Njema kwa Hamu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hubiri Habari Njema kwa Hamu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Dhihirisha Shauku ya Kuzitangaza Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Hubiri na Kutoa Ushahidi Kamili
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Je! Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi Aprili?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 4/99 uku. 1

Hubiri Habari Njema kwa Hamu

1 “Nina hamu sana ya kuwaona nyinyi . . . Kuna hamu upande wangu kuitangaza habari njema kwenu pia.” Hivi ndivyo mtume Paulo alivyojieleza mwanzoni mwa barua yake kwa akina ndugu katika Roma. Kwa nini Paulo alikuwa na hamu ya kuwatembelea? Yeye alisema: “Ili niweze kujipatia baadhi ya matunda miongoni mwenu pia . . . , Kwa maana siaibikii habari njema; kwa kweli, hiyo ni nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu.”—Rom. 1:11-16.

2 Paulo alionyesha hamu hiyohiyo akiongea na wazee wa Efeso. Aliwakumbusha hivi: “Tangu siku ya kwanza niliyokanyaga wilaya ya Asia . . . sikuepuka . . . kuwafundisha nyinyi hadharani na kutoka nyumba hadi nyumba. Lakini nilitoa ushahidi kikamili kwa Wayahudi na Wagiriki pia.” (Mdo. 20:18-21) Katika eneo lake lote alilogawiwa, Paulo alikusudia kueneza habari njema ya wokovu na kupata matunda ya Ufalme. Hiyo ni roho nzuri kama nini kuiga!

3 Huenda tukajiuliza: ‘Je, ninaonyesha hamu ileile ya kutangaza habari njema katika jumuiya yangu? Badala ya kuiona kazi ya kuhubiri kuwa wajibu tu, je, mimi nina hamu ya kushiriki habari njema na watu wengi iwezekanavyo? Je, nimefikiria kwa sala hali zangu za kibinafsi? Je, nimechunguza yote yawezekanayo katika eneo letu, kama vile kuhubiri mlango hadi mlango, barabarani, maeneo ya biashara, kupitia simu iwezekanapo, na vivi hivi?’

4 Shiriki kwa Hamu Wakati wa Aprili: Mwezi wa Aprili ni wakati mzuri wa kuzidisha utendaji wetu wa kibinafsi wa kuhubiri. Takwa la saa lililopunguzwa lapasa kuwezesha wengi kufanya upainia-msaidizi. Labda hali zako zitakuruhusu utumikie ukiwa painia-msaidizi wakati wa Aprili na Mei. Au huenda ukaweza kujiandikisha uwe painia wa kawaida, kwa sababu ya takwa la saa lililorekebishwa. Ikiwa wewe ni mhubiri wa kutaniko, je, waweza kutumia wakati zaidi ya ule wa kawaida katika utumishi mwezi huu na ujao, ukiunga mkono wale ambao wanaweza kupainia? Jambo hilo litaufurahisha moyo wa Yehova!

5 Kama Paulo, wahubiri wote wa Ufalme wapaswa kuendelea kudhihirisha hamu kwa kujitahidi katika kazi ya kuhubiri. Kufanya yote tuwezayo katika huduma kutatuletea shangwe halisi. Paulo alikuwa na shangwe ya namna hii katika utumishi wake mtakatifu. Itakuwa vema kuiga kielelezo chake bora.—Rom. 11:13; 1 Kor. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki