Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/99 uku. 6
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Tudumishe Mahali Petu pa Ibada Katika Hali Nzuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Tunaweza Kusaidiaje Kudumisha Jumba Letu la Ufalme?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Je! Wewe Unastahi Jumba la Ufalme Lenu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Hapa Ni Mahali Petu pa Ibada
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 11/99 uku. 6

Sanduku La Swali

◼ Ni nani mwenye daraka la kusafisha Jumba la Ufalme?

Jumba la Ufalme lililo safi na lenye kuvutia hufanya watu wavutiwe na ujumbe tunaohubiri. (Linganisha 1 Petro 2:12.) Kuliweka jumba likiwa nadhifu ni jambo muhimu, na kila mtu anaweza kushiriki kulisafisha. Hatupaswi kutazamia watu wachache tu wabebe mzigo wote. Mara nyingi, usafi hupangwa kulingana na vikundi vya Funzo la Kitabu la Kutaniko, kiongozi wa funzo au msaidizi wake akichukua uongozi. Katika majumba ambamo zaidi ya kutaniko moja hukutania, wazee watapanga mambo ili makutaniko yote yashiriki kazi ya kulidumisha katika hali nzuri.

Twaweza kutimizaje daraka hilo vizuri zaidi? Jumba la Ufalme lapasa kusafishwa kulingana na ratiba ya kawaida. Vifaa vya kusafishia vyapaswa kuwepo ili vitumiwe kusafishia. Orodha ya mambo yanayohitaji kufanywa yapasa kuandikwa na kubandikwa mahali ambapo wafanyakazi wanaweza kuiangalia wapate mwelekezo. Kwaweza kuwa na orodha mbili tofauti, moja ya kufanya usafi wa ujumla wa haraka baada ya mkutano na nyingine ya kufanya usafi kikamili wa kila juma. Kiongozi wa funzo la kitabu apaswa kuratibu usafi unaofanywa kikamili uwe siku na wakati ambao wote waliogawiwa watapatikana. Nyasi, maua, na vichaka vyapasa kutunzwa pia. Vijia vya kandokando na mahali pa kuegesha magari hapapaswi kuwa na takataka. Kila mwaka usafi kamili wapasa kufanywa, labda kabla tu ya Ukumbusho. Hiyo yaweza kutia ndani kusafisha madirisha na kuta, kung’arisha sakafu, na kufua pazia.

Bila shaka, sisi sote twaweza kufanya mzigo uwe rahisi kwa kutoangusha chingamu au takataka ndani au nje ya jumba. Twaweza kusafisha choo baada ya kukitumia, tukikiacha kikiwa safi kwa ajili ya mtu mwingine. Jihadhari kutovunja vyombo au kuharibu viti. Uwe mwepesi kuona viti vilivyoharibika, matatizo ya mifereji, taa zilizoungua, na kadhalika, na uripoti mambo hayo bila kukawia kwa ndugu anayehusika na udumishaji wa Jumba la Ufalme.

Sisi sote na tuwe tayari kutimiza sehemu yetu. Hiyo hufanya tuwe na nyumba ya ibada yenye kupendeza na inayotutofautisha sisi kuwa watu safi wanaomheshimu Yehova Mungu.—1 Pet. 1:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki