Je! Wewe Unastahi Jumba la Ufalme Lenu?
1 “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja.” (Zab. 133:1) Mikutano kwenye Jumba la Ufalme letu inaandaa fursa ya kuwa na umoja pamoja na ndugu zetu ili tuweze kuchochea mmoja na mwenzake kwenye upendo na kazi nzuri, tukitiana moyo.—Ebr. 10:24, 25.
2 Kwa kuwa Jumba la Ufalme ni la matumizi ya maana hivyo maishani mwetu, je! tunalistahi kweli kweli? Jumba la Ufalme ni kitovu cha ibada ya kweli katika eneo lile. Basi, tunapaswa kulistahi sana. Sisi sote tunapaswa kuhisi uhitaji wa kuliweka safi na katika hali njema. Kuna nyakati ambapo kikundi chetu cha funzo la kitabu kitapewa mgawo wa kusafisha jumba. Ikiwa inawezekana tushiriki katika kazi hiyo, twapaswa tutake kufanya hivyo, hivyo tukionyesha uthamini wetu kwa mahali pa kukutania palipo safi na penye kuvutia.
3 Sisi sote tunaweza kuonyesha upendezi katika Jumba la Ufalme, tuwe tumegawiwa kulisafisha au la. Jinsi gani? Kwa tendo rahisi kama vile kupangusa miguu yetu tunapoingia kwenye jumba ili tusiingize uchafu. Hii ni kweli hasa wakati halianga ni yenye mvua-mvua. Tukiwa na pindi ya kutumia choo, tunaweza kupangusa bakuli la kunawia baada ya kulitumia ili tuliache likiwa safi kwa ajili ya mtu atakayefuata. Wale wanaofanya kazi kwenye kaunta ya fasihi na magazeti wanaweza kuonyesha upendezi wao kwa kuondoa mara moja katoni zilizo tupu. Takataka zote zinapaswa kutupwa kwenye vikapu ambavyo vimewekwa kwa kusudi hilo. Tukiona karatasi au takataka zilizoangushwa sakafuni, tunapaswa kuziokota badala ya kuachia mtu mwingine afanye hivyo. Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1989 ilitoa madokezo juu ya kuweka ubao wa matangazo katika njia safi. Wengine wanapaswa kushirikiana na mwangalizi msimamizi kuhakikisha kwamba shauri hili linafuatwa.—kmSW 1/89 uku. 3.
4 Kanuni zile zile zinatumika tunapohudhuria makusanyiko au mikusanyiko. Mahali pa kusanyiko ni kitovu cha ibada safi, iwe ni mojapo Majumba ya Makusanyiko yetu au mahali pengine, na panapaswa kustahiwa. Tunapaswa kuangalia sikuzote tunapoondoka ili tuhakikishe kwamba hatujaacha takataka yoyote mahali ambapo tulikuwa tukiketi. Tunapaswa kuwa na mtazamo wa kusaidia na tusihisi kwamba wale ambao wamepewa mgawo wa kufanya usafi wapo pale ili wasafishe baada yetu.
KUTUMIA JUMBA KIUSHIRIKA
5 Kwa sababu ya gharama nyingi ya viwanja, Majumba ya Ufalme mengi yanatumiwa na kundi zaidi ya moja. Kila kundi lapaswa kupendezwa na Jumba la Ufalme, likitambua kwamba ni la Yehova na linatumiwa kwa ibada yake. Kwa hiyo kuonyesha staha kwa Jumba la Ufalme hakutii ndani upendo kwa Yehova tu bali pia upendo wetu kwa ajili ya ndugu zetu katika makundi mengine yanayotumia jumba lile.
6 Kwa ukawaida, kusafisha Jumba la Ufalme kunafanywa mara moja kwa juma. Mahali ambapo kundi zaidi ya moja linatumia jumba, ni jambo linalohitajiwa kufanya usafi kidogo baada ya kila mkutano ili kundi litakalotumia jumba baadaye lilipate likiwa lenye kupendeza. Hii inahusu Jumapili pia wakati kundi moja linaingia mara tu baada ya jingine. Ni jambo zuri usafi kidogo ufanywe kadiri wakati unavyoruhusu kwa ajili ya kundi linalofuata. Wakati makundi mengi yanapotumia jumba siku ile ile, linaweza kuwa chafu mwishoni mwa siku ikiwa hakuna mtu anayelitunza.
7 Sawa na vile ‘tunanena mamoja katika nia moja’ kwa habari ya mambo ya kiroho, na tuwe katika umoja pia kwa kuonyesha staha kwa Majumba ya Ufalme yetu.—1 Kor. 1:10.