Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/01 kur. 1-2
  • “Kwa Mungu Mambo Yote Yawezekana”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kwa Mungu Mambo Yote Yawezekana”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • “Haiwezekani!” Neno Hilo Linamaanisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • ‘Hii Habari Njema Itahubiriwa’!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Kwa Uwezo wa Kibinadamu? au kwa Roho ya Mungu?
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Iga Bidii ya Yesu ya Kuhubiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 4/01 kur. 1-2

“Kwa Mungu Mambo Yote Yawezekana”

1 Kazi kuu ya kutaniko la Kikristo ni kuhubiri ujumbe wa Ufalme ulimwenguni kote. (Mt. 24:14) Hiyo ni kazi kubwa sana. Machoni pa watu wengi, yaonekana kana kwamba kazi hiyo yahitaji fedha nyingi kuliko zile tulizo nazo. Kwa wengine, kutimiza kazi hii hakuwezekani kwa sababu tunadhihakiwa, tunapingwa, na kunyanyaswa. (Mt. 24:9; 2 Tim. 3:12) Watu wenye kutilia shaka wanasadiki kwamba kazi hii haiwezi kutimizwa. Hata hivyo, Yesu alisema: “Kwa Mungu mambo yote yawezekana.”—Mt. 19:26.

2 Vielelezo Vinavyofaa Kuigwa: Yesu alianza huduma yake huku akipingwa na ulimwengu wote. Ili kujaribu kumzuia asifanikiwe, wapinzani walimwaibisha kupita kiasi, hatimaye wakamwua kwa njia yenye maumivu makali mno. Lakini mwishowe, Yesu alisema hivi kwa ujasiri: “Mimi nimeushinda ulimwengu.” (Yn. 16:33) Kweli ulikuwa ushindi mkubwa kama nini!

3 Wanafunzi wa Yesu walikuwa na moyo mkuu na bidii hiyohiyo katika huduma ya Kikristo. Wengi wao walicharazwa viboko, wakatiwa gerezani, na hata kuuawa. Ingawa hivyo, walikuwa “wakishangilia kwa sababu walikuwa wamehesabiwa wenye kustahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 5:41) Wakiwa na magumu mengi, walitimiza kazi ambayo ilionekana kwamba haiwezekani ya kuhubiri habari njema “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.”—Mdo. 1:8; Kol. 1:23.

4 Jinsi ya Kufaulu Katika Siku Zetu: Sisi pia tunafanya kazi ya kuhubiri yajapokuwa yale yaonekanayo kuwa magumu yasiyoweza kushindwa. Yajapokuwa marufuku, minyanyaso, vifungo vya gerezani, na vitisho vingine vya jeuri vya kutusimamisha, tunaendelea kufaulu. Hiyo yawezekanaje? “Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema BWANA wa majeshi.” (Zek. 4:6) Kwa kuwa Yehova anatutegemeza, hakuna kitu chochote kiwezacho kusimamisha kazi yetu!—Rom. 8:31.

5 Tunapohubiri, hatuna sababu ya kuona haya au kuogopa au kuhisi hatustahili. (2 Kor. 2:16, 17) Tuna sababu zisizoshindwa za kuendelea mbele katika kueneza habari njema za Ufalme. Tutatimiza “yasiyowezekana” kwa msaada wa Yehova!—Luka 18:27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki