Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako
1 Kabla ya kupaa mbinguni, Yesu aliwaambia wanafunzi wake wafundishe wengine “kushika” mambo yote aliyowaamuru. (Mt. 28:19, 20) Ili mtu ‘ashike’ amri za Kristo, ni lazima habari hiyo imfikie moyoni. (Zab. 119:112) Unawezaje kufikia moyo wa mtu unayemfunza Biblia?
2 Omba Mwelekezo wa Yehova: Kufanya wanafunzi ni kazi ya Mungu. Tunafanikiwa kwa sababu ya baraka zake wala si kwa sababu ya uwezo wetu. (Mdo. 16:14; 1 Kor. 3:7) Hivyo, ni lazima tumwombe Yehova atusaidie kufundisha wengine kweli.—Isa. 50:4.
3 Fahamu Kile Ambacho Mwanafunzi Anaamini: Kujua yale ambayo watu wanaamini na kwa nini wanayaamini kwaweza kutupa ufahamu wa jinsi ya kufikia mioyo yao. Kwa nini mwanafunzi anapenda fundisho fulani? Ni nini kilichomsadikisha kwamba fundisho hilo laweza kuaminiwa? Kujua mambo hayo kwaweza kutusaidia tutumie busara tunapoongea.—Mdo. 17:22, 23.
4 Toa Hoja ya Kimaandiko Yenye Kuleta Maana: Lazima mwanafunzi aielewe kweli. (Mdo. 17:24-31) Lazima tutoe sababu ya maana ya tumaini letu. (1 Pet. 3:15) Hata hivyo, fanya hivyo sikuzote kwa fadhili, na subira.
5 Kazia kwa Kutumia Mifano: Mifano haifanyi iwe rahisi tu kwa mwanafunzi kuelewa bali pia huchochea hisia. Mifano huchochea akili na moyo. Yesu aliitumia mara nyingi. (Mr. 4:33, 34) Bila shaka, ili kuleta mafanikio, mifano inayotumiwa lazima ifaane na yale yanayozungumziwa, na yapaswa kuhusiana na maisha ya mwanafunzi.
6 Onyesha Faida za Kukubali Kweli: Watu hutaka kujua faida za kutumia yale wanayojifunza. Saidia mwanafunzi wako aone hekima ya maneno ya Paulo kwenye 2 Timotheo 3:14-17.
7 Usivunjike moyo watu fulani wasipokubali yale unayofundisha. Si mioyo yote hukubali kweli. (Mt. 13:15) Hata hivyo, watu wengine huja kuwa waamini. (Mdo. 17:32-34) Jitihada zako za kufikia mioyo ya watu kwa habari njema na zisaidie wengine zaidi wakubali na “kushika” yale ambayo Yesu aliamuru.