Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/01 uku. 1
  • Ushirika wa Kikristo Ni Muhimu Kadiri Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ushirika wa Kikristo Ni Muhimu Kadiri Gani?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Ratiba ya Familia—Mikutano ya Kutaniko
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kwa Nini Tunapaswa Kukutanika Pamoja kwa Ajili ya Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Kuthamini Makusanyiko ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Desturi Yako Ni Nini?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 8/01 uku. 1

Ushirika wa Kikristo Ni Muhimu Kadiri Gani?

1 “Mkaa pweke ni uvundo.” Usemi huo unaofanana na wa mshairi mmoja wa karne ya 17 hurudia tu maneno ambayo Biblia husema kuhusu uhitaji wa msingi wa binadamu, yaani ushirika. (Mit. 18:1) Ushirika wetu wa Kikristo hutimiza uhitaji huo. Kwa njia zipi zenye mafaa?

2 Katika Huduma: Faida moja kubwa ni jinsi ambavyo ndugu zetu hutuimarisha na kututegemeza katika huduma yetu ya hadharani. Yesu alituma wanafunzi wake wakiwa “wawili-wawili” ili wahubiri. (Mr. 6:7; Luka 10:1) Kulingana na kielelezo hicho, tunapohubiri na wengine katika utumishi wa shambani, sisi huona ukweli wa Mhubiri 4:9, 10. Tunapohubiri pamoja, imani, utii, na upendo wa wenzetu hututia moyo na kuongeza bidii yetu.

3 Kwa Ajili ya Msaada wa Kibinafsi: Udugu wetu pia ni chanzo cha kitia-moyo na msaada wa kukabiliana na misongo na kukinza vishawishi. Washiriki wenzetu ambao ni Wakristo huenda wakatutajia maandiko ambayo yanatoa ushauri kuhusu mahangaiko yetu. Hata huenda wakasali kwa niaba yetu, kama tunavyosali kwa niaba yao pia. (2 Kor. 1:11) Na kwa kweli, kielelezo chao bora hutuimarisha na kutuchochea kufanya kazi bora.

4 Kwenye Mikutano: Sisi hufurahia baraka za ushirika wa Kikristo tunapohudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida. (Ebr. 10:24, 25) Programu hiyo imejaa mafundisho ya kiroho, na tunapohudhuria mikutano, sisi huwa na uhusiano wa karibu pamoja na waamini wenzetu. Mikutano hiyo hutupa fursa ya kuwasikia ndugu na dada zetu wakieleza imani yao, iwe ni jukwaani au kutoka kwa wasikilizaji. (Rom. 1:12) Kifungo chetu cha ushirika huendelea kuimarika tunaposalimiana na kuongea kabla na baada ya mikutano. Vipindi kama hivyo hutupatia fursa za kusimulia mambo yaliyoonwa yanayoimarisha imani. Nyutu zetu zaathiriwa kwa njia yenye mafaa tunaposhirikiana kwa uhuru na wale wanaompenda Yehova, Neno lake, kazi yake, na watu wake.—Flp. 2:1, 2.

5 Twawahitaji washiriki wetu wa Kikristo. Bila wao, ingekuwa vigumu hata zaidi kutembea kwenye barabara iliyosongamana iongozayo kwenye uhai. Hata hivyo, kwa upendo wao na kitia-moyo chao, twaweza kuendelea hadi ulimwengu mpya mwadilifu wa Yehova.—Mt. 7:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki