Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/01 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 13
  • Juma Linaloanza Agosti 20
  • Juma Linaloanza Agosti 27
  • Juma Linaloanza Septemba 3
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 8/01 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Agosti 13

Wimbo 30

Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Mahali ambapo video zapatikana tia moyo kila mtu aitazame video The New World Society in Action akijitayarisha kuizungumzia kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Agosti 27. Mahali ambapo video hazipatikani makutaniko yatazungumzia Ziara ya Kurudia Ni Nini? Zungumzieni “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.” Tangaza tarehe ya siku ya kusanyiko la pekee linalofuata, na uwasihi wote wahudhurie programu yote. Watie moyo wahubiri waalike watu wenye kupendezwa na wanafunzi wa Biblia.

Dak. 17: “Je, Wataka Kufanya Mengi Zaidi?”a Tia ndani madokezo ya kufanya mengi ili kuwahubiria watu wanaoongea lugha tofauti katika eneo lenu. Toa maelezo mafupi kutoka gazeti Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1997, ukurasa wa 26-29.

Dak. 15: “Weka Starehe Mahali Panapoifaa.” Kiongozi wa funzo la kitabu azungumza pamoja na wenzi wa ndoa baada ya funzo. Anataja kwa fadhili kwamba hivi karibuni hajawaona katika utumishi wa shambani au kwenye mikutano ya mwisho-juma. Wenzi hao wanaeleza kwamba wamekuwa wakienda likizo na wamekuwa na shughuli nyinginezo. Mzee azungumzia mambo makuu yaliyo katika gazeti hilo, akiwasaidia wenzi hao waone kwamba mambo ya kiroho yanapaswa kutangulizwa sikuzote. Wanashukuru kwa vikumbusho hivyo vinavyofaa. Wanakubali kwamba watatanguliza mambo ya maana siku zijazo.—Ona Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2000, ukurasa wa 19-20.

Wimbo 68 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 20

Wimbo 33

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: “Nyinyi Ni ‘Tamasha’!”b Taja visa vya kwenu, ambapo watu wametoa maelezo mazuri juu ya kazi au mwenendo wa Mashahidi wa Yehova.—Ona Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 1998, ukurasa wa 10, na Januari 15, 1999, ukurasa wa 32.

Dak. 22: “Kuwa na Adabu Nzuri Ni Sifa ya Watu wa Mungu.” Mzee atoa hotuba ya dakika tano inayohusu fungu la 1-5. Kisha azungumzia sehemu iliyobaki jukwaani pamoja na mzee mwingine na mtumishi wa huduma. Wanazungumza jinsi ya kushinda mazoea yasiyofaa ambayo hukengeusha fikira mikutanoni na kupunguza manufaa tunayopokea. Wanakazia jinsi ushirika wetu na wengine unavyotia moyo sana tunapoonyesha kwamba tunawajali wengine.—Flp. 2:4.

Wimbo 72 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 27

Wimbo 40

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Agosti. Simulia kifupi dokezo moja au mawili ya jinsi ambavyo kitabu Mtu Mkuu Zaidi kinaweza kutolewa shambani mwezi wa Septemba.—Ona mifano katika Huduma Yetu ya Ufalme, Juni 1998, ukurasa wa 8, na Desemba 1994, ukurasa wa 6.

Dak. 10: Mahitaji ya kwenu. Pia zungumzia “Tenga Wakati wa Kutoa Magazeti.”

Dak. 25: Ziara ya Kurudia Ni Nini? Tia moyo watu waripoti kwa usahihi ziara zote za kurudia zinazofanywa. Ona kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu ukurasa wa 102-104. Mahali ambapo video zapatikana zungumzieni “Kutazama Historia ya The New World Society in Action.” Mazungumzo na wasikilizaji pamoja na mahojiano. Baada ya kuzungumzia maswali, hoji wowote ambao waliona filamu ya awali au ambao walihudhuria mikusanyiko ya kimataifa ya mwaka wa 1950. Waambie wasimulie kile wanachokumbuka juu ya matukio hayo, jinsi yalivyowaathiri kiroho, na usadikisho wao kwamba hili ni tengenezo la Yehova. Mwezi wa Oktoba tutazungumzia video United by Divine Teaching.

Wimbo 74 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 3

Wimbo 80

Dak. 8: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 17: “Ushirika wa Kikristo Ni Muhimu Kadiri Gani?”c Tia ndani maelezo yaliyo chini ya kichwa kidogo “Kupitia Kutaniko” katika Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1996, ukurasa wa 22.

Dak. 20: Mtu Akisema. Mazungumzo na maonyesho. Katika huduma, watu wanaposema mambo kadhaa au kuuliza maswali tusiyotazamia, twapaswa kujitahidi kuyajibu badala ya kuongea juu ya habari nyingine au kukatisha mazungumzo hayo. Kitabu Kutoa Sababu kitakuwa chenye msaada sikuzote kwa upande huu. Taja baadhi ya maelezo ya kawaida, na upange wahubiri watoe onyesho la jinsi ya kujibu wakitumia maelezo yaliyo katika kitabu Kutoa Sababu. Kwa mfano: ‘Mimi sina itikadi na Mungu.’ (ukurasa wa 223-224) ‘Kwa nini ninyi watu hamshiriki katika jitihada za kuboresha jumuiya iwe na hali bora?’ (ukurasa wa 187-188) ‘Si kitu wewe ni wa kanisa gani.’ (ukurasa wa 77) Tia moyo wote watumie sehemu hii ya kitabu Kutoa Sababu wakati mazungumzo yasiyotazamiwa yanapotokea kwenye huduma.

Wimbo 121 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki