Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/01 uku. 8
  • Je, Wataka Kufanya Mengi Zaidi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wataka Kufanya Mengi Zaidi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Panua Hazina Yako ya Utumishi wa Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 8/01 uku. 8

Je, Wataka Kufanya Mengi Zaidi?

1 Yesu aliulinganisha Ufalme na hazina zenye thamani. (Mt. 13:44-46) Kazi ya kueneza habari za Ufalme pia ni hazina yenye thamani. Huduma hii yastahili kutangulizwa zaidi ya mambo mengine maishani mwetu, hata kama twahitaji kujinyima mambo kadhaa ili kuifanya. (Mt. 6:19-21) Je, wataka kufanya mengi katika utumishi wa Ufalme?

2 Fikiria Mambo Haya Muhimu: Mambo kadhaa ni ya lazima ili kupanua huduma yetu: (1) kuazimia kutanguliza masilahi ya Ufalme kwanza maishani (Mt. 6:33); (2) kudhihirisha imani na kumtegemea Yehova (2 Kor. 4:1, 7); (3) kutafuta msaada wa Mungu kupitia sala ya kutoka moyoni na yenye kuendelea (Luka 11:8-10); (4) kutenda kulingana na sala zetu.—Yak. 2:14, 17.

3 Njia za Kupanua Huduma Yetu: Sisi sote twaweza kuweka mradi wa kuhubiri kwa ukawaida kila mwezi. Lakini je, umefikiria pia kutafuta fursa ya kutoa ushahidi wa vivi hivi, kujitahidi kufanya mazungumzo yako yawe yenye maana zaidi, kufanya ziara zako za kurudia ziwe na matokeo zaidi, na kujitahidi kuongoza mafunzo ya Biblia yanayofanya maendeleo? Je, huenda ukaweza kufanya upainia-msaidizi au wa kawaida au kutumikia mahali palipo na uhitaji mkubwa zaidi? Ikiwa wewe ni ndugu aliyebatizwa, je, unaweza kufikia kuwa mtumishi wa huduma au mzee? (1 Tim. 3:1, 10) Je, waweza kupanua huduma yako kwa kuomba kutumikia katika Betheli au kwenda kwenye Shule ya Mazoezi ya Kihuduma?—Luka 10:2.

4 Ndugu ambaye alikuwa akifanya kazi ya kimwili ya wakati wote na pia kutumia wakati mwingi zaidi katika michezo alitiwa moyo awe painia wa kawaida. Alianza kufanya upainia-msaidizi kisha akarekebisha hali zake ili aingie katika huduma ya wakati wote. Baadaye alihudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, ambayo ilimsaidia ajitayarishe kwa ajili ya mgawo wake wa sasa akiwa mwangalizi wa mzunguko. Yeye ni mwenye furaha sana kwamba alikubali kitia-moyo hicho alichopokea. Ana uhakika kwamba amepata furaha zaidi kwa sababu ya kuamua kufanya mengi katika utumishi wa Ufalme.

5 Yehova hubariki wale wanaojitolea. (Isa. 6:8) Usiache kitu chochote kikuzuie kupanua huduma yako na kufurahia uradhi zaidi na burudisho vilevile.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki