Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 15
“Ni jambo gani lingehitajiwa ili kufanya ulimwengu uwe mahali pazuri na penye furaha zaidi? [Ngoja jibu.] Mwanadamu amejaribu aina nyingi za serikali ili kuboresha hali. Lakini ona jinsi ambavyo Mungu anaona jambo hilo. [Soma Yeremia 10:23.] Makala hii yaonyesha ‘Jinsi Ulimwengu Wenye Furaha Utakavyotokea,’ ikionyesha jinsi jambo hilo litakavyotimizwa hivi karibuni.”
Amkeni! Okt. 22
“Je, hukubali kwamba leo watu wanaishi chini ya mkazo sana kuliko zamani? [Ngoja jibu.] Biblia ilitabiri hivyo. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Watu wengi wanaona maisha yakiwa magumu sana hivi kwamba wanakata tamaa. Gazeti hili linatia moyo sana. Laonyesha jinsi ya kupambana na hisia za kukata tamaa na kufanya maisha yawe na kusudi.”
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
Baada ya kutaja habari mbaya uliyosikia, uliza: “Kwa nini watu hutenda mambo maovu hivyo? Sote twapaswa kujua jema na baya, lakini bado watu hutenda maovu. Kwa nini? [Baada ya jibu, soma Ufunuo 12:9.] Gazeti hili laeleza jinsi ya kujilinda kwa kulinda dhamiri zetu.”
Amkeni! Nov. 8
“Yamkini utakubaliana nami kwamba tunaishi katika nyakati za jeuri. [Baada ya jibu, soma 2 Timotheo 3:3.] Mara nyingi matendo ya ‘ukali’ hutokea hata katika familia. Makala hii yenye kichwa, ‘Msaada kwa Wanawake Wanaopigwa,’ ina habari yenye tumaini. Huenda ukajua mtu fulani ambaye unaweza kumwambia habari hii.”