Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 15
“Kwa kuwa Mungu yuko mbinguni, watu husema kwamba haiwezekani kumjua. Je, umewahi kuhisi hivyo? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyoweza kupata ujuzi juu ya Mungu.”
Amkeni! Okt.
“Wengi wetu tumepoteza wapendwa wetu katika kifo. Je, unafikiri kuna mambo yoyote tunayoweza kufanya ili kuwasaidia baada ya wao kufa? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha jibu ambalo linatolewa na Biblia. Pia inaonyesha ahadi hii yenye kufariji.” Soma Yohana 5:28, 29. Kisha mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Leo kuna maoni mengi yenye kupingana kuhusu njia inayofaa zaidi ya kulea watoto. Je, unafikiri kwamba inawezekana kwa wazazi kupata mashauri yenye kutegemeka? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Zaburi 32:8.] Gazeti hili linatoa maagizo kutoka kwenye Biblia kuhusu kuwalea watoto.”
Amkeni! Nov.
“Je, umewahi kujiuliza kwa nini watu wanateseka sana ikiwa kuna Mungu mwenye upendo, haki, na nguvu? [Mruhusu ajibu.] Hebu ona andiko hili linasema nini kuhusu kisababishi cha kuteseka. [Soma 1 Yohana 5:19.] Gazeti hili linaeleza kupitia Biblia kile ambacho Mungu anafanya ili kumaliza kuteseka.”