Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 15
“Maamuzi mengi tunayofanya yana matokeo ya muda mrefu maishani mwetu. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuepuka kufanya maamuzi yasiyofaa? [Ngoja jibu. Kisha soma Methali 3:6.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linaonyesha kanuni tano zinazotegemea Biblia ambazo zinaweza kutusaidia kufanya maamuzi ya hekima.”
Amkeni! Okt. 22
“Je, umesikia kwamba viini vinavyokinza dawa vinazidi kuongezeka? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linaeleza visababishi na linaonyesha jinsi tunavyoweza kujilinda. Linazungumzia pia ahadi ya Biblia kuhusu ulimwengu usio na magonjwa.” Soma andiko la Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Sote tumekatishwa tamaa wakati fulani na mtu ambaye tulimtumaini. Umewahi kujiuliza, ‘Je, ninaweza kumtumaini mtu yeyote?’ [Ngoja jibu. Kisha soma Methali 3:5.] Gazeti hili linaeleza ni kwa nini tunaweza kumtumaini Mungu kabisa. Linazungumzia pia jinsi tunavyoweza kuwatambua watu tunaoweza kuwatumaini.”
Amkeni! Nov. 8
“Sisi hutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mafuta kila siku ya maisha yetu. Je, umewahi kujiuliza maisha yangekuwaje bila bidhaa hizo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi mafuta yalivyopata kuwa muhimu sana katika jamii. Linaeleza pia ni kwa nini hatupaswi kuogopa kwamba siku moja mafuta yatakwisha.”