Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 15
“Watu fulani huamini kwamba wakiwa na pesa nyingi watakuwa na maisha yenye kuridhisha. Je, unafikiri hiyo ni kweli? [Ngoja jibu.] Ona jinsi mwanamume aliyekuwa tajiri sana alivyoandika. [Soma Mhubiri 5:10.] Gazeti hili linazungumzia kanuni zenye thamani kuliko utajiri.”
Amkeni! Okt. 22
“Watu wengi wanaona umuhimu wa kuwazoeza watoto tangu wakiwa wachanga. Je, unaona uhitaji wa kufanya hivyo leo? [Ngoja jibu. Kisha soma Methali 22:6.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia mambo hususa ambayo wazazi wanaweza kufanya ili kuwasaidia watoto wao wawe watu wazima wanyofu na wenye mafanikio.”
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Watu wengi hawaamini kwamba viongozi wa kibinadamu wana uwezo wa kutatua matatizo ya sasa. Je, unafikiri kuna yeyote anayeweza kutimiza yale yaliyotabiriwa katika mistari hii? [Soma Zaburi 72:7, 12, 16. Kisha ungoje jibu.] Gazeti hili linaeleza kiongozi huyo aliyetabiriwa ni nani na atatimiza nini.”
Amkeni! Nov. 8
“Watoto wanahitaji mwongozo ili kukabiliana na mikazo wanayopata leo, sivyo? [Ngoja jibu. Kisha soma Waefeso 6:4.] Gazeti hili linazungumzia maana halisi ya nidhamu. Pia linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kuwaongoza na kuwarekebisha watoto wao bila kuwavunja moyo.”