Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/01 uku. 1
  • Litumie Sawasawa Neno la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Litumie Sawasawa Neno la Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Tumia Lile Neno la Kweli kwa Ustadi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Je, Unalitumia Neno la Mungu Sawasawa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Uwe Stadi Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Tumia kwa Ustadi “Upanga wa Roho”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 12/01 uku. 1

Litumie Sawasawa Neno la Mungu

1 Alipokuwa akihubiria afisa mmoja, “Filipo akafungua kinywa chake na, akianza na Andiko [fulani], akamtangazia habari njema juu ya Yesu.” (Mdo. 8:35) Filipo alikuwa ‘akilitumia sawasawa neno la ile kweli.’ (2 Tim. 2:15) Hata hivyo, waangalizi wasafirio wameona kwamba wahubiri wengi siku hizi hawatumii Biblia sana wanapohubiri. Je, wewe hutumia Biblia katika huduma yako?

2 Neno la Mungu ndilo chanzo cha kila kitu tunachoamini na kufundisha. (2 Tim. 3:16, 17) Ndilo huvuta watu waje kwa Yehova na huwafundisha namna ya kuishi. Ndiyo sababu ni muhimu tutumie Biblia katika huduma yetu badala ya kuzungumzia tu mambo tunayopendezwa nayo. (Ebr. 4:12) Kwa kuwa ni watu wachache wanaojua Biblia, twahitaji kuisoma na kuwaonyesha mwongozo unaofaa unaopatikana ndani yake na wakati ujao ambao inaahidi wanadamu.

3 Soma Biblia Moja kwa Moja: Unaweza kubeba Biblia mkononi mwako au mfukoni mwako. Kisha unapoanza kuzungumza na mtu, unaweza kutoa Biblia bila kumfanya mtu huyo ahisi kwamba unajaribu kumtolea hotuba. Shika Biblia yako kwa namna ambayo msikilizaji wako atafuatana nawe ukiisoma. Labda unaweza kumwomba asome mstari mmoja kwa sauti. Anaweza kuvutiwa zaidi anapoona yale ambayo Biblia inasema badala ya kuyasikia tu kutoka kwako. Bila shaka, ili kumsaidia aelewe maana ya andiko hilo, kazia maneno yanayotokeza mambo makuu.

4 Utoaji wa Andiko Moja: Baada ya kujijulisha, unaweza kusema hivi: “Watu huvitegemea vyanzo tofauti-tofauti ili wapate mwelekezo maishani. Je, wafikiri ni chanzo kipi kilicho na mwongozo bora? [Ngoja ajibu.] Unaonaje maelezo haya? [Soma Mithali 2:6, 7, na ungoje ajibu.] Hekima ya kibinadamu imethibitika kuwa yenye upungufu kabisa, ikifanya watu wengi wakate tamaa. Ingawa hivyo, hekima ya kimungu imethibitika sikuzote kuwa yenye kutegemeka na yenye manufaa.” Kisha mwonyeshe kichapo unachotoa, na ukazie mfano mmoja wa hekima ya Mungu.

5 Yesu alitumia Maandiko kusaidia watu wenye mioyo minyofu. (Luka 24:32) Paulo alithibitisha mambo aliyofunza kwa kutumia Maandiko. (Mdo. 17:2, 3) Uhakika wetu na shangwe yetu katika huduma itaongezeka tunapokuwa na ustadi zaidi katika kulitumia Neno la Mungu sawasawa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki