Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/02 uku. 1
  • Kuhubiri Ufalme Husaidia Kuokoa Uhai!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri Ufalme Husaidia Kuokoa Uhai!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Dumisha Hisi Yako ya Uharaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • ‘Kuleta Habari Njema za Jambo Bora’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 4/02 uku. 1

Kuhubiri Ufalme Husaidia Kuokoa Uhai!

1 Ndiyo kazi muhimu zaidi inayoendelea ulimwenguni hivi sasa. Yehova Mungu, Yesu Kristo, na makumi ya maelfu ya malaika wamekaza fikira zao katika kazi hiyo. Ni kazi gani hiyo, na kwa nini ni muhimu? Ni kazi ya kuhubiri Ufalme, nayo husaidia kuokoa uhai!—Rom. 1:16; 10:13, 14.

2 Huenda watu fulani wakahisi kwamba tungetoa msaada bora kama tungejaribu kuboresha maisha ya wengine ulimwenguni. Wengi wamejiingiza kabisa katika jitihada za kutafuta amani, kuponya magonjwa, au kuboresha uchumi. Lakini ni kazi gani itakayowasaidia watu zaidi?

3 Kazi ya Maana Zaidi: Ni ujumbe wa Ufalme tu unaoeleza kusudi la uhai, sababu ya wanadamu kuteseka, na tumaini pekee lenye kutegemeka la wakati ujao. Habari njema huwezesha watu kuwa rafiki za Yehova na hivyo kupokea “amani ya Mungu izidiyo fikira yote.” (Flp. 4:7) Ni ujumbe wa Ufalme tu unaotoa mwongozo unaofaa ili kusaidia watu wakabiliane na matatizo ya maisha sasa na kueleza jinsi ya kuokolewa wakati ulimwengu mwovu utakapoharibiwa wakati ujao. (1 Yoh. 2:17) Mambo hayo yapaswa kutufanya tujitahidi kwelikweli kuhubiri Ufalme.

4 Kwa mfano: Ni ipi ingekuwa njia bora zaidi ya kusaidia kijiji cha watu waliolala usingizi kutokana na hatari ya bwawa linalokaribia kupasuka na kusababisha mafuriko? Je, ni kwa kupunguza maji ya bwawa hilo lenye kuharibika? Ni kwa kurembesha kijiji kinachokaribia kuharibiwa? La! Lazima wanakijiji waamshwe, waonywe juu ya msiba unaokaribia, na wasaidiwe kukimbia! Wale ambao leo wamelala usingizi wa kiroho wamo katika hatari kubwa. (Luka 21:34-36) Kwa kuwa mfumo huu wa mambo utatoweka hivi karibuni, na tujitahidi kuhubiri kwa uharaka zaidi kadiri tuwezavyo!—2 Tim. 4:2; 2 Pet. 3:11, 12.

5 Endelea na Kazi Hiyo: Na tutafute njia za kuwahubiria watu wengi zaidi wenye mioyo minyofu habari njema—nyumbani mwao, barabarani, kupitia simu, na kwa mahubiri yasiyo rasmi. Kazi ambayo Yehova ametupatia tufanye ndiyo ya maana zaidi. Tukiifanya kwa bidii, ‘tutajiokoa wenyewe na wale watusikilizao pia.’—1 Tim. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki