Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/02 uku. 1
  • Imani Yetu Hutuchochea Kufanya Kazi Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Imani Yetu Hutuchochea Kufanya Kazi Njema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • “Imani Iliyotenganishwa na Matendo Imekufa Kama Mzoga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • “Tupe Imani Zaidi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Imani Yako Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 5/02 uku. 1

Imani Yetu Hutuchochea Kufanya Kazi Njema

1 Imani ilimfanya Noa, Musa, na Rahabu kutenda. Noa alijenga safina. Musa aliacha faida za muda za maisha katika makao ya Farao. Rahabu alificha wapelelezi, akatii maagizo yao, na hivyo akaokoa familia yake. (Ebr. 11:7, 24-26, 31) Imani yetu hutuchochea kufanya kazi gani njema leo?

2 Kuhubiri: Imani hutuchochea kuongea juu ya Mungu wetu wa ajabu na mipango yake ya kuandaa furaha ya milele. (2 Kor. 4:13) Nyakati nyingine huenda tukasita kuhubiri. Lakini ‘tukimweka Yehova mbele yetu daima,’ tutaimarishwa na pia woga utapungua. (Zab. 16:8) Kisha imani yetu hutuchochea kutumia kila pindi inayofaa kuwahubiria habari njema watu wa ukoo, majirani, wanafunzi, na wengine.—Rom. 1:14-16.

3 Kukutanika Pamoja: Kuhudhuria mikutano kwa ukawaida ni kazi nyingine njema inayotokana na imani. Jinsi gani? Huonyesha kuwa tunasadiki kwamba Yesu yuko pamoja nasi kupitia roho takatifu ya Mungu tunapokusanyika kwenye mikutano ya Kikristo. (Mt. 18:20) Huonyesha tamaa yetu ya ‘kusikia lile ambalo roho huyaambia makutaniko.’ (Ufu. 3:6) Tunatii maagizo tunayopokea kwa sababu macho yetu ya imani yanaona kwamba yule anayetufundisha ni Mfundishaji wetu Mkuu, Yehova.—Isa. 30:20.

4 Mambo Tunayochagua: Usadikisho imara wa mambo ya hakika yasiyoonekana hutuchochea kutanguliza mambo ya kiroho maishani mwetu. (Ebr. 11:1) Mara nyingi hiyo hutia ndani kutofuatilia vitu vya kimwili. Kwa mfano, mzee mmoja alikataa kupandishwa cheo kazini kwa sababu kazi hiyo ingemfanya akose mikutano, awe mbali na familia yake, na kuacha huduma ya upainia. Sisi vilevile na tutumaini kabisa uhakikisho wa Biblia kwamba Yehova atawaandalia wale ‘wanaofuliza kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.’—Mt. 6:33.

5 Watu wengine huona jinsi imani inavyofanya kazi katika maisha yetu. Kwa kweli, imani yetu inajulikana ulimwenguni pote. (Rom. 1:8) Kwa hiyo, sisi sote na tuonyeshe kwa kazi zetu njema kwamba imani yetu iko hai.—Yak. 2:26.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki