Kufaidika Kabisa na Kusanyiko la Wilaya la “Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii”
1 Programu Yenye Kuchochea: Tulifurahia programu yenye kuchochea kwelikweli katika kusanyiko letu la wilaya la hivi karibuni! Tulikusanyika kwa kusudi moja, ili tutayarishwe ifaavyo kutangaza Ufalme wa Mungu kwa bidii. Je, wakumbuka jinsi msemaji wa kwanza alivyofafanua usemi “kutangaza”? Je, wakumbuka tulitiwa moyo kufanya utafiti gani katika hotuba “Msiogope kwa Maana Yehova Yu Pamoja Nasi”? Umechunguza masimulizi gani ya maisha kufikia sasa?
2 Mfululizo wa hotuba “Ubora wa Imani Yetu Wajaribiwa na Magumu Mbalimbali” ulitoa sababu tatu kuu ambazo zaonyesha kwa nini Yehova huruhusu mnyanyaso. Je, waweza kuzieleza? Msingi wetu wa Kimaandiko wa kutojiingiza katika siasa ni upi? Tulitiwa moyo kufanya nini ili kujitayarisha kwa ajili ya matatizo yanayotokea kwa sababu ya msimamo wetu wa kutojiingiza katika siasa? Tunamleteaje Yehova sifa tunapovumilia majaribu kwa uaminifu?
3 Ni mambo gani katika drama “Simama Imara Katika Nyakati za Taabu” ambayo hasa yalikuimarisha? Twaweza kuwaje kama Yeremia?
4 Hotuba ya watu wote, “Mandhari ya Ulimwengu Huu Inabadilika,” ilifafanua mabadiliko gani muhimu ambayo yatatukia na yanayoongoza kwenye siku ya Mungu yenye kuogofya? Ulipokuwa ukisikiliza hotuba ya kumalizia, “Zidisheni Kazi Zilizo Bora Mkiwa Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii,” ulihusianishaje habari hiyo na huduma yako mwenyewe?
5 Mambo Makuu ya Kutumia: Kama ilivyoelezwa katika hotuba “Jionyesheni Kuwa Wenye Shukrani,” twaweza kuonyeshaje shukrani zetu kwa Yehova? Katika hotuba ya msingi, “Watangazaji wa Ufalme Wachochewa na Bidii,” tulitiwa moyo kuiga bidii ya nani? Tulitiwa moyo kufanya uchunguzi gani juu yetu wenyewe?
6 Mfululizo wa hotuba “Unabii wa Mika Hutuimarisha Tutembee Katika Jina la Yehova,” ulikazia matakwa gani matatu ambayo lazima tutimize ili tupate kibali cha Yehova? Je, twaweza kutimiza matakwa hayo? (Mika 6:8) Kulingana na hotuba “Dumisha Usafi wa Maadili kwa Kulinda Moyo Wako,” ni lazima tudumu tukiwa safi kiadili katika njia zipi? Hotuba “Jilinde Dhidi ya Udanganyifu” ilituonya tusidanganywe na tusidanganye wengine katika njia zipi?
7 Ni mambo gani yanayokufaa kutokana na mfululizo wa hotuba “Watangazaji wa Ufalme Ambao Huitukuza Huduma Yao” ambayo umeanza kutumia katika huduma yako? Katika hotuba “Maongezi ya Kiroho Hujenga,” tulichunguza Wafilipi 4:8. Andiko hilo latusaidiaje kufanya maongezi yetu kuwa ya kiroho, na twapaswa kufanya hivyo wakati gani?
8 Hotuba “Mtumaini Yehova Kikamili Katika Nyakati za Taabu” ilizungumzia jinsi tunavyoweza kustahimili misiba, magumu ya kiuchumi, afya mbaya, matatizo ya familia, na udhaifu wa muda mrefu. Twaweza kuonyeshaje kwamba twamtumaini Yehova tunapokabiliwa na matatizo hayo?
9 Hazina Mpya za Kiroho: Tulifurahi kupokea kitabu kipya Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Tangazo lililoeleza kusudi la kitabu hicho lilikuathirije? Kwa nini kitatusaidia katika kazi ya kufanya wanafunzi kikiwa kitabu cha pili cha funzo?
10 Kisha tulipokea kitabu chenye kupendeza Mkaribie Yehova. Baadhi ya sehemu zake za pekee ni zipi? Unapenda picha zipi hasa? Je, unamkaribia Yehova zaidi unapoendelea kukisoma? Ni nani wengine wanaoweza kufaidika na kitabu hicho?
11 Kusanyiko la Wilaya la “Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii” lilitupa kitia-moyo cha kiroho tunachohitaji ili kukabiliana na nyakati hizi zilizo ngumu. Ili tufaidike kabisa na mpango huo wa kiroho wa pekee, na tufanye yote tuwezayo kukumbuka yaliyosemwa, tuonyeshe shukrani zetu kwa yale tuliyopokea, na tutumie yale tuliyojifunza. (2 Pet. 3:14) Kufanya hivyo kutatuimarisha tudumishe uaminifu wetu na tuwe watangazaji wa Ufalme wenye bidii tukimwiga Bwana wetu Yesu Kristo, kwa utukufu wa Yehova.—Flp. 1:9-11.