Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/02 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Oktoba 14
  • Juma Linaloanza Oktoba 21
  • Juma Linaloanza Oktoba 28
  • Juma Linaloanza Novemba 4
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 10/02 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Oktoba 14

Wimbo 103

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Mtie moyo kila mtu asome Hesabu sura ya 25, na Insight, Buku la 2, ukurasa wa 419, fungu la 3-5, au Kila Andiko, ukurasa wa 34-35, fungu la 27, 28 na 36 akijitayarishia mazungumzo ya Mkutano wa Utumishi wa juma la Oktoba 28. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15 na Amkeni! la Septemba 22. Katika kila onyesho, tumia njia tofauti ya kujibu kizuia-mazungumzo “Tayari naijua sana kazi yenu.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 20.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Waangalizi wa Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko Wanavyoonyesha Wanapendezwa na Watu Binafsi.” Mazungumzo ya maswali na majibu yatakayoongozwa na mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko. Katika maelezo ya utangulizi, eleza kifupi jinsi ambavyo mpango wa funzo la kitabu ulivyoanzishwa. (jv uku. 237 fu. 4) Panga mapema ili wahubiri wawili au watatu waeleze jinsi ambavyo wamenufaika na upendezi ambao walionyeshwa kupitia Funzo la Kitabu la Kutaniko.

Wimbo 65 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Oktoba 21

Wimbo 206

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 35: “Kufaidika Kabisa na Kusanyiko la Wilaya la ‘Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii.” Ishughulikiwe na kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi. Baada ya utangulizi wa dakika moja, zungumza na wasikilizaji kuhusu programu ya kusanyiko la wilaya, ukitumia maswali yaliyo kwenye makala hiyo. Gawa wakati wako kwa uangalifu. Maelezo mafupi yanaweza kutiwa ndani ili kuwakumbusha wasikilizaji mambo makuu. Inapofaa, uliza wasikilizaji jinsi ambavyo wametumia yale waliyojifunza na waeleze manufaa ambazo wamepata kwa kufanya hivyo.

Wimbo 194 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Oktoba 28

Wimbo 110

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote warudie maandishi yao ya kusanyiko la pekee wakijitayarishia mazungumzo ya Mkutano wa Utumishi katika juma lifuatalo. Wakumbushe wahubiri wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Oktoba. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga dada aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1 na ndugu atoe gazeti la Amkeni! la Oktoba 8. Baada ya kila onyesho, kazia kifupi sehemu inayofaa ya onyesho hilo.

Dak. 12: Habari za Kitheokrasi. Mambo yaliyoonwa ya kwenu. Alika kutaniko lisimulie mambo yaliyoonwa ambayo wamefurahia walipokuwa wakisafiri kwenda na kutoka kusanyikoni, wakiwa huko, au wakihubiri isivyo rasmi kazini, shuleni, sokoni, na kadhalika.

Dak. 25: “Tii Vielelezo vya Kuonya Leo.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee moja kwa moja na mazungumzo pamoja na wasikilizaji ukiuliza kila swali lililo katika makala hiyo.

Wimbo 41 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 4

Wimbo 66

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzieni kifupi madokezo yaliyo kwenye nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 kuhusu kutoa broshua Anataka na kitabu Ujuzi. Toa onyesho la moja ya madokezo hayo.

Dak. 13: Siaibikii Habari Njema. (Waroma 1:16) Kijana mmoja anamwendea baba yake akiwa na tatizo. Kijana huyo hataki ajulikane kuwa yeye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova kwa sababu anahofu kudhihakiwa na marika wake. Baba anamshukuru kijana huyo kwa kuwa mnyofu kuhusu jambo hilo. Anamweleza jinsi ambavyo wakati mwingine Petro alitenda kwa sababu ya mkazo wa marika. (Mt. 26:69-74) Baba anatoa shauri lifuatalo: Hatupaswi kuaibika kamwe kwamba sisi ni Wakristo. (Marko 8:38) Ni muhimu kujitambulisha kuwa Shahidi shuleni. Walimu wengi wakijulishwa kuhusu imani yako wataiheshimu na hawatajaribu kukulazimisha ufanye mambo usiyotaka. Ukifanya hivyo, yaelekea kwamba vijana wasio na kanuni hawatajaribu kukukaza ufanye maovu. Wanashule wengine wataelewa kwa nini hufanyi urafiki pamoja na watu wa jinsia tofauti, hushiriki michezo baada ya masomo, au kushiriki katika shughuli nyingine zinazofanywa baada ya shule. Wakati ukiruhusu, baba na kijana wazungumzie mambo yanayopatikana katika kichwa kidogo “Kujulisha Rasmi Peupe Urafiki Wako Pamoja na Mungu” katika kitabu Vijana Huuliza, ukurasa wa 315-318. Kijana anashukuru kwa ushauri huo mzuri.

Dak. 22: Jitiisheni Wenyewe kwa Mungu—Mpingeni Ibilisi. (Yak. 4:7) Mzee akitumia maswali yaliyopo, anazungumza na wasikilizaji kuhusu programu ya kusanyiko la pekee lililofanywa mwaka wa utumishi uliopita. Alika kutaniko lisimulie jinsi ambavyo limetumia yale waliojifunza. (Sehemu za programu hiyo zaweza kugawanywa mapema.) Kazia sehemu zifuatazo za programu: (1) “Ujitiisho kwa Mungu Katika Ulimwengu Ulio Utumwani.” Kwa nini ni lazima tuwe macho ili tuepuke mitego ya kilimwengu? (2) “Kudhihirisha Ujitiisho kwa Mungu Mkiwa Washiriki wa Familia.” Kwa nini kuna uhitaji mkubwa wa kuimarisha vifungo vya familia katika tengenezo la Yehova? Twaweza kufanyaje hivyo? (3) “Wasaidie Wanafunzi Wapya Wasimame Imara Upande wa Yehova.” Twaweza kusaidiaje wapya washinde vizuizi vya imani yao? (4) “Kinachomaanishwa na Kumpinga Ibilisi.” Ni nini siri ya kufanikiwa kumpinga Ibilisi? Silaha za kiroho zinazofafanuliwa katika Waefeso 6:11-18 zinatulindaje? (w92 5/15 21-23) (5) “Vijana Wanaofanikiwa Kumpinga Yule Mwovu.” Ni baadhi ya hila gani za Shetani ambazo lazima vijana wajilinde dhidi yake? Vijana wanathawabishwaje kwa kujitiisha wenyewe kwa Yehova? (w90 8/1 13-14, fu. 15-17) (6) “Kunufaika Kutokana na Ujitiisho kwa Mungu.” Eleza jinsi Wakristo wanavyojitiisha kwa mamlaka za serikali, waajiri, katika familia, na katika kutaniko la Kikristo. Ni sifa gani zitakazotusaidia kufanya hivyo?

Wimbo 185 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki