Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/02 kur. 3-6
  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2003

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2003
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa vidogo
  • Maagizo
  • RATIBA
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 10/02 kur. 3-6

Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2003

Maagizo

Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaongozwa kulingana na mipango ifuatayo mwaka wa 2003.

VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo [bi7], Biblia ya Union Version, Mnara wa Mlinzi [w], Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi [be], “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Chapa ya 1992) [si], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko (Chapa ya 1989) [rs].

Shule inapaswa kuanza KWA WAKATI, kwa wimbo, sala, na maneno ya kukaribisha, kisha utaratibu ufuatao unapaswa kufuatwa:

SIFA YA USEMI: Dakika 5. Mwangalizi wa shule, mshauri msaidizi, au mzee mwingine anayestahili atazungumzia sifa moja ya usemi akitumia habari kutoka katika kitabu cha Shule ya Huduma. (Katika makutaniko yenye wazee wachache, mtumishi wa huduma anayestahili anaweza kutoa hotuba hiyo.) Kama maagizo mengine hayajatolewa, masanduku yaliyo kwenye kurasa zilizogawiwa kuzungumziwa yanapaswa kutiwa ndani. Mazoezi yanayotiwa ndani ya kila somo hayapaswi kushughulikiwa. Hayo yamekusudiwa kutumiwa na wanafunzi na ili kutoa ushauri faraghani.

HOTUBA NA. 1: Dakika 10. Hotuba hiyo inapaswa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma, na habari zitatolewa katika Mnara wa Mlinzi, Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, au “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Hii ni hotuba ya maagizo ya dakika kumi bila maswali ya kurudia. Kusudi la hotuba halipaswi kuwa kuzungumzia tu habari zilizogawiwa bali jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa maishani zinapaswa kukaziwa, na vilevile habari ambazo hasa zitanufaisha kutaniko. Kichwa cha hotuba kilichoandikwa kwenye ratiba chapaswa kutumiwa. Ndugu wanaogawiwa hotuba hiyo wanatarajiwa kumaliza kwa wakati. Ushauri unaweza kutolewa faraghani inapohitajika.

MAMBO MAKUU YA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee au mtumishi wa huduma anayestahili, anapaswa kutumia dakika sita za kwanza kuonyesha jinsi habari hiyo inavyohusu kutaniko lenu. Anaweza kutoa maelezo kuhusu sehemu yoyote ya usomaji wa Biblia wa juma hilo, kwa kuwa ndugu anayetoa hotuba Na. 2 hatatoa maelezo juu ya mistari anayosoma. Maelezo hayo hayapasi kuwa tu muhtasari wa usomaji wa Biblia. Lengo kuu ni kuwasaidia wasikilizaji kuelewa kwa nini habari hiyo ni yenye faida na jinsi inavyotufaidi. Kisha, msemaji atatumia dakika nne kuwaomba wasikilizaji washiriki kwa kutoa maelezo mafupi (yasiyozidi nusu dakika) juu ya maswali haya mawili: “Uliona nini katika usomaji wa Biblia wa juma hili kitakachokusaidia katika huduma yako au maishani mwako?” na “Ni nini kilichoimarisha imani yako na kuzidisha uthamini wako kwa Yehova?” Kisha mwangalizi wa shule atawaruhusu wanafunzi watakaotoa hotuba katika shule ya pili na ya tatu kuondoka.

HOTUBA NA. 2: Dakika 4. Ndugu anapaswa kugawiwa usomaji huu. Kwa kawaida sehemu fulani ya Biblia itasomwa. Mara moja kwa mwezi sehemu fulani katika Mnara wa Mlinzi itasomwa. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari aliyogawiwa bila kutoa utangulizi wala maneno ya kumalizia. Sehemu zilizoratibiwa kusomwa hazitakuwa zenye urefu mmoja kila juma, lakini sehemu zote zinapaswa kusomwa kwa dakika nne au chini ya dakika nne. Mwangalizi wa shule anapaswa kuchunguza habari kabla ya kuigawia msomaji, ili kuhakikisha kwamba habari inafaa umri na uwezo wa wanafunzi. Mwangalizi wa shule hupendezwa hasa kuwasaidia wanafunzi kusoma kwa njia ya kueleweka, kwa ufasaha, kukazia maana kwa njia inayofaa, kuwa na ubadilifu wa sauti, kutua kwa njia inayofaa, na kusoma kwa njia ambayo watu huongea kwa kawaida.

HOTUBA NA. 3: Dakika 5. Dada atagawiwa hotuba hiyo. Wanafunzi wanaogawiwa hotuba hiyo watachagua kikao au wataonyeshwa kikao cha kutumiwa katika orodha kwenye ukurasa wa 82 katika kitabu cha Shule ya Huduma. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa katika ratiba na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani katika eneo la kutaniko lao. Iwapo vichapo vya kutumiwa havijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi kufanya utafiti wa habari hiyo katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Wanafunzi wapya wanapaswa kugawiwa hotuba zenye marejezo ya vichapo vya kutumia. Mwangalizi wa shule hupendezwa hasa kuona jinsi mwanafunzi anavyofafanua habari hiyo na jinsi anavyomsaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na kuelewa mambo makuu. Wanafunzi wanaogawiwa hotuba hiyo wanapaswa kujua kusoma. Mwangalizi wa shule atateua msaidizi mmoja.

HOTUBA NA. 4: Dakika 5. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa katika ratiba. Kama vichapo vya kutumiwa havijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi kufanya utafiti kuhusu habari hii katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Ndugu anapogawiwa hotuba hiyo, anaweza kuitayarisha ili ifae wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapogawiwa hotuba hiyo, inapaswa kutolewa siku zote jinsi Hotuba Na. 3 inavyotolewa. Tafadhali ona kwamba habari zenye nyota zapaswa kugawiwa ndugu pekee na kutolewa kama hotuba bila msaidizi.

WAKATI: Hotuba na maelezo ya mshauri hayapaswi kamwe kupitisha wakati uliowekwa. Wanafunzi wanaotoa hotuba Na. 2 hadi 4 wanapaswa kukatizwa kwa upole muda wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa hotuba juu ya sifa ya usemi, Hotuba Na. 1, au mambo makuu ya usomaji wa Biblia, wanapaswa kushauriwa faraghani wakipitisha wakati uliowekwa. Wote wanapaswa kuchunga wakati vizuri. Programu nzima: Dakika 45, mbali na wimbo na sala.

USHAURI: Dakika 1. Mwangalizi wa shule atatumia muda usiozidi dakika moja kutoa maelezo yanayojenga kuhusu sehemu ya hotuba inayostahili kusifiwa. Lengo lake si la kumpongeza tu, bali, kuonyesha ni kwa nini jambo fulani katika hotuba lilikuwa zuri. Kulingana na uhitaji wa kila mwanafunzi, ushauri unaweza kutolewa baada ya mkutano au wakati mwingine ili kumsaidia kufanya maendeleo.

MSHAURI MSAIDIZI: Mzee mwingine mwenye uwezo mbali na mwangalizi wa shule akipatikana, baraza la wazee linaweza kumteua na kumweka kuwa mshauri msaidizi. Daraka lake litakuwa kuwashauri akina ndugu wanaoshughulikia Hotuba Na. 1 na mambo makuu ya usomaji wa Biblia, wanapohitaji ushauri. Si lazima awashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo. Utaratibu huo utafuatwa katika mwaka wa 2003 na huenda ukarekebishwa baada ya hapo.

FOMU YA MASHAURI: (Katika kitabu cha shule)

PITIO LA MASWALI NA MAJIBU: Dakika 30. Kila baada ya miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza pitio la maswali na majibu. Sehemu hiyo itafanywa baada ya hotuba juu ya sifa ya usemi na mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama ilivyoorodheshwa hapo juu. Pitio hilo litahusisha habari zilizozungumziwa katika shule katika miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la pitio.

RATIBA

Jan. 6 Usomaji wa Biblia: Mathayo 1-6 Wimbo 91

Sifa ya Usemi: Karibu Kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (be uku. 5¶ 1–uku. 8 ¶ 1)

Na. 1: Furahia Neno la Mungu (be uku. 9 ¶ 1-5)

Na. 2: Mathayo 4:1-22

Na. 3: Ishara za Siku za Mwisho Huwaathirije Wakristo wa Kweli? (rs uku. 301¶1-2)

Na. 4: Yesu Anafanya Nini Wakati Huu?

Jan. 13 Usomaji wa Biblia: Mathayo 7-11 Wimbo 40

Sifa ya Usemi: Soma Biblia Kila Siku (be uku. 10 ¶ 1−uku. 12 ¶ 3)

Na. 1: ‘Kimbieni kwa Njia Hiyo’ (w01 1/1 uku. 28-31)

Na. 2: Mathayo 9:9-31

Na. 3: Kwa Nini Tunawahubiria Wengine?

Na. 4: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Husema Kwamba Siku za Mwisho Zilianza Mwaka wa 1914? (rs uku. 302¶ 1-4)

Jan. 20 Usomaji wa Biblia: Mathayo 12-15 Wimbo 133

Sifa ya Usemi: Kusoma kwa Usahihi (be uku. 83 ¶ 1-5)

Na. 1: Unaweza Kukabiliana na Kivunja-Moyo! (w01 2/1 uku. 20-23)

Na. 2: Mathayo 13:1-23

Na. 3: Je! Yeyote Atapata Kuishi Duniani Baada ya Mwisho wa Ulimwengu Uliopo? (rs uku. 303 ¶ 1-4)

Na. 4: Je, Mungu Hubadilika?

Jan. 27 Usomaji wa Biblia: Mathayo 16-21 Wimbo 129

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kusoma kwa Usahihi (be uku. 84 ¶ 1–uku. 85 ¶ 3)

Na. 1: Wakati Unapita Haraka Sana (si uku. 278 ¶ 1–uku. 279 ¶ 6)

Na. 2: w01 1/15 uku. 20 ¶ 20–uku. 21 ¶ 24

Na. 3: Ni Nini Kitakacholeta Umoja Ulimwenguni?

Na. 4: Kwa Nini Mungu Anaruhusu Wakati Mwingi Sana Upite Kabla ya Kuharibu Waovu? (rs uku. 303 ¶ 5–uku. 304 ¶ 2)

Feb. 3 Usomaji wa Biblia: Mathayo 22-25 Wimbo 139

Sifa ya Usemi: Kusema kwa Njia Inayoeleweka Wazi (be uku. 86 ¶ 1-6)

Na. 1: ‘Kazia Uangalifu Jinsi Unavyosikiliza’ (be uku. 13 ¶ 1–uku. 14 ¶ 5)

Na. 2: Mathayo 22:15-40

Na. 3: Jinsi Tunavyojua Kwamba Ishara Hutimizwa Katika Wakati Huu Wetu (rs uku. 304 ¶ 4–uku. 305 ¶ 1)

Na. 4: Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara Ni Nani?

Feb. 10 Usomaji wa Biblia: Mathayo 26-28 Wimbo 27

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kusema kwa Njia Inayoeleweka Wazi (be uku. 87 ¶ 1–uku. 88 ¶ 3)

Na. 1: Jinsi ya Kupata Furaha ya Kweli (w01 3/1 uku. 4-7)

Na. 2: Mathayo 26:6-30

Na. 3: Kile Kinachofanya Nisitumie Dawa za Kulevya

Na. 4: Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai wa Kibinadamu? (rs uku. 341 ¶ 4–uku. 342 ¶ 4)

Feb. 17 Usomaji wa Biblia: Marko 1-4 Wimbo 137

Sifa ya Usemi: Matamshi Mazuri—Mambo ya Kufikiria (be uku. 89 ¶ 1–uku. 90 ¶ 2)

Na. 1: Viishara vya Wakati Vilivyotumiwa Nyakati za Biblia (si uku. 279 ¶ 7–uku. 280 ¶ 13)

Na. 2: w01 2/15 uku. 25 ¶ 10–uku. 26 ¶ 14

Na. 3: Je, Wanadamu Waliumbwa Waishi kwa Muda Mfupi Kisha Wafe? (rs uku. 343 ¶ 1-3)

Na. 4: Kwa Nini Kucheza Kamari Ni Makosa?

Feb. 24 Usomaji wa Biblia: Marko 5-8 Wimbo 72

Sifa ya Usemi: Njia za Kuboresha Matamshi (be uku. 90 ¶ 3–uku. 92)

Pitio la Maswali na Majibu

Mac. 3 Usomaji wa Biblia: Marko 9-12 Wimbo 195

Sifa ya Usemi: Ufasaha (be uku. 93 ¶ 1–uku. 94 ¶ 3)

Na. 1: Kuwa Msikivu, Unaposikiliza Hotuba, Wakati wa Mazungumzo, na Kusanyikoni (be uku. 15 ¶ 1–uku. 16 ¶ 5)

Na. 2: Marko 10:1-22

Na. 3: Jinsi Tunavyoweza Kupata Nguvu Kutoka kwa Mungu

Na. 4: Tumaini Letu la Kuishi Milele Linategemea Nini? (rs uku. 344 ¶ 5-7)

Mac. 10 Usomaji wa Biblia: Marko 13-16 Wimbo 187

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuboresha Ufasaha (be uku. 94 ¶ 4–uku. 96 ¶ 3, isipokuwa sanduku kwenye uku. 95)

Na. 1: Paradiso ya Kiroho Ni Nini? (w01 3/1 uku. 8-11)

Na. 2: Marko 13:1-23

Na. 3: Matazamio kwa Ajili ya Uhai wa Wakati Ujao Yatatimizwaje? (rs uku. 344 ¶ 8–uku. 345 ¶ 3)

Na. 4: Je, Mungu Anaunga Mkono Upande Fulani Katika Vita ya Wanadamu?

Mac. 17 Usomaji wa Biblia: Luka 1-3 Wimbo 13

Sifa ya Usemi: Kukabiliana na Kigugumizi (be uku. 95, sanduku)

Na. 1: “Heri Mtu Yule Aonaye Hekima” (w01 3/15 uku. 25-28)

Na. 2: Luka 3:1-22

Na. 3: Je, Inafaa Kumwabudu Yesu?

Na. 4: aJe, Ni Jambo la Maana Kufunga Ndoa Kupatana na Matakwa ya Kisheria? (rs uku. 241 ¶ 2–uku. 242 ¶ 2)

Mac. 24 Usomaji wa Biblia: Luka 4-6 Wimbo 156

Sifa ya Usemi: Kutua kwa Kufuata Alama za Vituo na ili Kubadili Mawazo (be uku. 97 ¶ 1–uku. 98 ¶ 5)

Na. 1: Je, Unahisi Umeeleweka Vibaya? (w01 4/1 uku. 20-23)

Na. 2: Luka 6:1-23

Na. 3: Maana ya Ukumbusho Ni Nini? (rs uku. 353 ¶ 1-3)

Na. 4: Je, Wakristo Wanaweza Kutarajia Ulinzi Kutoka kwa Mungu?

Mac. 31 Usomaji wa Biblia: Luka 7-9 Wimbo 47

Sifa ya Usemi: Kutua ili Kutia Mkazo, Kutua ili Kusikiliza (be uku. 99 ¶ 1–uku. 100 ¶ 4)

Na. 1: “Hofu Mungu wa Kweli na Uzishike Amri Zake” (be uku. 272 ¶ 1–uku. 275 ¶ 3)

Na. 2: w01 3/15 uku. 18 ¶ 17–uku. 19 ¶ 20

Na. 3: Jinsi Tunavyojua Kwamba Biblia ni Neno la Mungu

Na. 4: Mkate na Divai Inayotumiwa Kwenye Ukumbusho Ni Mifano ya Nini? (rs uku. 353 ¶ 4–uku. 354 ¶ 1)

Apr. 7 Usomaji wa Biblia: Luka 10-12 Wimbo 68

Sifa ya Usemi: Kukazia Maana kwa Njia Inayofaa (be uku. 101 ¶ 1–uku. 102 ¶ 3)

Na. 1: ‘Kutoa Ushahidi Kuhusu Yesu’ (be uku. 275 ¶ 4–uku. 278 ¶ 4)

Na. 2: Luka 10:1-22

Na. 3: Ni Nani Wanaopaswa Kushiriki Katika Chakula cha Jioni cha Bwana? (rs uku. 354 ¶ 3-4)

Na. 4: Watu Wawili wa Kwanza Waliunganishwa Katika Ndoa Jinsi Gani? (rs uku. 242 ¶ 3-4)

Apr. 14 Usomaji wa Biblia: Luka 13-17 Wimbo 208

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kukazia Maana Vizuri Zaidi (be uku. 102 ¶ 4–uku. 104 ¶ 4)

Na. 1: “Habari Njema Hii ya Ufalme” (be uku. 279 ¶ 1–uku. 281 ¶ 4)

Na. 2: Luka 15:11-32

Na. 3: Jinsi Tunavyoweza Kujilinda na Uvutano wa Mashetani

Na. 4: Ukumbusho Unapaswa Kuadhimishwa Mara Ngapi, na Wakati Gani? (rs uku. 355 ¶ 3–uku. 356 ¶ 1)

Apr. 21 Usomaji wa Biblia: Luka 18-21 Wimbo 23

Sifa ya Usemi: Kukazia Mawazo Makuu (be uku. 105 ¶ 1–uku. 106 ¶ 1)

Na. 1: Majira Ambayo Yehova Amepanga kwa Hekima na Upendo (si uku. 280 ¶ 14-17)

Na. 2: w01 4/15 uku. 6 ¶ 19–uku. 7 ¶ 22

Na. 3: Jinsi Tumaini la Ufufuo Linavyotusaidia Maishani

Na. 4: bJe, Biblia Inakubali Ndoa ya Wake Wengi? (rs uku. 243 ¶ 1–uku. 244 ¶ 1)

Apr. 28 Usomaji wa Biblia: Luka 22-24 Wimbo 218

Sifa ya Usemi: Kiasi cha Sauti Kinachowafaa Wasikilizaji (be uku. 107 ¶ 1–uku. 108 ¶ 5)

Pitio la Maswali na Majibu

Mei 5 Usomaji wa Biblia: Yohana 1-4 Wimbo 31

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuboresha Kiasi cha Sauti (be uku. 108 ¶ 6–uku. 110 ¶ 2)

Na. 1: Unaweza Kuboresha Kumbukumbu Yako (be uku. 17 ¶ 1–uku. 19 ¶ 1)

Na. 2: Yohana 2:1-25

Na. 3: Je, Mungu Amekataza Utumizi wa Kileo?

Na. 4: cMaoni ya Mungu Ni Nini Kuhusu Kutengana? (rs uku. 244 ¶ 2)

Mei 12 Usomaji wa Biblia: Yohana 5-7 Wimbo 150

Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Rekebisha Kiasi cha Sauti (be uku. 111 ¶ 1–uku. 112 ¶ 2)

Na. 1: Unaweza Kufanikiwa Licha ya Malezi Yako (w01 4/15 uku. 25-28)

Na. 2: Yohana 5:1-24

Na. 3: Kwa Nini Si Jambo la Akili Kuamini Kwamba Mungu Ameamua Kimbele Wale Watakaookoka?

Na. 4: dBiblia Inasema Nini Kuhusu Talaka na Kuoa au Kuolewa Tena? (rs uku. 244 ¶ 3–uku. 245 ¶ 3)

Mei 19 Usomaji wa Biblia: Yohana 8-11 Wimbo 102

Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Badili Mwendo wa Kuzungumza (be uku. 112 ¶ 3-6)

Na. 1: ‘Kwa hekima Siku Zetu Zitazidishwa’ (w01 5/15 uku. 28-31)

Na. 2: Yohana 10:16-42

Na. 3: Kwa Nini Mungu Aliruhusu Ndoa Kati ya Ndugu na Dada Hapo Zamani? (rs uku. 245 ¶ 4-5)

Na. 4: Jinsi ya Kukabiliana na Msongo wa Maisha

Mei 26 Usomaji wa Biblia: Yohana 12-16 Wimbo 24

Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Kuinua na Kupunguza Sauti (be uku. 113 ¶ 1–uku. 114 ¶ 2)

Na. 1: Maana ya Mwaka Katika Maandiko Matakatifu (si uku. 280 ¶ 18–uku. 282 ¶ 23)

Na. 2: w01 5/1 uku. 14 ¶ 4–uku. 15 ¶ 7

Na. 3: ‘Kutokuwa Sehemu ya Ulimwengu’ Kunamaanisha Nini?

Na. 4: Ni Nini Kinachoweza Kuiboresha Ndoa? (rs uku. 246 ¶ 1-4)

Juni 2 Usomaji wa Biblia: Yohana 17-21 Wimbo 198

Sifa ya Usemi: Zungumza kwa Hisia (be uku. 115 ¶ 1–uku. 116 ¶ 4)

Na. 1: Jinsi Roho ya Mungu Inavyoweza Kutusaidia Kukumbuka (be uku. 19 ¶ 2–uku. 20 ¶ 3)

Na. 2: Yohana 20:1-23

Na. 3: Ni Nini Kinachoweza Kuiboresha Ndoa? (rs uku. 246 ¶ 5-8)

Na. 4: Je, Ni Lazima Dini Iwe Imepangwa kwa Njia Maalumu?

Juni 9 Usomaji wa Biblia: Matendo 1-4 Wimbo 92

Sifa ya Usemi: Shauku Inayofaa Habari (be uku. 116 ¶ 5–uku. 117 ¶ 4)

Na. 1: Imarisha Tumaini Lako Katika Yehova (w01 6/1 uku. 7-10)

Na. 2: Matendo 4:1-22

Na. 3: Biblia Inatuambia Nini Kumhusu Mariamu? (rs uku. 172 ¶ 1-6)

Na. 4: Je, Jinsi Tunavyoabudu Ni Muhimu kwa Mungu?

Juni 16 Usomaji wa Biblia: Matendo 5-7 Wimbo 2

Sifa ya Usemi: Kuongea kwa Huruma (be uku. 118 ¶ 1–uku. 119 ¶ 5)

Na. 1: Ungamo Liletalo Ponyo la Kiroho (w01 6/1 uku. 28-31)

Na. 2: Matendo 7:1-22

Na. 3: Kile Kinachowafanya Mashahidi wa Yehova Wawe Tofauti na Dini Nyingine

Na. 4: Je, Kweli Mariamu Alikuwa Bikira Alipomzaa Yesu? (rs uku. 172 ¶ 7–uku. 173 ¶ 1)

Juni 23 Usomaji wa Biblia: Matendo 8-10 Wimbo 116

Sifa ya Usemi: Kuongea kwa Hisia (be uku. 119 ¶ 6–uku. 120 ¶ 4)

Na. 1: Watazame Mayatima na Wajane katika Dhiki Yao (w01 6/15 uku. 9-12)

Na. 2: w01 6/1 uku. 12 ¶ 1–uku. 13 ¶ 5

Na. 3: Je, Mariamu Alikuwa Bikira Sikuzote? (rs uku. 173 ¶ 2–uku. 174 ¶ 1)

Na. 4: eKuhudhuria Mikutano Ni Muhimu Ili Kufanya Maendeleo ya Kiroho

Juni 30 Usomaji wa Biblia: Matendo 11-14 Wimbo 167

Sifa ya Usemi: Ishara za Mwili na za Uso Ni Muhimu (be uku. 121 ¶ 1-4)

Pitio la Maswali na Majibu

Julai 7 Usomaji wa Biblia: Matendo 15-17 Wimbo 38

Sifa ya Usemi: Kutumia Ishara za Mwili na za Uso (be uku. 122 ¶ 1–uku. 123 ¶ 2)

Na. 1: Jitahidi Uwe Msomaji Mzuri (be uku. 21 ¶ 1–uku. 23 ¶ 3)

Na. 2: Matendo 15:1-21

Na. 3: Jinsi Tunavyounga Mkono Enzi Kuu ya Yehova

Na. 4: Je, Mariamu Alikuwa Mama ya Mungu? (rs uku. 174 ¶ 2-4)

Julai 14 Usomaji wa Biblia: Matendo 18-21 Wimbo 32

Sifa ya Usemi: Kuwatazama Wasikilizaji Katika Huduma (be uku. 124 ¶ 1–uku. 125 ¶ 4)

Na. 1: Usiruhusu Imani Yako Iharibiwe na Shaka (w01 7/1 uku. 18-21)

Na. 2: Matendo 19:1-22

Na. 3: fJe, Mariamu Alikingiwa Dhambi ya Asili Mama Yake Alipopata Mimba? (rs uku. 175 ¶ 1-2)

Na. 4: ‘Kuendelea Kuutafuta Ufalme Kwanza’ Kunamaanisha Nini?

Julai 21 Usomaji wa Biblia: Matendo 22-25 Wimbo 222

Sifa ya Usemi: Kuwatazama Wasikilizaji Unapotoa Hotuba (be uku. 125 ¶ 5–uku. 127 ¶ 1)

Na. 1: Je, Wewe Ni Mvumilivu Kweli? (w01 7/15 uku. 21-23)

Na. 2: Matendo 24:1-23

Na. 3: Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?

Na. 4: gJe, Mariamu Alipaa Mbinguni Akiwa na Mwili wa Binadamu? (rs uku. 175 ¶ 3–uku. 176 ¶ 1)

Julai 28 Usomaji wa Biblia: Matendo 26-28 Wimbo 14

Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Katika Huduma ya Shambani (be uku. 128 ¶ 1–uku. 129 ¶ 1)

Na. 1: Hakuna Mwaka Sifuri (si uku. 282 ¶ 24-26)

Na. 2: w01 7/1 uku. 14 ¶ 5-8

Na. 3: Je, Inafaa Kusali kwa Mariamu Akiwa Mwombezi? (rs uku. 176 ¶ 2-4)

Na. 4: Jinsi Tunavyoonyesha Kwamba Tunaheshimu Zawadi ya Uhai

Ago. 4 Usomaji wa Biblia: Waroma 1-4 Wimbo 106

Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Jukwaani (be uku. 129 ¶ 2-5)

Na. 1: Jinsi ya Kujizoeza Kuwa Msomaji Mzuri (be uku. 23 ¶ 4–uku. 26 ¶ 5)

Na. 2: Waroma 2:1-24

Na. 3: Je, Umewahi Kuishi Ukiwa na Umbo Jingine?

Na. 4: Je, Mariamu Aliheshimiwa kwa Njia ya Pekee Katika Kutaniko la Kikristo la Karne ya Kwanza? (rs uku. 177 ¶ 2–uku. 178 ¶ 1)

Ago. 11 Usomaji wa Biblia: Waroma 5-8 Wimbo 179

Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Mbele ya Watu (be uku. 130 ¶ 1-3)

Na. 1: ‘Baraka kwa Waadilifu’ (w01 7/15 uku. 24-27)

Na. 2: Waroma 5:6-21

Na. 3: hJe, Ninyi Mnamwamini Bikira Mariamu? (rs uku. 178 ¶ 2-4)

Na. 4: Je, Unaamini Kwamba Watu Huzaliwa Upya Katika Umbo Jingine?

Ago. 18 Usomaji wa Biblia: Waroma 9-12 Wimbo 206

Sifa ya Usemi: Sura Safi Hufanya Ujumbe Uvutie Zaidi (be uku. 131 ¶ 1-3)

Na. 1: Acha Mazoea Yakunufaishe (w01 8/1 uku. 19-22)

Na. 2: w01 8/15 uku. 21 ¶ 10–uku. 22 ¶ 13

Na. 3: Je, Wanadamu Wameibadili Biblia?

Na. 4: Je, Mkate na Divai Hubadilika Kuwa Mwili na Damu Halisi ya Kristo? (rs uku. 201 ¶ 1–uku. 202 ¶ 3)

Ago. 25 Usomaji wa Biblia: Waroma 13-16 Wimbo 43

Sifa ya Usemi: Jinsi Kiasi na Utimamu wa Akili Zinavyotusaidia kwa Habari ya Mavazi na Mapambo (be uku. 131 ¶ 4–uku. 132 ¶ 3)

Pitio la Maswali na Majibu

Sept. 1 Usomaji wa Biblia: 1 Wakorintho 1-9 Wimbo 48

Sifa ya Usemi: Umuhimu wa Mavazi Yanayofaa (be uku. 132 ¶ 4–uku. 133 ¶ 1)

Na. 1: Jinsi ya Kujifunza (be uku. 27 ¶ 1−uku. 31 ¶ 2)

Na. 2: 1 Wakorintho 3:1-23

Na. 3: Ni Nini Maana ya Yohana 6:53-57? (rs uku. 202 ¶ 4–uku. 203 ¶ 1)

Na. 4: Je, Umaskini Unampa Mtu Udhuru wa Kuiba?

Sept. 8 Usomaji wa Biblia: 1 Wakorintho 10-16 Wimbo 123

Sifa ya Usemi: Tukiwa Nadhifu Hatutamkwaza Mtu Yeyote (be uku. 133 ¶ 2-4)

Na. 1: Shinda Vikwazo Vinavyokuzuia Usifanye Maendeleo! (w01 8/1 uku. 28-30)

Na. 2: 1 1 Wakorintho 12:1-26

Na. 3: Kwa Nini Mungu Huruhusu Mambo Mabaya Yatukie?

Na. 4: Je, Yesu Alianzisha Misa? (rs uku. 203 ¶ 2–uku. 205 ¶ 2)

Sept. 15 Usomaji wa Biblia: 2 Wakorintho 1-7 Wimbo 16

Sifa ya Usemi: Jinsi Unavyosimama na Vifaa Nadhifu (be uku. 133 ¶ 5–uku. 134 ¶ 4)

Na. 1: Jinsi ya Kufanikisha Ujana Wako (w01 8/15 uku. 4-7)

Na. 2: 2 Wakorintho 6:1–7:1

Na. 3: Maoni ya Mkristo Kuhusu Mamlaka ya Ulimwengu (rs uku. 138 ¶ 3–uku. 139 ¶ 2)

Na. 4: Mungu Anauonaje Uchafuzi wa Mazingira?

Sept. 22 Usomaji wa Biblia: 2 Wakorintho 8-13 Wimbo 207

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kupunguza Wasiwasi Unapotoa Hotuba (be uku. 135 p. 1–uku. 137 ¶ 2)

Na. 1: Jinsi Unavyoweza Kufanya Maamuzi ya Hekima (w01 9/1 uku. 27-30)

Na. 2: 2 Wakorintho 8:1-21

Na. 3: Nafsi Inakwenda Wapi Baada ya Kifo?

Na. 4: Maandiko Yanayohusisha Maoni ya Mkristo Juu ya Vita (rs uku. 139 ¶ 3–uku. 140 ¶ 2)

Sept. 29 Usomaji wa Biblia: Wagalatia 1-6 Wimbo 163

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuwa Mtulivu (be uku. 137 ¶ 3–uku. 138 ¶ 5)

Na. 1: Kwa Nini Tarehe za Msingi Ni Muhimu Sana? (si uku. 282 ¶ 27–uku. 283 ¶ 30)

Na. 2: w01 9/1 uku. 15 ¶ 8–uku. 17 ¶ 11

Na. 3: Kwa Nini Yehova Aliwaruhusu Waisraeli Kwenda Vitani? (rs uku. 140 ¶ 3-4)

Na. 4: Jinsi Tunavyojua Kwamba Ufalme wa Mungu Unatawala Sasa

Okt. 6 Usomaji wa Biblia: Waefeso 1-6 Wimbo 99

Sifa ya Usemi: Umuhimu wa Kikuza-Sauti (be uku. 139 ¶ 1–uku. 140 ¶ 1)

Na. 1: Funzo Lina Faida (be uku. 31 ¶ 3–uku. 32 ¶ 3)

Na. 2: Waefeso 2:1-22

Na. 3: Kumwamini Mungu Ni Jambo la Akili

Na. 4: Maoni ya Mkristo Kuhusu Kuunga Mkono Masuala ya Kisiasa Hutegemea Maandiko Gani? (rs uku. 142 ¶ 1-5)

Okt. 13 Usomaji wa Biblia: Wafilipi 1-4 –Wakolosai 1-4 Wimbo 105

Sifa ya Usemi: Tumia Kikuza-Sauti kwa Njia Inayofaa (be uku. 140 ¶ 2–uku. 142 ¶ 1)

Na. 1: Tembea Katika ‘Njia ya Unyofu’ (w01 9/15 uku. 24-28)

Na. 2: Wafilipi 2:1-24

Na. 3: Maoni ya Mkristo Kuhusu Sherehe za Kizalendo Hutegemea Maandiko Gani? (rs uku. 143 ¶ 1–uku. 144 ¶ 2)

Na. 4: Kile Ambacho Yehova Anataka Tufanye Leo

Okt. 20 Usomaji wa Biblia: 1 Wathesalonike 1-5 –2 Wathesalonike 1-3 Wimbo 145

Sifa ya Usemi: Kutumia Biblia Kujibu Maswali (be uku. 143 ¶ 1-3)

Na. 1: Maoni ya Yehova Kuhusu Wakati (si uku. 283 ¶ 31–uku. 284 ¶ 33)

Na. 2: w01 10/15 uku. 23 ¶ 6–uku. 24 ¶ 9

Na. 3: Ni Nani Watakaokwenda Mbinguni?

Na. 4: Je, Wakristo Hukataa Kuunga Mkono Vita na Siasa kwa Sababu Hawawajali Majirani Wao? (rs uku. 144 ¶ 3)

Okt. 27 Usomaji wa Biblia: 1 Timotheo 1-6 –2 Timotheo 1-4 Wimbo 46

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kutumia Biblia Vizuri Zaidi (be uku. 144 ¶ 1-4)

Pitio la Maswali na Majibu

Nov. 3 Usomaji wa Biblia: Tito 1-3 –Filemoni 1-25 Wimbo 30

Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia (be uku. 145-146)

Na. 1: Jinsi ya Kufanya Utafiti (be uku. 33 ¶ 1–uku. 35 ¶ 2)

Na. 2: Filemoni 1-25

Na. 3: Je, Maisha Katika Hali Kamilifu Yatakuwa ya Kuchosha?

Na. 4: Kwa Nini Jina la Yehova Limetumiwa Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya? (rs uku. 250 ¶ 3–uku. 251 ¶ 1)

Nov. 10 Usomaji wa Biblia: Waebrania 1-8 Wimbo 149

Sifa ya Usemi: Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko Ni Muhimu (be uku. 147 ¶ 1–uku. 148 ¶ 2)

Na. 1: Enoki Alitembea Pamoja na Mungu Katika Ulimwengu Wenye Dhambi (w01 9/15 uku. 29-31)

Na. 2: Waebrania 2:1-18

Na. 3: iKumjibu Mtu Asemaye, ‘Ninyi Mna Biblia Yenu Wenyewe’ (rs uku. 251 ¶ 3–uku. 252 ¶ 2)

Na. 4: Watakaofufuliwa Watahukumiwa Kufuatana na Matendo Gani?

Nov. 17 Usomaji wa Biblia: Waebrania 9-13 Wimbo 144

Sifa ya Usemi: Kuchagua Maelezo Yanayofaa Kutoa Utangulizi wa Maandiko (be uku. 148 ¶ 3–uku. 149 ¶ 3)

Na. 1: Inamaanisha Nini Kuwa Mwaminifu-Mshikamanifu? (w01 10/1 uku. 20-23)

Na. 2: Waebrania 9:11-28

Na. 3: Je, Viumbe wa Mungu wa Mbinguni Wamepangwa Kitengenezo? (rs uku. 311 ¶ 3-4)

Na. 4: Mwenendo Unaomheshimu Mungu Una Faida Kubwa

Nov. 24 Usomaji wa Biblia: Yakobo 1-5 Wimbo 88

Sifa ya Usemi: Mkazo Unaofaa Unatia Ndani Kusoma kwa Hisia (be uku. 150 ¶ 1-2)

Na. 1: Kupima Matukio Katika Mkondo wa Wakati (si uku. 284 ¶ 1-4)

Na. 2: w01 11/1 uku. 12 ¶ 15–uku. 13 ¶ 19

Na. 3: Sifa ya Kiasi Ni Muhimu

Na. 4: Mungu Aliwapa Watumishi Wake wa Kale Waliokuwa Duniani Maagizo Jinsi Gani? (rs uku. 312 ¶ 1-2)

Des. 1 Usomaji wa Biblia: 1 Petro 1-5 –2 Petro 1-3 Wimbo 54

Sifa ya Usemi: Kazia Maneno Yanayofaa (be uku. 150 ¶ 3–uku. 151 ¶ 2)

Na. 1: Kujifunza Kutumia Vifaa Vingine vya Utafiti (be uku. 35 ¶ 3–uku. 38 ¶ 4)

Na. 2: 1 Petro 1:1-16

Na. 3: Je, Biblia Inaonyesha Kwamba Wakristo wa Kweli Wangepangwa Kitengenezo? (rs uku. 313 ¶ 1-4)

Na. 4: Dhabihu ya Fidia ya Kristo Inapaswa Kuwa na Matokeo Gani Maishani Mwetu?

Des. 8 Usomaji wa Biblia: 1 Yohana 1-5; 2Yo 1-13; 3Yo 1-14 –Yuda 1-25 Wimbo 22

Sifa ya Usemi: Njia za Kutia Mkazo (be uku. 151 ¶ 3–uku. 152 ¶ 5)

Na. 1: Linda Dhamiri Yako (w-01SW 11/1 uku. 4-7)

Na. 2: 1 Yohana 3:1-18

Na. 3: Biblia Haiungi Mkono Kuwatendea Wanawake Bila Heshima

Na. 4: Je, Watumishi Waaminifu wa Mungu Wametawanyika Katika Makanisa Mbalimbali Yanayodai Kuwa ya Kikristo (rs uku. 314 ¶ 1-3)

Des. 15 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 1-6 Wimbo 219

Sifa ya Usemi: Kutumia Maandiko Vizuri (be uku. 153 ¶ 1–uku. 154 ¶ 3)

Na. 1: Noa Auhukumu Ulimwengu kwa Imani Yake (w01 11/15 uku. 28-31)

Na. 2: Ufunuo 2:1-17

Na. 3: Sehemu Inayoonekana ya Tengenezo la Yehova Inaweza Kutambuliwa Jinsi Gani? (rs uku. 314 ¶ 4–uku. 315 ¶ 2)

Na. 4: Kwa Nini Wakristo Hawasherehekei Krismasi?

Des. 22 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 7-14 Wimbo 6

Sifa ya Usemi: Onyesha Vizuri Jinsi Andiko Linavyohusika (be uku. 154 ¶ 4–uku. 155 ¶ 4)

Na. 1: Unaweza Kuepuka Ugonjwa wa Moyo wa Mfano (w01 12/1 uku. 9-13)

Na. 2: w01 12/15 uku. 17 ¶ 10–uku. 18 ¶ 13 (kutia ndani kielezi-chini)

Na. 3: Unaweza Kushinda Vishawishi vya Marika

Na. 4: Tunaweza Kuonyesha Heshima kwa Tengenezo la Yehova Jinsi Gani? (rs uku. 315 ¶ 3-7)

Des. 29 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 15-22 Wimbo 60

Sifa ya Usemi: Tumia Maandiko Kutoa Sababu (be uku. 155 ¶ 5–uku. 156 ¶ 5)

Pitio la Maswali na Majibu

[Maelezo ya Chini]

a Wagawie akina ndugu pekee sehemu hii.

b Wagawie akina ndugu pekee sehemu hii.

c Wagawie akina ndugu pekee sehemu hii.

d Wagawie akina ndugu pekee sehemu hii.

e Wagawie akina ndugu pekee sehemu hii.

f Muda ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

g Muda ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

h Muda ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

i Muda ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki