Wimbo 206
“Lifurahieni Tumaini”
1. Tushukuru Mungu wetu
Kuishi kwa tumaini.
Hilo ni nanga hakika;
Kwalo tunathibitika.
Tumaini ni kofia
Humuzuia Shetani;
Hupinga mbali uovu
Hupa nguvu za adili.
2. Twalifurahia lile
Tumaini letu mbele
Na wafu kufufuliwa
Waipande Paradiso!
Milele hata milele
Watu watafaidika
Na mupango wake Mungu,
Wapate furaha tele.
3. Ili tulitie nguvu,
Tutunze safi mioyo,
Tusome Neno la Mungu,
Sala zetu zisikiwe.
Wengine wafurahie,
Tusiwe wenye uchoyo,
Bali tutangaze kote,
Wengine waje kwa Mungu.