Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/03 uku. 1
  • Iweni Timamu Katika Akili Mwisho Unapokaribia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Iweni Timamu Katika Akili Mwisho Unapokaribia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Tumia Miradi ya Kiroho ili Kumtukuza Muumba Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Kujiwekea Miradi ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Jinsi Unavyoweza Kufikia Miradi Yako ya Kiroho
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Vijana—Miradi Yenu ya Kiroho Ni Ipi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 2/03 uku. 1

Iweni Timamu Katika Akili Mwisho Unapokaribia

1 Neno la Mungu husema tena na tena kwamba siku ya Yehova itakuja “kama mwizi,” yaani, kwa ghafula, mara moja, na bila onyo. (1 The. 5:2; Mt. 24:43; 2 Pet. 3:10; Ufu. 3:3; 16:15) “Kwa sababu hiyo,” Yesu alisema, “jithibitisheni wenyewe kuwa tayari, kwa sababu kwenye saa msiyoifikiri kuwa hiyo, Mwana wa binadamu anakuja.” (Mt. 24:44) Tunawezaje kuwa macho kiroho kadiri mwisho unavyokaribia? Tutafanikiwa tukifuata maneno haya yaliyoandikwa kwa mwongozo wa Mungu: “Iweni timamu katika akili.”—1 Pet. 4:7.

2 Kuwa timamu katika akili kwahusisha kuona mambo kama Yehova anavyoyaona. (Efe. 5:17) Hutusaidia kujiona kuwa “wakaaji wa kigeni na wakazi wa muda” katika mfumo huu wa mambo. (1 Pet. 2:11) Hutuwezesha kufahamu mambo yaliyo ya maana kabisa, kuamua mambo ya kutanguliza, na kufanya maamuzi mazuri.—Flp. 1:10.

3 Weka Miradi ya Kiroho: Kuweka na kutimiza miradi ya kiroho hutusaidia kuwa timamu katika akili. Je, una miradi ya kiroho unayojitahidi kutimiza? Je, unajitahidi kusoma Biblia kila siku, kuhudhuria mikutano yote ya Kikristo, kusoma kila toleo la Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, au labda kuhubiri zaidi? Ukiweka miradi inayokufaa, uazimie kuitimiza, na kumwomba Yehova abariki jitihada zako, utapata matokeo mazuri ajabu.

4 Mzee mmoja aliwauliza wenzi wa ndoa vijana kuhusu miradi yao ya kiroho. Swali hilo liliwafanya watambue kwamba wangeweza kuwa mapainia iwapo wangefanya maisha yao kuwa sahili na kulipa deni kubwa walilokuwa nalo. Waliamua kuweka mradi huo. Walijitahidi kulipa deni hilo na kutafuta njia za kupunguza mambo yasiyo ya lazima yaliyokuwa yakichukua wakati wao na nguvu zao. Baada ya mwaka mmoja tu, walitimiza mradi wao. Matokeo yakawaje? Mume anasema hivi: “Kama hatungekuwa na miradi, hali yetu ingekuwa tofauti. Tuna furaha na utulivu zaidi. Maisha yetu yana kusudi halisi.”

5 Tunapongoja siku ya Yehova, na tuendelee kuwa macho kiroho kwa kuishi kwa utimamu wa akili, na kufanya mapenzi ya Mungu bila kukengeushwa.—Tito 2:11-13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki