Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/03 uku. 8
  • Neno la Mungu Ni Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Neno la Mungu Ni Kweli
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • “Neno la Mungu Lina . . . Nguvu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • “Neno la Mungu . . . Hukazia Nguvu”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Je, Wewe Hulitetea Neno la Mungu?
    Huduma ya Ufalme—2007
  • ‘Endelea Kutembea Katika Kweli’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 5/03 uku. 8

Neno la Mungu Ni Kweli

1 Mtunga-zaburi aliandika hivi: “Jumla ya neno lako ni kweli.” (Zab. 119:160) Kupitia Neno lake aliloliongoza kwa roho yake, Yehova huwapa watu majibu yenye kuridhisha kwa maswali muhimu zaidi maishani. Yeye huwapa faraja na tumaini wale wanaotaabika. Na hutuonyesha jinsi tunavyoweza kumkaribia. Mwanamke mmoja mwenye uthamini aliandika hivi: “Kujifunza kweli ya Biblia ni kama kuondoka kwenye giza tititi na kuingia kwenye chumba changavu, chenye nuru, na chenye kupendeza.” Je, wewe hujitahidi kuwaambia wengine kweli ya Neno la Mungu kila unapopata nafasi?

2 Biblia Huvutia Watu Ulimwenguni Pote na Ina Nguvu ya Kuwafanya Wabadilike: Kweli ya Biblia ina nguvu ya kuchochea mioyo na kufanya watu wabadili maisha yao. (Ebr. 4:12) Mwanamke mmoja anayeitwa Rosa alikuwa kahaba, na pia alitumia dawa za kulevya na alikunywa pombe kupindukia. Yeye anasema hivi: “Siku moja, nilipokuwa nimeshuka moyo sana, wenzi wa ndoa Mashahidi waliniambia jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia kutatua matatizo yetu. Nikaanza kujifunza Neno la Mungu, na kulifurahia sana. Baada ya mwezi mmoja nilikuwa na nguvu za kuanza kuishi maisha safi kiadili. Kwa kuwa sasa nilikuwa nimepata kusudi maishani, sikuhitaji tena kutegemea pombe au dawa za kulevya. Na kwa kuwa nilitaka kujitahidi ili niwe rafiki ya Yehova, niliazimia kuishi kupatana na sheria zake. Kama singepata hekima ya Neno la Mungu, kwa kweli sasa ningekuwa nimejiua.”—Zab. 119:92.

3 Tofauti na vitabu vingi leo, Biblia huvutia watu kutoka katika ‘mataifa yote, makabila, vikundi vya watu, na lugha.’ (Ufu. 7:9) Mapenzi ya Mungu ni “kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Kwa hiyo, tusidhanie kamwe kwamba huenda mtu asipendezwe na habari njema kwa sababu tu ya malezi yake. Badala yake, waambie watu wote habari za Ufalme, ukitumia Biblia ikiwezekana.

4 Kazia Maandiko: Kuna fursa nyingi sana za kutumia Biblia katika huduma. Unapotoa magazeti, jaribu kutia ndani andiko lililo katika utoaji uliopendekezwa. Wengine hupata matokeo mazuri kwa kutumia andiko lililochaguliwa kwa uangalifu katika utangulizi wao wanapotumia toleo la mwezi. Unapofanya ziara za kurudia, soma andiko moja au zaidi kutoka katika Biblia kila mara ili umsaidie mwenye nyumba atwae ujuzi sahihi hatua kwa hatua. Unapoongoza funzo la Biblia, kazia maandiko ya msingi katika mazungumzo. Beba Biblia sikuzote hata kama huendi katika huduma, ili uweze kuitumia wakati wowote fursa zinapotokea.—2 Tim. 2:15.

5 Na tusaidie wengine wanufaike na nguvu yenye kuchochea ya Neno la Mungu kwa kutumia Biblia wakati wowote ufaao katika huduma yetu.—1 The. 2:13.

[Maswali ya Funzo]

1. Biblia ina habari gani muhimu?

2. Biblia husaidiaje watu kuboresha maisha yao?

3. Kwa nini tusikose kuwaambia wengine ujumbe wa Biblia?

4. Tunaweza kutumiaje Biblia tunapohubiri?

5. Kwa nini tujitahidi kutumia Biblia katika huduma yetu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki