Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/07 uku. 1
  • Je, Wewe Hulitetea Neno la Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Hulitetea Neno la Mungu?
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Fundisha kwa Ushawishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • “Neno la Mungu Lina . . . Nguvu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Tumia Biblia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 5/07 uku. 1

Je, Wewe Hulitetea Neno la Mungu?

1 Katika ulimwengu ambao mara nyingi hudharau Biblia, Wakristo wa kweli wanalitetea Neno la Mungu kwa bidii. Tukiwa tumesadikishwa kwamba “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu,” tunakubaliana na Yesu Kristo, aliyesema hivi aliposali kwa Yehova: “Neno lako ni kweli.” (2 Tim. 3:16; Yoh. 17:17) Tunaweza kuliteteaje vizuri Neno la Mungu?

2 Jifunze Maandiko: Bila shaka, Yesu alijifunza Neno la Mungu kwa bidii. Hilo lilimwezesha kutumia Maandiko alipofundisha muda wote wa huduma yake. (Luka 4:16-21; 24:44-46) Tunaweza kufanya nini ili kukumbuka maandiko? Tunahitaji kusoma Biblia kila siku na kutafakari mstari ambao ulitutia moyo au ambao tunaona utafaa katika huduma. Tunapotayarisha mikutano, tunapaswa kufungua Biblia na kusoma maandiko ambayo hayakunukuliwa na labda kutayarisha maelezo kuhusu maandiko hayo. Tunapohudhuria mikutano, tunapaswa kufungua Biblia zetu na kufuatana na msemaji anaposoma maandiko. Kujifunza maandiko ya Biblia kutatutayarisha ‘kulitumia sawasawa neno la kweli.’—2 Tim. 2:15.

3 Acha Biblia Iseme: Tunaposhiriki katika huduma, tunapaswa kuacha Biblia iseme. Kwa mfano, hali zikiruhusu, tunapaswa kujaribu kumsomea mwenye nyumba andiko moja. Akiuliza swali au kuzusha kipingamizi, ni afadhali kumjibu tukitumia Biblia. Ikiwa mwenye nyumba ana shughuli, huenda bado tunaweza kukazia jambo fulani katika Biblia kwa kusema, “Kabla sijaondoka, niruhusu nikusomee andiko hili moja.” Inapowezekana, soma moja kwa moja katika Biblia, ukimruhusu msikilizaji afuatane nawe unaposoma.

4 Mwenye nyumba fulani alisema hivi alipoonyeshwa maandiko ya kukanusha Utatu, “Nimekuwa nikienda kanisani maisha yangu yote, na sikujua kabisa kwamba Biblia inasema hivi!” Alikubali funzo la Biblia. Yesu alisema kwamba kondoo wake wataisikiliza sauti yake. (Yoh. 10:16, 27) Njia bora ya watu wenye mioyo minyoofu kutambua ukweli ni kuuona moja kwa moja katika Maandiko. Basi, acheni tulitetee Neno la Mungu la kweli!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki