Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Mei 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Aprili 15 na Amkeni! la Aprili.
Dak. 20: Kutegemeza Kazi ya Ufalme Kwenu na Ulimwenguni Pote. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea sura ya 12 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Dak. 15: “Anampa Nguvu Mtu Aliyechoka.”a Wakati ukiruhusu, waalike wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyoonyeshwa.
Wimbo 1 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia Sanduku la Swali.
Dak. 15: Unaweza Kujifunza Lugha Nyingine! Hotuba inayotegemea Amkeni! la Machi 2007, ukurasa wa 10-12. Kazia umuhimu wa kujifunza lugha nyingine ili kuendeleza habari njema.
Dak. 20: “Je, Wewe Hulitetea Neno la Mungu?”b Tia ndani maelezo kutoka katika masanduku yaliyo kwenye ukurasa 143-144 katika kitabu Shule ya Huduma.
Wimbo 202 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Mei. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Mei 1 na Amkeni! la Mei.
Dak. 20: Toa Kitabu Muumba au Siri ya Familia mwezi wa Juni. Taja mambo yanayohusu eneo lenu ambayo yanapatikana katika vitabu hivyo na upange kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa vitabu hivyo ukitumia njia itakayokuwa na matokeo katika eneo lenu. Wakati ukiruhusu, waombe wasikilizaji waeleze matokeo mazuri waliyopata walipotoa vitabu hivyo kwa marafiki au watu wa familia.
Dak. 15: Mambo Yaliyoonwa Shambani. Simulia mambo mazuri ambayo mapainia wasaidizi na wahubiri wengine walijionea walipoongeza utumishi wao mwezi wa Machi, Aprili, na Mei. Pia, simulia matokeo ambayo wahubiri walipata walipowarudia watu waliochukua magazeti wakiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Jambo moja au mawili yenye kupendeza yanaweza kuigizwa.
Wimbo 21 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Wafundishe Watoto Wako Kumsifu Yehova.”c Unapozungumzia fungu la 4, tia ndani habari iliyo kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 2005, ukurasa wa 7.
Wimbo 169 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.