-
MatangazoHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Matangazo
◼ Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa katika sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them. Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele kinaweza kutolewa hasa katika maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida. Septemba: Tunaweza kutoa kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali?, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, na broshua Endeleeni Kukesha! iliyo na kurasa 32, au kitabu kingine chochote cha zamani ambacho kinapatikana kutanikoni. Oktoba: Tutatoa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mwenye nyumba akipendezwa, tafadhali mtolee broshua Anataka, na urudi ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Kwa Nini Uongozwe na Biblia?”
◼ Inapendekezwa kwamba fomu ya ombi la upainia wa kawaida itumwe kwenye ofisi ya tawi angalau siku 30 kabla ya tarehe ambayo mtu anatazamia kuanza upainia. Mwandishi wa kutaniko anapaswa kuchunguza fomu ya ombi ili kuhakikisha kwamba imejazwa kikamili. Ikiwa wahubiri wanaotoa ombi hawakumbuki tarehe hususa waliyobatizwa, wanapaswa kukadiria tarehe hiyo na kuiandika ili waitumie kwa ukawaida kama tarehe yao ya ubatizo. Mwandishi anapaswa kuandika tarehe hiyo iliyokadiriwa katika kadi ya Rekodi ya Kutaniko ya Mhubiri (S-21).
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuhakikisha kwamba wana Barua ya Kuwekwa Rasmi kwa Painia (S-202) kwa ajili ya kila painia wa kawaida kutanikoni. Ikiwa hawana barua hiyo, tafadhali andikieni ofisi ya tawi kuhusu jambo hilo.
-
-
Wasaidie Watoto Wako Wafanye Maendeleo Katika HudumaHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Wasaidie Watoto Wako Wafanye Maendeleo Katika Huduma
1 Wazazi Wakristo wana wajibu mzito wa kuwazoeza watoto wao kuhubiri tangu wakiwa wachanga. Wanaweza kutimiza wajibu huo kwa njia mbalimbali. Baadhi ya watoto wanaweza kukariri andiko fulani la Biblia hata kabla hawajajua kusoma. Hilo linaweza kuwavutia sana wasikilizaji. Kadiri watoto wanavyokua, ndivyo wanavyoweza kushiriki zaidi katika huduma. Ninyi wazazi, mnaweza kuwasaidiaje watoto wenu wahubiri? Mapendekezo yafuatayo yanaweza kuwasaidia.
2 Baada ya kumsalimu mwenye nyumba, unaweza kusema hivi:
◼ “Mwana wangu, [taja jina lake], ana andiko muhimu ambalo angependa ulisikie.” Mtoto wako anaweza kusema: “Andiko hili la Zaburi lilinijulisha jina la Mungu. [Mtoto asome au akariri Zaburi 83:18.] Magazeti haya yanazungumzia yale ambayo Yehova Mungu atatufanyia. Ninaweza kukuachia magazeti haya?” Unaweza kumalizia mazungumzo kwa kueleza jinsi kazi ya ulimwenguni pote inavyotegemezwa.
3 Au unaweza kujaribu njia hii:
◼ “Hujambo. Ninamzoeza binti yangu, [taja jina lake], kuwajali watu wengine katika jamii. Angependa kukupa ujumbe mfupi kutoka katika Biblia.” Binti yako anaweza kusema: “Njia moja ninayotumia kuwasaidia watu ni kuwaonyesha tumaini letu la wakati ujao ambalo linategemea Biblia. [Mtoto asome au akariri Ufunuo 21:4.] Magazeti haya yanaeleza mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatufanyia. Natumaini utafurahia kuyasoma.”
4 Kutumia utangulizi rahisi bila kuubadili-badili huwafanya watoto wawe na uhakika kwamba wanaweza kuhubiri ujumbe wa Ufalme vizuri. Mkiwa na vipindi vya mazoezi ya kusema kwa njia inayoeleweka wazi na kwa kiasi kinachofaa cha sauti, watoto wataweza kuhubiri chini ya hali mbalimbali. Kuwatayarisha vizuri na mapema, na pia kuwapongeza kwa unyoofu kutawachochea watoto wawaeleza wengine mambo wanayoamini.
5 Watoto wengi ambao wamesaidiwa jinsi hiyo wamestahili kuwa wahubiri ambao hawajabatizwa. Tunashangilia jinsi gani kuwaona watoto wetu wakifanya maendeleo katika huduma ya Kikristo!—Zab. 148:12, 13.
-