Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/03 uku. 7
  • Kuwa Mwenye Matokeo Licha ya Ulemavu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuwa Mwenye Matokeo Licha ya Ulemavu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • “Waliniambia Singetembea Tena Kamwe!”
    Amkeni!—1991
  • Naweza Kukabilianaje na Ulemavu Wangu?
    Amkeni!—1993
  • Yehova Atakupa Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 6/03 uku. 7

Kuwa Mwenye Matokeo Licha ya Ulemavu

1 Ikiwa wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova walemavu, bado unaweza kuwa na matokeo katika huduma. Kwa kweli, hali zako zinaweza kutokeza nafasi za pekee za kuhubiri na kuwatia moyo wengine.

2 Kuhubiri: Wengi ambao hupambana na ulemavu wanashiriki kikamili katika huduma. Kwa mfano, dada mmoja ambaye hangeweza kutembea wala kuongea vizuri kutokana na upasuaji aliofanyiwa, aliona kwamba angeweza kufanya utumishi wa magazeti kama mume wake angeegesha gari lao karibu na njia yenye watu wengi. Wakati mmoja, aliwapa watu magazeti 80 kwa muda wa saa mbili! Hali zako za pekee zaweza kukufanya uwafikie watu ambao ni vigumu kuwafikia katika hali za kawaida. Ikiwa hivyo, waone watu hao kuwa eneo lako la pekee.

3 Kazi yako ya kuhubiri yaweza kuwa na matokeo sana! Huenda wengine wakavutiwa na ujumbe wa Ufalme wanapoona azimio lako na jinsi ambavyo kweli ya Biblia imekuwa na matokeo katika maisha yako. Zaidi ya hayo, unapokutana na watu ambao wanateseka, huenda hali yako ya maisha ikakusaidia kuwapa faraja ya Neno la Mungu.—2 Kor. 1:4.

4 Watie Moyo Wengine: Je, ulitiwa moyo na simulizi la maisha la Laurel Nisbet, aliyetiwa katika mashine ya kumsaidia kupumua kwa miaka 37 na bado akawasaidia watu 17 kupata ujuzi sahihi wa kweli ya Biblia? Vivyo hivyo, mfano wako unaweza kuwachochea waamini wenzako wajitahidi katika utumishi wa Yehova.—g93 1/22 uku. 18-21.

5 Hata ikiwa hali zako zinakuzuia kwenda shambani kwa kadiri upendavyo, bado unaweza kuwatia moyo wengine. Ndugu mmoja alisema: “Nimekuja kujua kwamba, hata mlemavu anaweza kuwatumikia wengine. Mimi na mke wangu tumekuwa kama nanga kwa watu mbalimbali kutanikoni. Kwa sababu ya hali zetu, sisi hupatikana nyakati zote.” Lakini, kwa sababu ya ulemavu, inaeleweka kwamba huenda usiweze kuhubiri kupatana na bidii yako sikuzote. Hata hivyo, ukisaidiwa unaweza kushiriki zaidi katika huduma. Kwa hiyo, ukihitaji msaada, usisite kuwaambia wazee au wengine kutanikoni ambao wanaweza kukusaidia.

6 Yehova huona jitihada zako zote za kumtumikia, naye hufurahia utumishi wako wa nafsi yote. (Zab. 139:1-4) Ukiendelea kumtegemea, atakuimarisha uwe na huduma yenye matokeo na yenye kuridhisha.—2 Kor. 12:7-10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki