Makusanyiko ya Wilaya na ya Kimataifa Yametuchochea Kumtukuza Mungu!
Makusanyiko ya Wilaya na ya Kimataifa ya “Mtukuzeni Mungu” ambayo yamefanywa kufikia sasa yametoa ushahidi mkubwa. Makusanyiko hayo ya kitheokrasi yamelitukuza jina la Yehova na kuboresha uwezo wetu wa ‘kumhesabia Yehova utukufu wa jina lake.’ (Zab. 96:8) Kwa kweli, anastahili kutukuzwa kwa sababu ya kazi zake za ajabu za uumbaji, zinazoonyesha sifa zake nzuri ajabu.—Ayu. 37:14; Ufu. 4:11.
Tumia maswali yanayofuata pamoja na habari ulizoandika, unapotayarisha na kushiriki pitio litakalofanywa juma la Oktoba 20 la programu ya kusanyiko.
1. Uumbaji usio na uhai huutangazaje utukufu wa Mungu, na hilo linatofautianaje na jinsi wanadamu wanavyomtukuza? (Zab. 19:1-3; “Uumbaji Unatangaza Utukufu wa Mungu”)
2. Leo, mgeuko-umbo huwakilisha jambo gani halisi, na Wakristo leo huchochewaje na jambo hilo? (hotuba ya msingi, “Maono Matukufu ya Kinabii Hutuchochea!”
3. Tunawezaje kusitawisha unyenyekevu ulioonyeshwa na nabii Danieli, nasi tutafaidikaje kwa kufanya hivyo? (Dan. 9:2, 5; 10:11, 12; “Yehova Huwafunulia Wanyenyekevu Utukufu Wake”)
4. (a) Tunaweza kujifunza mambo gani matatu kuhusu hukumu ya Mungu kutokana na unabii wa Amosi? (Amo. 1:3, 11, 13; 9:2-4, 8, 14) (b) Mashahidi wa Yehova wanaweza kujifunza nini leo kutokana na mfano wa kuonya unaopatikana katika Amosi 2:12? (“Unabii wa Amosi—Ujumbe Wake kwa Ajili ya Siku Zetu”)
5. (a) Kuna hatari gani ya kutumia kileo kupita kiasi, hata kama mtu halewi? (b) Tatizo la kutumia kileo kupita kiasi linaweza kurekebishwaje? (Marko 9:43; Efe. 5:18; “Epuka Mtego wa Kutumia Kileo Kupita Kiasi”)
6. Umefaidikaje na vile vichapo vipya, “Ona Nchi Nzuri” (“‘Nchi Nzuri’—Mwonjo wa Paradiso”) pamoja na “Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya” katika Kiswahili? (“Hatua Muhimu ya Kiroho!”)
7. Tunawezaje ‘kutoa kama vioo mrudisho wa utukufu wa Yehova’? (2 Kor. 3:18; “Tutoe Kama Vioo Mrudisho wa Utukufu wa Yehova”)
8. Kwa nini tunachukiwa bila sababu, na ni nini kinachoweza kutusaidia kudumisha ushikamanifu licha ya kuchukiwa bila sababu? (Zab. 109:1-3; “Wanachukiwa Bila Sababu”)
9. Kristo ana maoni gani kuhusu umashuhuri, na mtu anaweza kujuaje kwamba anahitaji kusitawisha maoni hayo zaidi? (Mt. 20:20-26; “Kusitawisha Maoni ya Kristo Kuhusu Umashuhuri”)
10. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuendelea kuwa watendaji kiroho licha ya uchovu wa kimwili? (“Kuchoka Kimwili Wala Si Kiroho”)
11. Shetani hutumia njia gani kuendeleza uwongo, na ni Maandiko gani yanayoweza kutusaidia kukabiliana na njia hizo za kujaribu kuvunja imani yetu? (Yoh. 10:5; “Jihadhari na ‘Sauti ya Wageni’”)
12. (a) Wazazi wanawezaje kuiga mfano wa Yesu katika Marko 10:14, 16? (b) Ni nini kinachokupendeza katika kile kitabu kipya Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu? (“Watoto Wetu Ni Urithi Wenye Thamani”)
13. Vijana wanamsifu Yehova jinsi gani? (1 Tim. 4:12; “Jinsi Vijana Wanavyomsifu Yehova”)
14. Unakumbuka mambo gani katika drama yenye kichwa “Kuhubiri kwa Ujasiri Licha ya Upinzani”?
15. Tunawezaje kuiga mfano wa (a) Petro na Yohana? (Mdo. 4:10) (b) Stefano? (Mdo. 7:2, 52, 53) (c) kutaniko la Wakristo la karne ya kwanza? (Mdo. 9:31; drama na hotuba yenye kichwa “Tangaza Habari Njema ‘Bila Kuacha’”)
16. (a) Tuliazimia kumpa Mungu utukufu katika njia gani? (b) Tunaweza kuwa na hakika juu ya jambo gani tunapotumia mambo ambayo tumejifunza katika Makusanyiko ya “Mtukuzeni Mungu”? (Yoh. 15:9, 10, 16; “‘Endeleeni Kuzaa Matunda Mengi’ Ili Kumtukuza Yehova”)
Tukitafakari maagizo mazuri ya kiroho yaliyotolewa katika kusanyiko, tutachochewa kutumia mambo tuliyojifunza. (Flp. 4:8, 9) Hilo litaimarisha azimio letu la ‘kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’—1 Kor. 10:31.