Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/04 uku. 6
  • Uwe na Mwonekano Safi Kiadili, Wenye Kustahili Sifa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe na Mwonekano Safi Kiadili, Wenye Kustahili Sifa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Mavazi Yenye Mpangilio Mzuri Humstahi Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Je, Mtindo Wako wa Mavazi Unamtukuza Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 6/04 uku. 6

Uwe na Mwonekano Safi Kiadili, Wenye Kustahili Sifa

1 “Mashahidi wa Yehova ndio watu wema zaidi! Watu wenu ni wenye fadhili nao huvalia vizuri, na wana heshima kubwa.” Ndivyo alivyosema mwakilishi wa hoteli moja kuhusu akina ndugu na dada kwenye kusanyiko moja la wilaya mwaka jana. Kwenye kusanyiko lingine, mhudumu mmoja wa hoteli alisema hivi: “Ni wazi kwamba nyinyi huvaa ili kumpendeza Mungu.” Naam, wajumbe wa kusanyiko hutazamwa na wengine. Kwa hiyo tunapaswa kuvalia “kwa namna inayostahili habari njema,” na mara nyingi kufanya hivyo huwachochea watu wasio Mashahidi watupongeze na hiyo huonyesha wazi kwamba sisi ni wahudumu wa Mungu. (Flp. 1:27) Tunapojitayarisha kuhudhuria kusanyiko la wilaya, ni vema tufikirie mwonekano wetu mapema.

2 “Hekima inayotoka juu kwanza kabisa ni safi kiadili,” akaandika mwanafunzi Yakobo. (Yak. 3:17) Inaweza kuwa vigumu kuwa na mwonekano ulio safi kiadili. Ulimwengu wa Shetani wenye maadili mapotovu huwachochea watu wafuate mitindo isiyo na kiasi, yenye kusisimua kingono, ya ajabu-ajabu ambayo haifai. (1 Yoh. 2:15-17) Kwa hiyo, tunapofanya maamuzi kuhusu mavazi na mapambo tunahitaji kutii shauri la Biblia la “kukataa kabisa kutomwogopa Mungu na tamaa za kilimwengu na tuishi kwa utimamu wa akili . . . katikati ya mfumo wa mambo wa sasa.” (Tito 2:12) Hatungependa kamwe kuwaudhi wengine kwa mwonekano wetu, iwe ni ndugu zetu, wahudumu wa hoteli na mikahawa, au watazamaji wengine.—1 Kor. 10:32, 33.

3 Mavazi Yenye Kiasi na Mpangilio Mzuri: Unapojitayarisha kwa ajili ya kusanyiko, jiulize hivi: ‘Je, mavazi yangu ni yenye kiasi, au yanawavutia watu isivyofaa? Je, yanaheshimu maoni ya wengine? Je, blauzi zangu zina shingo pana sana au ni fupi mno hivi kwamba zinaacha tumbo wazi? Je, nguo zangu zinaonyesha sana sehemu za mwili au ni zenye kubana? Je, nguo zangu ni safi na hazina harufu mbaya? Ninapokula au kupumzika baada ya programu, je, mwonekano wangu utakuwa safi, nadhifu kama wa mhudumu, au mavazi yangu yatakuwa ya kizembe, yenye mitindo ya kisasa, au ya starehe mno, na yasiyomfaa mjumbe wa kusanyiko aliyevaa beji? Je, mavazi ninayovalia wakati wa kupumzika yatanifanya nione aibu kuhubiri isivyo rasmi?’—Rom. 15:2, 3; 1 Tim. 2:9.

4 Maoni ya Wakristo wakomavu yanaweza kutusaidia. Wake wanapaswa kuwauliza waume zao jinsi ambavyo wengine watayaona mavazi yao. Wazazi wanaomwogopa Mungu wanaweza kuwasaidia watoto wao matineja. Zaidi ya hayo, akina dada wenye umri mkubwa wanaomheshimu Mungu wanaweza “kuziamsha akili za wanawake vijana . . . wawe na utimamu wa akili” katika mwonekano wao “ili neno la Mungu lisitukanwe.” (Tito 2:3-5) Vitabu vyetu vina picha zinazotusaidia kuona mavazi yenye kiasi, yaliyo na mpangilio mzuri.

5 Mletee Yehova Sifa: Makusanyiko ya wilaya huandaa nafasi nzuri sana ya kumsifu Yehova, kwetu sisi sote na kwa wenye migawo pia. Bila shaka, mwenendo wetu na usemi wetu wa Kikristo utamheshimu. Lakini jambo la kwanza ambalo watazamaji huona ni mavazi na mapambo yetu. Sisi sote na tumletee Yehova sifa kwa mwonekano wetu ulio safi kiadili, na wenye kustahili sifa.—Zab. 148:12, 13.

[Maswali ya Funzo]

1. Tunapojitayarisha kuhudhuria kusanyiko la wilaya, kwa nini tufikirie mwonekano wetu?

2. Kwa nini ni vigumu kuvaa na kujipamba kwa njia safi kiadili?

3. Ni maswali gani yatakayotusaidia tuangalie mwonekano wetu?

4. Wengine wanaweza kutusaidiaje tuwe na mwonekano ulio safi kiadili?

5. Sisi sote tunawezaje kumletea Yehova sifa wakati wa kusanyiko?

[Picha katika ukurasa wa 6]

Mambo ya Kutusaidia Tuwe na Mwonekano Unaostahili Sifa

◼ Neno la Mungu

◼ Kujichunguza

◼ Maoni ya wengine

◼ Vitabu vya Kikristo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki