Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/05 kur. 3-4
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Endeleeni Kumtarajia Yehova
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Mfuateni Kristo kwa Kujiendesha kwa Heshima
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Pindi ya Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 6/05 kur. 3-4

Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa

1 Kila mwaka, makusanyiko yetu ya wilaya hutupa nafasi ya kumtukuza Yehova. Tunahisi kama Daudi, aliyeimba: “Nitakusifu katika kutaniko kubwa; nitakusifu kati ya kikundi cha watu wengi.” (Zab. 35:18) Katika Kusanyiko la Wilaya linalokaribia la “Utii wa Kimungu,” tunawezaje kuhakikisha kwamba tukiwa tengenezo, tunamsifu Yehova?

2 Mojawapo ya njia tunazoweza kufanya hivyo ni kupitia mwenendo wetu. Wasimamizi wa mahali fulani palipofanyiwa kusanyiko walisema hivi; “Kwa sababu ya kusanyiko lenu, tumeambia vikundi vingine vya kidini vinavyotaka kukodisha mahali hapa vije vijionee jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyopanga kusanyiko, nao wana utaratibu mzuri.” Kupitia sura, ushirikiano, na mwenendo, kila mmoja wetu anaweza kuchangia sifa kama hizo, ambazo Mungu wetu anastahili.—1 Pet. 2:12.

3 Sura: Ili kumletea Yehova sifa, lazima tuvae na kujipamba kwa kiasi. (1 Tim. 2:9) Kitabu cha Shule ya Huduma, ukurasa wa 132, chasema hivi: “Mtu mwenye kiasi anatahadhari asiwaudhi wengine isivyofaa na kutojielekezea fikira mno.” Katika nchi nyingi, ni kawaida kwa watu kutovalia kwa kiasi. Hata hivyo, Yehova huthamini jitihada zenu za kumwakilisha inavyofaa. (Mdo. 15:14) Ingawa huenda kusanyiko likafanyiwa katika uwanja wa michezo au katika majumba mengine ya burudani, kwa siku hizo tatu za kusanyiko mahali hapo panakuwa “kutaniko kubwa.” Kwa hiyo, tunapokusanyika mbele za Yehova, tunapaswa kuvalia kwa njia itakayomletea sifa Mkuu wa ulimwengu.—1 Nya. 29:11.

4 Pia, tunapaswa kuzingatia sura yetu baada ya kila kipindi kila siku. Ingawa huenda tukataka kuvaa mavazi ya starehe zaidi wakati wa mapumziko au tunapokula kwenye mikahawa, bado ni muhimu mavazi na mapambo yetu yawafae wale “wanaodai kumheshimu Mungu.” (1 Tim. 2:10) Mavazi yanayofaa hayategemei mitindo inayopendwa ulimwenguni. (1 Yoh. 2:16, 17) Vichapo vyetu vya Kikristo vina picha za ndugu na dada waliovalia kwa kiasi na kwa njia yenye kupendeza katika hali mbalimbali. Kuvaa beji zetu tunapokuwa katika jiji la kusanyiko kutatukumbusha kwamba sisi ni Wakristo nyakati zote.—2 Kor. 6:3, 4.

5 Heshimu Meza ya Yehova: Katika siku za Ezra, alipokuwa akijitayarisha kusoma Maandiko, ‘watu walisimama’ ili kuonyesha heshima na hamu ya kupokea mafundisho hayo. Ezra alipoendelea kusoma, ‘watu wote walisikiliza kwa makini.’ (Neh. 8:3, 5, 6) Walitambua kwamba Yehova ndiye aliyekuwa akizungumza nao, na hilo liliwachochea wasikilize kwa makini. Je, ndivyo tunavyotenda wakati wa makusanyiko yetu?

6 Bwana Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu ametuandalia karamu. (Isa. 25:6; 1 Kor. 10:21) Ikiwa tunathamini sana kuwapo kwenye meza ya kiroho ya Yehova, mradi wetu utakuwa kuhudhuria siku zote tatu za kusanyiko letu. Je, umepanga mahali utakapolala, jinsi utakavyosafiri, na kuomba ruhusa kazini? Je, umetenga wakati wa kutosha kujitayarisha na kusafiri ili uweze kufika mahali pa kusanyiko mapema vya kutosha kupata viti, kushirikiana na ndugu zetu, na kujiunga nao katika kumsifu Yehova kwa wimbo na sala ya kufungua?—Zab. 147:1.

7 Kuheshimu meza ya Yehova kutatuchochea kusikiliza kwa makini programu inapoendelea na kuepuka kuzungumza-zungumza na wengine, kula, au kutembea-tembea. Kupitia jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara, Yehova anaandaa chakula tunachohitaji sasa hivi. (Mt. 24:45) Hakuna yeyote kati yetu anayepaswa kukosa sehemu yoyote ya programu hiyo. Wazazi wanapaswa kuketi pamoja na watoto wao na kuwasaidia wafaidike kikamili.—Kum. 31:12.

8 Tunaombwa kuleta chakula cha mchana badala ya kuondoka mahali pa kusanyiko kwenda kutafuta chakula wakati wa mapumziko ya mchana. Wengi walifuata maagizo hayo katika kusanyiko la mwaka jana nao wanastahili pongezi. Itakuwa vizuri kama nini ikiwa wote watafanya hivyo mwaka huu! (Ebr. 13:17) Mpango huo hutupa nafasi ya kufurahia ushirika wenye kujenga pamoja na ndugu zetu na kuchangia mazingira yenye umoja na amani ambayo humletea Yehova heshima.—Zab. 133:1.

9 Hubiri: Tunaposafiri kuelekea au kutoka mahali pa kusanyiko, tuna nafasi nyingi za kumsifu Yehova kwa midomo yetu. (Ebr. 13:15) Iwe tunakula kwenye mkahawa au tunazungumza na wafanyakazi wa hoteli, na tutafute nafasi ya kuwahubiria. Akili na mioyo yetu itakuwa na hazina nyingi za kiroho. Tusiwanyime watu tunaokutana nao vitu hivyo vizuri.—1 Pet. 3:15.

10 Tunatazamia kwa hamu nafasi hiyo ya kumbariki Yehova “kati ya makundi yaliyokutanika.” (Zab. 26:12) Na tumsifu Yehova pamoja kwenye Kusanyiko la Wilaya la “Utii wa Kimungu.”

[Maswali ya Funzo]

1, 2. Kusanyiko la wilaya linatupa nafasi ya kufanya nini, na mojawapo ya njia za kufanya hivyo ni gani?

3, 4. Kuwa na kiasi kutatusaidiaje kuvalia kwa njia inayowafaa wahudumu wa Kikristo, kwenye kusanyiko na baada ya vipindi vya kusanyiko?

5. Ni mfano gani mzuri uliowekwa na watu walioishi siku za Ezra?

6, 7. Tunawezaje kuonyesha kwamba tunaiheshimu meza ya Yehova ya kiroho?

8. Tunaombwa kufanya nini kuhusiana na chakula cha mchana, na kwa nini?

9, 10. Kusanyiko la wilaya linatuwezesha kumsifu Yehova katika njia gani nyingine?

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya

◼ Nyakati za Programu: Siku zote tatu, programu itaanza saa 3:30 asubuhi. Milango itafunguliwa saa 2:00 asubuhi. Dakika chache kabla ya kila kipindi kuanza, mwenyekiti ataketi kwenye jukwaa muziki wa utangulizi unapochezwa. Sote tunapaswa kuwa tumeketi ili programu iweze kuanza kwa utaratibu. Programu itaisha saa 11:05 jioni siku ya Ijumaa na Jumamosi, na saa 10:10 jioni siku ya Jumapili.

◼ Maegesho: Katika sehemu zote za makusanyiko zenye maegesho yanayolindwa, sehemu za kuegesha zitapatikana pasipo malipo. Wale watakaofika kwanza, ndio watakaopata mahali pa kuegesha kwanza. Beji za kusanyiko zitatumiwa kama vitambulisho ili kupata mahali pa kuegesha.

◼ Kuhifadhi Viti: Unaweza kuhifadhi viti kwa ajili ya wale tu wanaosafiri pamoja nawe katika gari moja, au wanaoishi pamoja nawe katika nyumba moja.

◼ Michango: Kupanga kusanyiko la wilaya hugharimu pesa nyingi. Tunaweza kuonyesha uthamini wetu kwa kutoa michango ya hiari kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote kwenye Jumba letu la Ufalme au kwenye kusanyiko.

◼ Wasio na Uwezo Mzuri wa Kusikia: Wale walio na matatizo ya kusikia wanapaswa kuijulisha halmashauri ya kusanyiko mapema ili wafanyiwe mpango wa kuketi mahali panapofaa.

◼ Chakula cha Mchana: Tafadhali bebeni chakula cha mchana, badala ya kuondoka mahali pa kusanyiko wakati wa mapumziko ya mchana kwenda kutafuta chakula. Sanduku dogo la kuhifadhi chakula kikiwa baridi, ambalo linaweza kutoshea chini ya kiti linaweza kutumiwa. Masanduku makubwa ya kuhifadhi baridi yanayotumiwa kwa ajili ya mandari, vyombo vya glasi, na pombe hairuhusiwi kusanyikoni.

◼ Kurekodi: Vifaa vyovyote vya kurekodi havipaswi kuunganishwa na mfumo wa umeme au wa sauti wa mahali pa kusanyiko navyo vyapaswa kutumiwa kwa njia ambayo haitawasumbua wengine.

◼ Kupiga Picha: Ukipiga picha, usitumie flashi vipindi vinapoendelea.

◼ Peja na Simu za Mkononi: Zipunguzwe sauti au kuzimwa ili zisiwakengeushe wasikilizaji.

◼ Aksidenti na Hali za Dharura: Hali ya dharura ya kimatibabu ikizuka kusanyikoni, tafadhali wasiliana na mkaribishaji aliye karibu, ambaye ataijulisha mara moja Idara ya Huduma ya Kwanza ili mtu anayestahili kutoa huduma ya kwanza aliyeko akague uzito wa hali hiyo na kutoa msaada unaohitajiwa.

◼ Mikahawa: Katika sehemu nyingi ni kawaida kutoa bakshishi ya asilimia 15-20, ikitegemea huduma.

◼ Hoteli: (1) Usihifadhi vyumba vingi kuliko utakavyohitaji, wala chumba kimoja kisikae watu wanaozidi idadi inayoruhusiwa. (2) Ukilazimika kufuta chumba ulichokuwa umeomba uhifadhiwe, ijulishe hoteli mara moja. (3) Usipike katika vyumba ambamo huruhusiwi kupika. (4) Mwachie mtunza-chumba bakshishi. (5) Usitumie vibaya kiamsha kinywa, kahawa, na barafu ambazo huandaliwa bure kwa ajili ya wale wanaokaa katika hoteli hiyo. (6) Onyesha matunda ya roho unaposhughulika na wafanyakazi wa hoteli, hasa wakati ambapo kuna wateja wengi wanaoingia na kutoka.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki