Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/07 kur. 4-5
  • Mfuateni Kristo kwa Kujiendesha kwa Heshima

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mfuateni Kristo kwa Kujiendesha kwa Heshima
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Pindi ya Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Endeleeni Kumtarajia Yehova
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko Kubwa
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 6/07 kur. 4-5

Mfuateni Kristo kwa Kujiendesha kwa Heshima

1 Biblia inamtaja Mwenye Enzi Kuu, Yehova, kuwa amevaa utukufu. (Zab. 104:1) Sikuzote Yesu alizungumza na kutenda kwa njia iliyomletea Baba yake utukufu na kuiheshimu kazi ya Baba yake. (Yoh. 17:4) Kila mmoja wetu atakuwa na fursa za kumwiga Yesu na kumletea Yehova utukufu wakati wa Kusanyiko la Wilaya la mwaka huu la “Mfuateni Kristo!”

2 Ibada Inayomletea Yehova Utukufu: Tunaweza kumletea Yehova utukufu kwa kufanya mipango ili tuwe kwenye karamu ya kiroho ambayo ametutayarishia. Je, umezungumza na mwajiri wako na kupanga mambo yako ili uhudhurie kila siku ya kusanyiko, kutia ndani Ijumaa? Je, umepanga kufika mapema vya kutosha ili kupata mahali pa kuketi na kushiriki katika wimbo na sala ya kufungua? Je, umefanya matayarisho yanayohitajiwa ili kula pamoja na ndugu zako katika mahali pa kusanyiko? Mwanzoni mwa kila kipindi wakati mwenyekiti anapotuomba tuketi kabla ya muziki kuanza, tunapaswa kumalizia mazungumzo yetu haraka na kuketi kabla ya programu kuanza.

3 Pia, kusikiliza programu kwa makini humletea Baba yetu wa mbinguni utukufu. Baada ya kuhudhuria kusanyiko la wilaya katika eneo la kwao, ripota mmoja aliandika kwamba mtu anayetazama angevutiwa na “mwenendo mzuri wa wahudhuriaji, huku wakiwa kimya na kusikiliza kwa makini yanayosemwa, wakionyesha kwamba wanapendezwa kikweli na mambo ya kiroho.” Pia alitaja “idadi kubwa ya watoto . . . , ambao kwa kushangaza wote walikuwa wenye adabu na hata wengine walifungua Biblia Takatifu.” Programu inapoendelea, si wakati wa kuongea isivyo lazima, kutuma ujumbe mfupi kupitia simu za mkononi, kula, au kutembea-tembea. Vijana wanapaswa kuketi na wazazi wao ili wazazi wawasaidie kufaidika na programu. (Kum. 31:12; Met. 29:15) Jitihada hizo huonyesha tunawaheshimu wengine na tunathamini chakula muhimu cha kiroho kinachoandaliwa.

4 Kuvalia na Kujipamba kwa Heshima: Wengi walithamini vikumbusho vya hotuba ya kusanyiko la wilaya la mwaka uliopita iliyokuwa na kichwa “Onyesha Heshima ya Kikristo Nyakati Zote,” ambayo ilikazia kwamba watumishi wa Mungu wanapaswa kujitahidi kuonyesha heshima ya Kikristo katika mavazi na mapambo yao. Mwaka huu pia tunapaswa kuzingatia sana jambo hilo. Mavazi na mapambo yetu yanaonyesha jinsi tunavyohisi kumwelekea Yehova na kuelekea pendeleo la kuwa Mashahidi wake. Sikuzote tuvalie kama wale “wanaodai kumheshimu Mungu.”—1 Tim. 2:9, 10.

5 Je, tuvalie na kujipamba kwa njia hiyo tunapokuwa kusanyikoni tu? Kumbuka kwamba wengi watatuona tukiwa tumevalia beji zetu za kusanyiko tutakapokuwa katika jiji la kusanyiko. Mavazi na mapambo yetu yanapaswa kututofautisha na watu wengine. Kwa hiyo, hata wakati wa mapumziko, kama vile jioni tunapoenda kula baada ya programu, tunapaswa kuvalia kama inavyostahili wahudumu wanaotembelea jiji hilo ili kuhudhuria kusanyiko la Kikristo. Hivyo hatupaswi kuvalia mavazi kama vile jinzi, suruali fupi, au fulana (yaani, T-shirt). Huo utakuwa ushahidi ulioje kwa wote wanaotutazama! Yehova hufurahi mavazi na mapambo yetu yanapotutambulisha kuwa wahudumu.

6 Matokeo Yenye Kuridhisha: Kuonyesha heshima ya Kikristo katika makusanyiko yetu hutokeza nafasi za kuhubiri isivyo rasmi na kuvutia wanaotutazama. Mwishoni mwa kusanyiko moja, ofisa mmoja alisema: “Hatujawahi kuona watu wenye mwenendo mzuri hivi. Mnajiendesha jinsi ambavyo Mungu anataka tujiendeshe.” Tunapojiendesha hivyo, tunaonyesha kwamba tunawaheshimu na kuwapenda wengine na hivyo kumletea Yehova utukufu. (1 Pet. 2:12) Tunaonyesha kwamba tunamheshimu Mungu na tunathamini sana pendeleo letu la kufundishwa na Baba yetu. (Ebr. 12:28) Na tujitahidi kumletea Yehova utukufu tunapotazamia Kusanyiko la Wilaya la mwaka huu la “Mfuateni Kristo!”

[Maswali ya Funzo]

1. Kichwa cha kusanyiko la mwaka huu kinaonyeshaje jinsi tunavyoweza kumletea Yehova utukufu?

2. Matayarisho tunayofanya ili kuhudhuria kila kipindi yanamleteaje Yehova utukufu?

3. Kusikiliza programu kwa makini kunamleteaje Yehova utukufu?

4. Kwa nini tunapaswa kuvalia na kujipamba kwa heshima tunapokuwa kusanyikoni?

5. Tunapaswa kuvalia na kujipamba jinsi gani wakati wa mapumziko katika jiji la kusanyiko ili kumletea Yehova utukufu?

6. Ni matokeo gani mazuri tunayopata kwa kuonyesha heshima ya Kikristo?

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya

◼ Saa za Programu: Siku zote tatu programu itaanza saa 3:20 asubuhi. Milango itafunguliwa saa 2:00 asubuhi. Muziki wa Ufalme wa utangulizi unapoanza, sisi sote tunapaswa kuwa tumeketi ili programu ianze kwa njia ya heshima. Programu itaisha saa 11:05 jioni siku ya Ijumaa na Jumamosi, na saa 10:10 jioni siku ya Jumapili.

◼ Maegesho: Katika sehemu zote za makusanyiko ambapo tumeruhusiwa kuegesha magari, sehemu za kuegesha zitapatikana pasipo malipo. Wale watakaofika kwanza, ndio watakaopata mahali pa kuegesha kwanza. Beji za kusanyiko zitatumiwa kama vitambulisho ili kupata mahali pa kuegesha. Kwa kuwa kwa kawaida kuna tatizo la nafasi za kutosha kuegesha magari, kwa kadiri iwezekanavyo ingefaa watu kadhaa wasafiri pamoja katika gari moja badala ya kila mtu kuja na gari lake.

◼ Viti: Unaweza kuhifadhi viti kwa ajili ya wale tu wanaosafiri pamoja nawe katika gari moja, au wanaoishi pamoja nawe katika nyumba moja.

◼ Chakula cha Mchana: Tafadhali bebeni chakula cha mchana badala ya kuondoka mahali pa kusanyiko wakati wa mapumziko ili kwenda kutafuta chakula. Sanduku dogo la kuhifadhi chakula kikiwa baridi, ambalo linaweza kutoshea chini ya kiti kimoja linaweza kutumiwa. Masanduku makubwa ya kuhifadhi chakula kikiwa baridi, vyombo vya glasi, na pombe haviruhusiwi kusanyikoni.

◼ Michango: Kupanga kusanyiko la wilaya hugharimu pesa nyingi. Tunaweza kuonyesha uthamini wetu kwa kutoa michango ya hiari kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote kwenye Jumba letu la Ufalme au kwenye kusanyiko. Hundi zozote zitakazotolewa kusanyikoni zinapaswa kuandikwa jina la shirika linalotambuliwa kisheria katika nchi yenu.

◼ Aksidenti na Hali za Dharura: Hali ya dharura ya kimatibabu ikizuka kusanyikoni, tafadhali wasiliana na mkaribishaji aliye karibu, ambaye ataijulisha mara moja Idara ya Huduma ya Kwanza ili mtu anayestahili kutoa huduma ya kwanza achunguze hali hiyo na kutoa msaada unaohitajiwa. Ikihitajika, mtu anaweza kupelekwa hospitali iliyo karibu.

◼ Wasio na Uwezo Mzuri wa Kusikia: Programu itatangazwa kotekote katika eneo la kusanyiko kupitia mawimbi ya FM. Ili kufaidika na maandalizi hayo, utahitaji kubeba redio ndogo inayoweza kupokea mawimbi ya FM pamoja na vidude vya kusikilizia masikioni.

◼ Kurekodi: Vifaa vyovyote vya kurekodi havipaswi kuunganishwa na mfumo wa umeme au mfumo wa sauti wa kusanyiko, navyo vinaweza kutumiwa tu kwa njia ambayo haitawasumbua wengine.

◼ Marashi: Huenda makusanyiko mengine yakafanyiwa katika majumba ambako watu hutegemea tu mifumo fulani ili kupata hewa safi. Basi, litakuwa jambo la fadhili kuepuka kutumia marashi yenye harufu kali ambayo huenda yakawaathiri wale walio na matatizo ya kupumua au matatizo mengine kama hayo.—1 Kor. 10:24.

◼ Fomu za Kufuatia Upendezi: Tukikutana na mtu yeyote anayependezwa tunapohubiri isivyo rasmi wakati wa kusanyiko, tunapaswa kutumia fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) kutoa habari kuhusu mtu huyo. Wahubiri wanapaswa kuwa na fomu moja au mbili kusanyikoni. Fomu hizo zitapatikana pia kwenye Idara ya Vitabu ya kusanyiko. Fomu zilizojazwa zinaweza kuachwa kwenye Idara ya Vitabu ili zishughulikiwe au unaweza kumpa mwandishi wa kutaniko lenu unaporudi kutanikoni.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2005, uku. 6.

◼ Mikahawa: Katika sehemu nyingi, ni jambo la kawaida kutoa bakshishi ya kati ya asilimia 15 hadi 20, ikitegemea huduma iliyotolewa.

◼ Hoteli: (1) Tafadhali usihifadhi vyumba vingi kuliko utakavyohitaji, wala chumba kimoja kisikaliwe na watu wanaozidi idadi inayoruhusiwa. (2) Ikiwa hutatumia chumba ulichokuwa umehifadhiwa, julisha hoteli mara moja. (3) Chukua kigari cha kubebea mizigo wakati tu unapokihitaji, na ukirudishe mara unapomaliza kukitumia. (4) Usipike ndani ya vyumba ikiwa hairuhusiwi kufanya hivyo. (5) Kila siku mwachie bakshishi yule anayetunza chumba. (6) Tukiwa Wakristo, kwa kweli hatutatumia vibaya vitu vinavyotolewa bure kwenye hoteli kwa ajili ya wageni kama vile kiamsha-kinywa, kahawa, au barafu. (7) Nyakati zote onyesha matunda ya roho unaposhughulika na wafanyakazi wa hoteli. (8) Kukiwa na shida katika chumba chako, hakikisha unaijulisha Idara ya Mahali pa Kulala ukiwa kusanyikoni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki