Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/09 kur. 3-4
  • Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Pindi ya Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye Shangwe
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Siku Tatu za Kuburudishwa Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mfuateni Kristo kwa Kujiendesha kwa Heshima
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 6/09 kur. 3-4

Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?

1. Ni matayarisho gani yanayohusika katika kuandaa karamu?

1 Inachukua wakati mwingi kuandaa karamu. Ni lazima mtu anunue chakula, akipike vizuri, kisha akiandae. Upakuaji wa chakula pia unahitaji kupangwa vizuri. Isitoshe, ni lazima mahali pa karamu hiyo patayarishwe. Wageni pia lazima wajitayarishe, hasa ikiwa watasafiri kutoka mbali. Ingawa kazi inayohusika ni nyingi, kula mlo mtamu wenye lishe pamoja na marafiki na familia, ni jambo linalofurahisha sana. Hivi karibuni, Mashahidi wa Yehova duniani kote watakusanyika katika vikundi vikubwa kwa vidogo ili kufurahia karamu ya kiroho ambayo wanaitarajia kwa hamu, yaani, Kusanyiko la Wilaya la “Endeleeni Kukesha!” Kazi nyingi tayari imefanywa ili kutayarisha programu na mambo mengine. Sote tumealikwa. Ili tuweze kuhudhuria na kunufaika kikamili, sisi pia lazima tujitayarishe.—Met. 21:5.

2. Unahitaji kufanya nini ili uweze kuhudhuria vipindi vyote vya kusanyiko letu?

2 Nufaika Kikamili: Je, umeshafanya mipango ili uweze kuhudhuria vipindi vyote vya kusanyiko hili? Ikihitajika, zungumza na mwajiri wako na umwambie utahudhuria siku zote za kusanyiko, hata siku ya kwanza. Je, umefanya mipango ya usafiri na mahali pa kulala? Wazee wanapaswa kuhakikisha kwamba wagonjwa na walio wazee kwa umri, na pia ndugu wengine ambao huenda wakahitaji msaada, wameshughulikiwa.—Yer. 23:4; Gal. 6:10.

3. Kwa nini hatupaswi kuhudhuria kusanyiko la kimataifa ambalo hatujaalikwa kulihudhuria?

3 Maeneo fulani yatakuwa na makusanyiko ya kimataifa. Kumbuka kwamba makutaniko na wajumbe hususa wa nchi za nje wamealikwa kwenye makusanyiko hayo. Walipofanya mipango kuhusu makusanyiko haya, ndugu katika ofisi ya tawi walikadiria kwa makini idadi ya watu watakaoalikwa, wakifikiria idadi ya viti na vyumba vya hoteli vinavyoweza kupatikana. Kunaweza kuwa na msongamano wa watu ikiwa wahubiri watahudhuria kusanyiko la kimataifa ambalo hawajaalikwa kulihudhuria.

4. Ni vikumbusho gani vitakavyotusaidia kuwa tayari wakati programu inapoanza kila siku?

4 Jitayarishe kufika kusanyikoni mapema kila siku ili upate kiti kabla ya programu kuanza. Tumia dakika chache kabla ya kila kipindi kuanza ili upitie programu iliyochapwa. Jambo hilo litakusaidia kuutayarisha moyo wako kwa ajili ya habari zitakazozungumziwa. (Ezra 7:10) Mwenyekiti wa kipindi anapotangaza kuanza kwa muziki, furahia kuusikiliza na uwe tayari kushiriki kuimba wimbo wa kufungua, na pia sala.

5. Familia zetu zinaweza kunufaikaje kikamili na programu?

5 Watu wa familia wakiketi pamoja kusanyikoni, wazazi wanaweza kuhakikisha kwamba watoto wao wanasikiliza kwa makini. (Kum. 31:12) Wote wanatiwa moyo kufungua Biblia zao na kufuatana na msemaji kila anaposoma maandiko. Kuandika kifupi mambo yanayozungumziwa kutakusaidia kusikiliza kwa makini zaidi. Baadaye mambo uliyoandika yatakusaidia kukumbuka mambo makuu katika hotuba. Epuka kuzungumza isivyo lazima wakati wa programu au kuondoka mahali unapoketi. Ikiwa una simu, usiruhusu ikukengeushe wala iwakengeushe wengine wakati wa programu. Baada ya vipindi vya kila siku, zungumza na wengine kuhusu mambo uliyofurahia katika programu.

6. Makusanyiko yetu yanatupa nafasi gani ya pekee, na tunaweza kuifurahiaje kikamili?

6 Kwenye kusanyiko la wilaya, tuna nafasi ya kufurahia ushirika wa kirafiki pamoja na ndugu na dada zetu ambao hatuwezi kuupata katika ulimwengu. (Zab. 133:1-3; Marko 10:29, 30) Wakati wa mapumziko ya mchana jitahidi kuzungumza na kujuana na wale wanaoketi karibu nawe. Hii ni mojawapo ya faida zinazotokana na kubeba chakula chepesi cha mchana na kubaki mahali pa kusanyiko badala ya kwenda kula kwenye mkahawa. Hakikisha kwamba unatumia nafasi hiyo ili kutiana moyo na ndugu zako.—Rom. 1:11, 12.

7. Kwa nini tunapaswa kufikiria kwa makini nguo tutakazovaa?

7 Mavazi: Kumbuka kwamba Yehova aliwaamuru Waisraeli watengeneze upindo wenye nyuzinyuzi kwenye nguo zao, na kuweka uzi wa bluu juu ya upindo huo. (Hes. 15:37-41) Upindo huo uliwakumbusha kwamba walikuwa watu walioteuliwa kumwabudu Yehova. Leo, mavazi yetu yenye heshima na ya kiasi ambayo tunavaa makusanyikoni huonyesha kwamba sisi ni tofauti na watu wa ulimwengu. Yanatoa ushahidi mzuri kwa wanatuona hata tunapokula kwenye mikahawa baada ya programu. Kwa hiyo, fikiria kwa makini nguo utakazovaa.

8. Tunaweza kuwahubiria watu jinsi gani tunapokuwa kwenye jiji la kusanyiko?

8 Toa Ushahidi: Kwa kujitayarisha mapema, tunaweza kuwahubiria watu tunapokuwa katika jiji la kusanyiko. Ndugu mmoja aliyeenda kwenye mkahawa pamoja na mke wake baada ya programu alimwonyesha mhudumu wa mkahawa beji yake ya kusanyiko na kumwuliza: “Je, umewaona watu wengi wakiwa wamevaa beji kama hii?” Mhudumu huyo alisema kwamba amewaona, kisha akauliza kwa nini watu walikuwa wamevalia beji hizo. Ndugu huyo alizungumza naye na kumwalika kwenye kusanyiko.

9. Tunaweza kuonyeshaje uthamini kwa Yehova ambaye ametualika kwenye karamu ya kiroho?

9 Ingawa ndugu zetu ndio watakaotoa hotuba zote na kufanya mahojiano na maonyesho, Baba yetu wa mbinguni, Yehova, ndiye anayeandaa kwa upendo karamu hii ya kiroho ya kila mwaka. (Isa. 65:13, 14) Tunaonyesha uthamini wetu kwa Yule ambaye ametualika kwa kuhudhuria siku zote na kuthamini chakula cha kiroho kinachoandaliwa. Je, umefanya mipango ya kuhudhuria karamu hii?

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya

◼ Saa za Programu: Siku zote tatu, programu itaanza saa 3:20 asubuhi. Milango itafunguliwa saa 2:00 asubuhi. Muziki wa kuanza programu unapotangazwa, sote tunapaswa kuwa tumeketi ili programu ianze kwa utaratibu unaomletea Yehova heshima. Programu itaisha saa 10:55 jioni siku ya Ijumaa na Jumamosi, na saa 10:00 jioni siku ya Jumapili. Programu ya makusanyiko ya kimataifa itaanza Alhamisi saa 7:20 adhuhuri na kuisha saa 10:45 jioni.

◼ Maegesho: Katika sehemu zote za makusanyiko ambapo tumeruhusiwa kuegesha magari, sehemu za kuegesha zitapatikana bila malipo. Wale watakaofika kwanza, ndio watakaopata mahali pa kuegesha kwanza. Walemavu tu ndio watakaoruhusiwa kuegesha magari yao mahali palipotengewa walemavu. Kwa kuwa kwa kawaida nafasi za kuegeshea magari hazitoshi, ingefaa sana watu wasafiri pamoja kwa gari moja, badala ya kila mmoja kuja kwa gari lake.

◼ Viti: Unaweza kuhifadhi viti kwa ajili ya wale tu wanaosafiri pamoja nawe katika gari moja, au wanaoishi pamoja nawe katika nyumba moja.

◼ Chakula cha Mchana: Tafadhali beba chakula cha mchana badala ya kuondoka mahali pa kusanyiko wakati wa mapumziko ili kwenda kutafuta chakula. Sanduku dogo la kuhifadhia chakula ambalo linaweza kutoshea chini ya kiti linaweza kutumiwa. Masanduku makubwa ya kuhifadhia chakula na vyombo vya glasi haviruhusiwi kusanyikoni.

◼ Michango: Tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini mipango ya kusanyiko kwa kutoa michango ya hiari kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote kwenye Jumba letu la Ufalme au kwenye kusanyiko. Hundi zozote zinazotolewa kusanyikoni zinapaswa kuandikwa jina la shirika letu la kisheria.

◼ Aksidenti na Hali za Dharura: Hali ya dharura ya kimatibabu ikitokea kusanyikoni, tafadhali wasiliana na mkaribishaji aliye karibu, ambaye ataijulisha mara moja Idara ya Huduma ya Kwanza ili mtu anayestahili kutoa huduma ya kwanza achunguze hali hiyo na kutoa msaada unaohitajiwa. Wafanyakazi wa huduma ya kwanza wataamua jambo la kufanya.

◼ Viatu: Kila mwaka watu kadhaa hujeruhiwa kwa sababu ya viatu. Kwa hiyo, ni vizuri kuvaa viatu vya kawaida, vinavyokutoshea vizuri na vinavyokuwezesha kutembea kwenye ngazi, viunzi vya chuma, na maeneo mengine, bila kujikwaa.

◼ Kurekodi: Vifaa vya kurekodi havipaswi kuunganishwa kwenye mfumo wa umeme au wa sauti. Vinaweza kutumiwa tu kwa njia ambayo haitawasumbua wengine.

◼ Vigari vya Kuwabebea Watoto na Viti vya Bustanini: Vigari vya kuwabebea watoto na viti vya bustanini havipaswi kuletwa kusanyikoni. Hata hivyo, viti vya watoto vinavyoweza kufungwa kwenye kiti karibu na wazazi vinakubalika.

◼ Marashi: Makusanyiko mengine hufanywa katika majumba ambamo mifumo ya kusafisha hewa hutumiwa kuingiza hewa safi. Basi, litakuwa jambo la fadhili kuepuka kutumia marashi yenye harufu kali ambayo huenda yakawaathiri wale walio na matatizo ya kupumua au matatizo mengine kama hayo.—1 Kor. 10:24.

◼ Fomu za Kufuatia Upendezi: Ukikutana na mtu yeyote anayependezwa tunapohubiri wakati wa kusanyiko, unapaswa kutumia fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) kutoa habari kumhusu mtu huyo. Wahubiri wanapaswa kubeba fomu moja au mbili kusanyikoni. Fomu zilizojazwa zinaweza kuachwa kwenye Idara ya Vitabu ili zishughulikiwe au unaweza kumpa mwandishi wa kutaniko lenu unaporudi nyumbani.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2005, uku. 6.

◼ Mikahawa: Fanya jina la Yehova liheshimiwe kupitia mwenendo wako mzuri kwenye mikahawa. Katika sehemu nyingi, ni jambo la kawaida kutoa bakshishi ya asilimia 15 hadi 20, ikitegemea huduma iliyotolewa.

◼ Hoteli: (1) Tafadhali usihifadhi vyumba vingi kuliko utakavyohitaji, wala chumba kimoja kisikaliwe na watu wanaozidi idadi inayoruhusiwa. (2) Ikiwa hutatumia chumba kilichokuwa kimehifadhiwa kwa ajili yako, julisha wasimamizi wa hoteli mara moja. (3) Usipike ndani ya vyumba ikiwa hairuhusiwi kufanya hivyo. (4) Kila siku, mwachie bakshishi yule anayetunza chumba. (5) Fuata vizuri mpango wa hoteli kuhusu kiamsha-kinywa, kahawa, au barafu ambazo huandaliwa kwa ajili ya wageni. (6) Nyakati zote, onyesha matunda ya roho unaposhughulika na wafanyakazi wa hoteli. Wanawahudumia watu wengi sana na wanathamini tunapokuwa wenye fadhili, subira, na kiasi. (7) Kukiwa na shida katika chumba chako hotelini, ijulishe Idara ya Mahali pa Kulala ukiwa kusanyikoni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki