Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/04 uku. 6
  • Iga Mtazamo wa Akili wa Yesu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Iga Mtazamo wa Akili wa Yesu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Dhihirisha Mtazamo wa Akili wa Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Mwige Yesu kwa Kuwatumikia Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Upendo wa Kristo Unatuchochea Kupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 4/04 uku. 6

Iga Mtazamo wa Akili wa Yesu

1 Ingawa hatujawahi kumwona Yesu, Mwana wa Mungu, tumekuja kumpenda kikweli kwa kusoma maandishi yanayohusu maisha na huduma yake. (1 Pet. 1:8) Alitii mapenzi ya Baba yake, akaacha cheo chake kikubwa mbinguni na kuja duniani. Akiwa mwanadamu, aliwatumikia wengine bila ubinafsi na kutoa uhai wake kwa ajili ya wanadamu. (Mt. 20:28) Neno la Mungu linatuhimiza hivi: “Iweni na mtazamo huu wa akili ndani yenu ambao ulikuwa pia ndani ya Kristo Yesu.” Tunaweza kuigaje roho yake ya kujidhabihu?—Flp. 2:5-8.

2 Tunapochoka: Ingawa alikuwa mkamilifu, Yesu alichoka. Pindi moja, alimhubiria mwanamke Msamaria hata ingawa alikuwa “amechoka kwa sababu ya safari.” (Yoh. 4:6) Wakristo wengi leo hukumbwa na tatizo hilohilo. Baada ya juma lenye kuchosha kazini, huenda isiwe rahisi kwenda kuhubiri. Hata hivyo, tukihubiri kwa ukawaida, huduma ya Kikristo itatuburudisha kiroho.—Yoh. 4:32-34.

3 Pindi nyingine, Yesu na wanafunzi wake walienda mahali pasipo na watu ili kupumzika kidogo. Hata hivyo, umati mkubwa ulipata habari ukakimbia mbele ili kukutana nao. Badala ya kuudhika, Yesu ‘aliwasikitikia’ akaanza “kuwafundisha mambo mengi.” (Marko 6:30-34) Tunahitaji kuwa na mtazamo huo ili kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia. Tunahitaji kuendelea kutia bidii na kuwapenda watu kikweli. Ikiwa kwa sasa huongozi funzo la Biblia, usichoke kutafuta angalau funzo moja.

4 Tanguliza Mambo ya Kiroho: Upainia msaidizi unaweza kutusaidia kukazia fikira zaidi mambo ya kiroho. Dada mmoja kijana aliandika hivi: “Mama ya rafiki yangu alitutia moyo kufanya upainia msaidizi pamoja naye kwa mwezi mmoja. Ninafurahi sana kwamba tulijiunga naye. Nilifurahi kuwajua vizuri zaidi akina ndugu na dada, na muda si muda niliwaona kama washiriki wa familia yangu. Nilifurahi pia kuwa na nafasi zaidi ya kuwahubiria wengine kumhusu Yehova na kuwafundisha kweli nzuri za Ufalme. Mambo hayo yote yalinisaidia kumkaribia zaidi Yehova na tengenezo lake.”—Zab. 34:8.

5 Sote tuna miili isiyo mikamilifu ambayo hupambana na tamaa yetu ya kumpendeza Yehova. (Rom. 7:21-23) Lazima tushinde roho ya ulimwengu ya kutojidhabihu. (Mt. 16:22, 23) Yehova anaweza kutusaidia tufaulu kupitia roho yake takatifu. (Gal. 5:16, 17) Tunapongojea kukombolewa na kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu, na tuige mtazamo wa akili wa Yesu kwa kutanguliza mambo ya Ufalme na mapendezi ya wengine.—Mt. 6:33; Rom. 15:1-3.

[Maswali ya Funzo]

1. Yesu alikuwa na mtazamo gani wa akili?

2. Wakristo wengi hukumbwa na tatizo gani, na ni nini kinachoweza kuwasaidia kulishinda?

3. Tunaweza kuigaje nia ya Yesu ya kutaka kufundisha?

4. Upainia msaidizi unawezaje kutusaidia kuiga mtazamo wa akili wa Kristo?

5. Kwa nini ni lazima tuendelee kujitahidi kuiga mtazamo wa akili wa Yesu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki