Kutoa Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
◼ “Je, unafikiri ulimwengu ungekuwa mahali pazuri ikiwa watu wangefuata maneno haya? [Soma Mathayo 7:12a. Kisha ngoja jibu.] Kitabu hiki kina mafunzo mengi kutoka kwa mwalimu mkuu zaidi aliyewahi kuishi.” Kazia picha na maelezo yaliyo kando ya picha kwenye sura ya 17.
◼ “Wazazi wengi leo hujaribu kuwafundisha watoto wao maadili mazuri. Je, unafikiri ni muhimu kufanya hivyo? [Ngoja jibu. Kisha soma Methali 22:6.] Ona kwamba wazazi wanatiwa moyo kuanza kuwafundisha watoto wao wakiwa bado wachanga. Kitabu hiki kimekusudiwa kuwasaidia kufanya hivyo.” Kazia picha na maelezo yaliyo kando ya picha kwenye sura ya 15, 18, au 32.
◼ “Mara nyingi, wazazi hushangazwa na maswali ambayo watoto wao huuliza. Si rahisi kujibu baadhi ya maswali hayo, sivyo? [Ngoja jibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:14, 15.] Mama na nyanya ya Timotheo walimfundisha Maandiko tangu utotoni. Kitabu hiki kinaweza kuwasaidia wazazi wawafundishe watoto wao vivyo hivyo leo.” Kazia picha chache na maelezo yake kwenye sura ya 11 na 12 au 34 mpaka 36.