Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/04 uku. 1
  • Kusanyiko la Wilaya Latuchochea Kutembea Pamoja na Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusanyiko la Wilaya Latuchochea Kutembea Pamoja na Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Utatembea Pamoja na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Karibuni Kwenye Kusanyiko la Wilaya la “Tembea Pamoja na MUNGU”
    Amkeni!—2004
  • Kutembea Pamoja na Mungu—Hatua za Mwanzo-Mwanzo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • “Njia za Yehova Zimenyooka”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 10/04 uku. 1

Kusanyiko la Wilaya Latuchochea Kutembea Pamoja na Mungu

Kusanyiko la Wilaya la “Tembea Pamoja na Mungu” lilitukumbusha agizo hili la Yehova lililo wazi: “Hii ndiyo njia. Tembeeni ndani yake”! (Isa. 30:21) Kufuata maagizo tuliyopata kutatusaidia ‘kuangalia sana jinsi tunavyotembea.’ (Efe. 5:15) Kutafakari mambo tuliyojifunza kutatusaidia ‘kuendelea kutembea katika kweli.’—3 Yoh. 3.

Tumia maswali yanayofuata pamoja na mambo uliyoandika ili kujitayarisha na kushiriki katika pitio la programu ya kusanyiko la mwaka huu. Pitio hilo litafanywa katika Mkutano wa Utumishi wa juma la Oktoba 18.

1. Enoko aliwezaje kutembea pamoja na Mungu ijapokuwa alikuwa akiishi katika nyakati za msukosuko? (Ebr. 11:1, 5, 6; Yuda 14, 15; “Tembea Pamoja na Mungu Nyakati za Msukosuko”)

2. Kanuni ya Luka 16:10 inaweza kutumiwa katika mambo gani maishani? (“Je,Wewe Ni ‘Mwaminifu Katika Lililo Dogo Zaidi’?”)

3. (a) Taja mambo manne tunayojifunza katika Hosea sura ya 6 hadi 9 ambayo yatatusaidia kutembea pamoja na Mungu. (Hos. 6:6, 7; 7:14; 8:7) (b) Ni mambo gani mengine katika Hosea sura ya 10 hadi 14 yanayotusaidia kutembea pamoja na Mungu? (“Unabii wa Hosea Hutusaidia Kutembea Pamoja na Mungu”—Mfululizo)

4. Ni mambo gani ambayo mume na mke wanaweza kufanya ili kuimarisha ndoa yao? (Met. 12:4; Efe. 5:29; “Usitenganishe ‘Kile Ambacho Mungu Ameunganisha’”)

5. Tunaonyeshaje kwamba tunaheshimu mikusanyiko yetu mitakatifu? (Mhu. 5:1; Isa. 66:23; “Kuheshimu Mikusanyiko Yetu Mitakatifu”)

6. (a) Ni mambo gani matatu muhimu tunayopaswa kuchanganua ili kuhakikisha kwamba tunashiriki kikamili katika kazi yetu ya kuhubiri? (Isa. 52:7; Zek. 8:23; Marko 6:34) (b) Ni mambo gani yaliyo katika kijitabu Good News for People of All Nations yatakayokusaidia? (“Habari Njema kwa Watu wa Mataifa Yote”; “Kuwasaidia Wale Wanaoongea Lugha Nyingine”)

7. Tunawezaje kuwasaidia wapya wawe na ujasiri wanapohubiri ujumbe wa Ufalme? (Amu. 7:17; “Kuwasaidia Wengi Kujiunga Nasi Katika Huduma”)

8. Tunaonyeshaje kuwa tunasadiki “siku kuu ya Yehova iko karibu”? (Sef. 1:14; “Tunatembea kwa Imani, Si kwa Kuona”)

9. (a) Kukwazika au kuwakwaza wengine ni jambo zito kadiri gani? (Marko 9:42-48) (b) Tunawezaje kuepuka kukwazika? (Zab. 119:165) (c) Tunawezaje kuepuka kuwakwaza wengine? (1 Kor. 10:24; “Epuka ‘Sababu Yoyote ya Kukwaza’”)

10. Tunawezaje kudumisha usawaziko wetu tunapotafuta mwenzi wa ndoa, kuhangaikia afya nzuri, na katika mambo ya kibiashara? (Zab. 26:4; Mt. 6:25; 1 Tim. 6:9; “Tunzeni Akili Zenu kwa Ukamili”)

11. (a) Yesu alitendaje alipoalikwa na wengine? (Luka 10:42; 24:32) (b) Tunawezaje kufurahia tafrija kwa njia inayotuburudisha na kuwaburudisha wengine? (1 Kor. 10:31-33; “Utendaji Unaojenga na Kuburudisha”)

12. Kulingana na Zaburi ya 23, tunapata baraka gani tukiwa kondoo wa Yehova, nasi tuna wajibu gani? (1 Kor. 10:21; “Yehova Ni Mchungaji Wetu”)

13. Wakristo hutiije shauri lililoongozwa na roho ya Mungu kuhusu ‘kujinunulia wakati unaofaa’? (Efe. 5:16; “Kununua Wakati Unaofaa”)

14. (a) “Saa ya hukumu” inayotajwa katika Ufunuo 14:7 inahusisha nini? (b) Tunaonyeshaje kwamba kwa kweli sisi si sehemu ya Babiloni Mkubwa? (“‘Endeleeni Kukesha’—Saa ya Hukumu Imefika”) (c) Ni nini ambacho kimekufurahisha katika broshua Endeleeni Kukesha!?

15. Taja sifa tatu zinazohitajiwa ili kuepuka ‘kuiacha njia iliyo nyoofu.’ (2 Pet. 2:15; “Jilinde ‘Usiiache Njia Iliyo Nyoofu’”)

16. Vijana wanawezaje kuepuka “njia ya wabaya”? (Met. 4:14; “Enyi Vijana, Tembeeni Katika Njia ya Uadilifu”)

17. (a) Paulo alikuwa mfano bora wa uvumilivu katika njia zipi? (Mdo. 14:19, 20; 16:25-33) (b) Kwa nini hatuhitaji kuogopa wale wanaopinga ibada ya kweli? (Drama na hotuba “Toa Ushahidi Kamili Leo Licha ya Upinzani”)

18. Wale wanaotembea pamoja na Mungu hupata baraka zipi? (“Kutembea Pamoja na Mungu Huleta Baraka Sasa na Milele”)

Na tuazimie kutii ‘neno lililo nyuma yetu’ ili tutembee milele na Baba yetu wa mbinguni.—Isa. 30:21; Yoh. 3:36.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki