Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/04 uku. 4
  • Sehemu ya 3: Kutumia Maandiko kwa Matokeo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sehemu ya 3: Kutumia Maandiko kwa Matokeo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kazia Uangalifu ‘Ufundi Wako wa Kufundisha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 11/04 uku. 4

Sehemu ya 3: Kutumia Maandiko kwa Matokeo

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

1 Kusudi letu la kuongoza mafunzo ya Biblia ni ‘kufanya wanafunzi’ kwa kuwasaidia watu waelewe na kukubali mafundisho ya Neno la Mungu, kisha kuyatumia maishani mwao. (Mt. 28:19, 20; 1 The. 2:13) Kwa hiyo, tunapaswa kukazia Maandiko tunapoongoza funzo. Mwanzoni, huenda ikafaa kuwaonyesha wanafunzi jinsi ya kutafuta maandiko katika Biblia zao. Hata hivyo, tunawezaje kutumia Maandiko kuwasaidia wanafunzi hao wafanye maendeleo ya kiroho?

2 Chagua Maandiko ya Kusoma: Unapojitayarisha, chunguza jinsi kila andiko lililotajwa bila kunukuliwa linavyohusiana na jambo linalozungumziwa, kisha uamue ni yapi utakayosoma na kuzungumzia wakati wa funzo. Kwa kawaida, itafaa kusoma yale yanayoonyesha msingi wa imani yetu. Si lazima usome maandiko yanayotoa habari za ziada. Fikiria mahitaji na hali za kila mwanafunzi.

3 Tumia Maswali: Badala ya kumfafanulia mwanafunzi maandiko ya Biblia, mwache yeye akufafanulie. Unaweza kumchochea afanye hivyo kwa kutumia maswali kwa ustadi. Ikiwa maana na matumizi ya andiko ni wazi, unaweza kumwuliza jinsi andiko hilo linavyounga mkono jambo linalozungumziwa kwenye fungu. Kuhusu maandiko mengine, huenda ukahitaji kuuliza swali fulani hususa au maswali kadhaa ili kumsaidia mwanafunzi apate kuelewa maana ya maandiko hayo. Ikiwa unahitaji kueleza zaidi, unaweza kufanya hivyo baada ya mwanafunzi kutoa maelezo yake.

4 Usieleze Mambo Mengi: Mara nyingi mpiga-mishale stadi huhitaji kutumia mshale mmoja tu ili kulenga shabaha. Vivyo hivyo, mwalimu stadi hahitaji kutumia maneno mengi ili kukazia jambo fulani. Anaweza kueleza jambo kwa njia rahisi, iliyo wazi, na sahihi. Huenda wakati mwingine ukahitaji kufanya utafiti katika vichapo vya Kikristo ili kuelewa andiko fulani na kulieleza kwa usahihi. (2 Tim. 2:15) Lakini epuka kujaribu kueleza kila jambo katika andiko wakati wa funzo. Eleza tu yale yanayohusiana na jambo linalozungumziwa.

5 Onyesha Jinsi ya Kutumia Maandiko: Inapofaa, msaidie mwanafunzi aone jinsi anavyoweza kutumia maandiko katika maisha yake. Kwa mfano, unapozungumzia andiko la Waebrania 10:24, 25 pamoja na mwanafunzi ambaye bado hajaanza kuhudhuria mikutano ya Kikristo, unaweza kutaja mojawapo ya mikutano na kumwalika ahudhurie. Usifanye mwanafunzi ahisi kama analazimishwa kuhudhuria. Badala yake, acha Neno la Mungu limchochee kuchukua hatua inayohitajiwa ili kumpendeza Yehova.—Ebr. 4:12.

6 Tunapotimiza kazi yetu ya kufanya wanafunzi, na ‘tuendeleze utii kwa njia ya imani’ kwa kutumia Maandiko kwa matokeo.—Rom. 16:26.

[Maswali ya Funzo]

1. Kwa nini tukazie Maandiko tunapoongoza mafunzo ya Biblia?

2. Tuamueje maandiko ya kusoma na kuzungumzia?

3. Kuna manufaa gani kutumia maswali, nasi tunawezaje kufanya hivyo?

4. Ni maelezo mengi kadiri gani yanayohitajiwa kuhusu maandiko tunayosoma?

5, 6. Tunawezaje kuwasaidia wanafunzi watumie Neno la Mungu katika maisha zao, lakini tunapaswa kuepuka nini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki